Kwetu sisi waislamu, tunaamini umasikini ni dalili ya kiama

BAKIIF Islamic

JF-Expert Member
Jul 11, 2021
594
1,827
Inafahamika kuwa umasikini ni ukosefu wa chakula, makazi, mavazi, huduma za afya na mahitaji mengine ya msingi kwa sababu ya kipato duni. Licha ya fursa zinazopatikana kutokana na maendeleo ya teknolojia, umasikini hivi leo ni moja kati ya matatizo makubwa kabisa yanayoukabili ulimwengu. Katika mabara ya Afrika, Asia, Amerika Kusini na Ulaya Mashariki watu wengi wanahangaika na njaa kila siku.

Kwa sababu ya mgao mbaya wa rasilimali za ulimwengu umasikini umesababisha uwepo mgawanyiko kati ya nchi za kaskazini ya jangwa la sahara ambazo ni za ulimwengu wa kwanza na nchi za kusini maskini ambazo ni za ulimwengu wa tatu.

Ubeberu na Ubepari usio na mipaka unazuia mgawanyo wa kipato ulimwenguni kote na unakwaza maendeleo ya nchi changa na nchi zinazoendelea. Wakati ambapo kuna watu wachache wanaofurahia kipato kinachozidi mahitaji yao, kuna idadi kubwa ya watu wanaohangaika na matatizo ya umasikini na ufukara. Katika Ulimwengu wa leo umasikini umefikia hatua mbaya au kiwango kibaya sana.

Haya yote, Mtume (s.a.w.w) aliyasema juu ya kuongezeka kwa umasikini. ''Umasikini na njaa ni miongoni mwa dalili za kipindi cha kwanza cha zama za mwisho:'' ''Masikini wataongezeka.'' ''Kipato kitagawanywa kwa matajiri tu, hakuna mafao kwa masikini.''

Ni dhahiri kuwa kipindi hicho kilichobashiriwa na Mtume (s.a.w.w) kinawiana na hali ya wakati wetu wa leo. Tukiangalia karne zilizopita tunaona kuwa shida na tabu zilizoletwa na ukame, vita na majanga mengine zilikuwa za muda mfupi na ziliishia katika eneo moja moja. Lakini umasikini na shida za leo ni za kudumu na sugu. Kwa hakika Mola wetu ni Mwingi wa Rehma, yeye hadhulumu watu lakini kwa sababu ya ukosefu wa shukurani wa wanadamu na maovu wanayoyafanya, umasikini na tabu vimeongezeka. Kwa hakika hali ya mambo ya kusikitisha inaonesha wazi kuwa dunia imetanzwa na uchoyo na ubinafsi.


poverty-in-africa-ethiopian-classroom.jpg
 
Tafuta pesa mkuu hizo hadithi zipo mababu na mababu usitake kuhalalisha umasikini kwa kigezo cha dini
Wapo watu waliamini thamani zao zipo katika pesa hivyo wakazitafuta kwa nguvu zote, katika maandishi yangu hapo hakuna neno hata moja linalo sema ''Pesa''. Mimi nimezungumzia umasikini na wala sijazungumzia pesa, unaweza ukawa na pesa lakini bado ukawa masikini.

Ukitaka kujua umaskini ni nini, inabidi kwanza ujue kutokuwa maskini ni nini? Uwezo wa kumudu maisha ya chini kabisa (yaani kupata chakula kizuri, malazi mazuri, elimu, mavazi na usafiri mzuri na wa hakika), kuwa na uhakika wa kupata matibabu mazuri unapoumwa, uwe na uhakika wa kupata mapumziko na burudani baada ya kazi, uwe na uhakika wa maisha yako na kupata mahitaji hayo kwa walau mwaka mmoja. Hapo unaweza kusema kuwa wewe sio maskini. Kama huwezi kupata hayo basi upo kwenye kundi la maskini au unakaribia kwenye kundi la umaskini.

Mazingatio ni kwamba: Ukiona wewe umeyamudu hayo lakini katika ndugu zako kuna ambao wanahangaika na hayo, elewa bado upo kwenye kundi la umasikini hata kama una mabox ya pesa ndani kwako.
 
