Hii mada iliishawahi kuwekwa humu lakini sijui ni jukwaa gani ila niliiona ni kawaida tu, sasa yamenikuta mimi ndio nimeshtuka na kuona sio ya kawaida. Nilikuwa natafuta kitu kwenye mkoba wa mpenzi wangu, hamadi KY Gel tena ipo nusu kwenye mkopa wa mpenzi wangu. Hajui kama nimeiona maana hayupo, ila mkoba wake upo nyumbani kwangu. Nipeni ushauri nianzie wapi kumuuliza ni ya nini hiyo KY Gel?