Nasema tafuta pesaa
Pesa kila mtu anayo ndugu, hakuna asiyekuwa na pesa. Pesa inahitaji matunzo na sio kutafutwa, kwasababu inasifa ya kuja na kuondoka. Pesa inatafuta watu nasio watu wanatafuta pesa. || Mimi nazungumzia umasikini kwamba ni dalili ya kiama sijazungumzia pesa, tofautisha hayo mambo ewe mtafuta pesa zisizopatikana.
 
Science imetoa majibu mengi sana ya maswali katika dunia ya leo kuliko dini...kimsingi dini ni ulevi kama ilivyo ulevi wa bangi na madawa mengine.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
Sayansi haiwezi kwenda bila dini, na pia bila sayansi punde tu dini itaharibika na kuwa ushirikina, sayansi bila dini inakuwa chombo tu cha ulaji wa kawaida– na maendeleo ya kimwili yasiyo thibitiwa hayawezi kutupeleka kwenye ufanisi wa kweli.

Sayansi na dini vyote viwili vinaeleza uhalisi mmoja, na uhalisi ni mmoja. Haiwezekani kwamba kitu kikawa siyo sahihi kisayansi na kikawa cha kweli kidini. Mikanganyiko inatokana na mapungufu ya kiutu. Sayansi inazifunda akili zetu kugundua halisi zilizofichwa. Dini inatusaidia kugundua maana na matumizi sahahi ya uvumbuzi wa kisayansi.
Dini inatoa majibu kwa yale maswali ya kimaadili, ya kusudi la kiutu, na uhusiano wetu na Mungu ambao sayansi haiwezi kuufikia. Kutambua asili ya upatano na ukamilisho wa sayansi na dini, hapo ndipo jamii ya kiutu inaweza kusogea mbele kwa usalama.
 
Hiyo bila shaka Mtume SAW aliongea akiwa abnormal.
Dunia ya sasa life span inakuwa kwaajili ya maendeleo ya Sayansi na teknolojia, wakati tunapata Uhuru nyumba za bati zilikuwa za kuhesabika, miaka 100 nyuma Watanganyika wengi walikuwa na nguo pea moja au mbili tu.
Miaka ya 2000 kurudi nyuma Dodoma, Lindi, Singida n.k watu wengi tu walikuwa wakifa miezi ya Desemba hadi Machi kwasababu ya njaa leo hii karibu kila nyumba wanatia mafuta mboga ndipo wale.
Leo hii watu wana fedha mpaka wanaonunua simu za Malaki.
Note: Dunia haiwezi kurudi nyuma kimaendeleo
 
Umasikini ni kama jela, sasa kuna kiama kingine zaidi ya Umaskini mkuu???
Ni sahihi ndugu, ndio maana ''Qur'an'' inasisitiza wenye mali kuwasaidia masikini., kwasababu umasikini ni janga, “na chochote mtakachokitoa atakibadilisha; Naye ndiye mbora wa wanaoruzuku” (Ch 34:39). Quran pia inaamrisha sehemu ya masikini katika mali ya mtu na inawashauri Waislamu kutumia mali zao kwa ajili ya ustawi wa umma kwa ujumla. Na sio ubinafsi na ubadhirifu.
 
Hiyo bila shaka Mtume SAW aliongea akiwa abnormal.
Dunia ya sasa life span inakuwa kwaajili ya maendeleo ya Sayansi na teknolojia, wakati tunapata Uhuru nyumba za bati zilikuwa za kuhesabika, miaka 100 nyuma Watanganyika wengi walikuwa na nguo pea moja au mbili tu.
Miaka ya 2000 kurudi nyuma Dodoma, Lindi, Singida n.k watu wengi tu walikuwa wakifa miezi ya Desemba hadi Machi kwasababu ya njaa leo hii karibu kila nyumba wanatia mafuta mboga ndipo wale.
Leo hii watu wana fedha mpaka wanaonunua simu za Malaki.
Note: Dunia haiwezi kurudi nyuma kimaendeleo
Unadhani wakati huo nchi zingine zilikuwa na maendeleo gani ?

Ripoti ya mwisho ya UNICEF ilieleza kuwa mmoja kati ya kila watu wanne duniani anaishi katika tabu na shida isiyoelezeka. Watu bilioni 1.3 duniani wanaishi kwa wastani wa chini ya dola moja kwa siku. Watu bilioni 3 duniani wanaishi kwa dola mbili kwa siku. Takribani watu bilioni 1.3 hawapati maji safi. Watu bilioni 2.6 hawapati maji salama.

Kwa mujibu wa ripoti ya shirika la chakula duniani, (FAO) , Mwaka 2000, watu milioni 826 duniani kote hawapati chakula cha kutosha. Kwa maneno mengine mmoja katika kila watu sita ana njaa. Katika miaka kumi iliyopita dhulma katika mgawanyo wa kipato imeongezeka kwa kiwango kisichosemeka.

Ripoti za umoja wa Mataifa zinaonesha kuwa, katika mwaka 1960 asilimia 20 (20%) ya watu wanaoishi katika nchi tajiri kabisa duniani walikuwa na pato lilozidi mara thelathini pato la nchi 20 masikini kabisa. Hadi kufikia mwaka 1995 iliongezeka mara 82. Kikiwa ni kielezeo cha kutoweka kwa haki ulimwenguni, mali za matajiri 225 wakubwa kabisa ulimwenguni ni sawa na pato la mwaka la asilimia 47 (47%) ya nchi masikini ulimwenguni.

Takwimu za sasa zinaonyesha yale ambayo Mtume (s.a.w.w) aliyasema juu ya kuongezeka kwa umasikini. Katika hadithi inabainishwa kuwa umasikini na njaa ni miongoni mwa dalili za kipindi cha kwanza cha zama za mwisho.
 
ila waislam mna amini vitu vingi vya ajabu ajabu na visivyo wezekana………...
Mtume (s.a.w.w) alisema juu ya kuongezeka kwa umasikini kutokana na maovu ya watu. Katika hadithi inabainishwa kuwa umasikini na njaa ni miongoni mwa dalili za kipindi cha kwanza cha zama za mwisho. Nasio kwamba tunaamini umasikini ni sehemu yetu laa! bali umasikini kukithiri duniani ni dalili za kiama, kama vile kukithiri kwa mauaji na uzinifu nazo ni dalili za kiama.
 
Pesa kila mtu anayo ndugu, hakuna asiyekuwa na pesa. Pesa inahitaji matunzo na sio kutafutwa, kwasababu inasifa ya kuja na kuondoka. Pesa inatafuta watu nasio watu wanatafuta pesa. || Mimi nazungumzia umasikini kwamba ni dalili ya kiama sijazungumzia pesa, tofautisha hayo mambo ewe mtafuta pesa zisizopatikana.​
Mkuu nimekuelewa sana ulichowasilisha ingawa watu wanalichukulia kimzaha kwa jinsi walivyotoa comments zao, absolute poverty limekuwa tatizo sugu zaidi hasa kwa nchi maskini hususan Asia na Africa miongo ya hivi karibuni na hii hali haionekani kuboreka, hasa ikichagizwa zaidi na janga la korona, mabadiliko ya tabia nchi nk. Chukulia mfano hapa Tanzania maskini wanazidi kuongezeka na hali ya vipato vya watu inazidi kuwa mbaya. Ninakubaliana pia kwamba kuna spiritual element kwenye hili tatizo kama ulivyolihusisha na unabii wa kiama wa Prophet Muhamad na maandiko hayo hayo ya kinabii pia yamo katika biblia kwa sisi wakristo ambayo yanaashiria hali ya dhiki kuu kuelekea mwisho wa dunia.​
 
Mtume (s.a.w.w) alisema juu ya kuongezeka kwa umasikini kutokana na maovu ya watu. Katika hadithi inabainishwa kuwa umasikini na njaa ni miongoni mwa dalili za kipindi cha kwanza cha zama za mwisho. Nasio kwamba tunaamini umasikini ni sehemu yetu laa! bali umasikini kukithiri duniani ni dalili za kiama, kama vile kukithiri kwa mauaji na uzinifu nazo ni dalili za kiama.
binafsi nina uheshim sana sana uislam na tena watu waislam wengi wao ni watu wema na wnye upendo sana !
 
Mkuu nimekuelewa sana ulichowasilisha ingawa watu wanalichukulia kimzaha kwa jinsi walivyotoa comments zao, absolute poverty limekuwa tatizo sugu zaidi hasa kwa nchi maskini hususan Asia na Africa miongo ya hivi karibuni na hii hali haionekani kuboreka, hasa ikichagizwa zaidi na janga la korona, mabadiliko ya tabia nchi nk. Chukulia mfano hapa Tanzania maskini wanazidi kuongezeka na hali ya vipato vya watu inazidi kuwa mbaya. Ninakubaliana pia kwamba kuna spiritual element kwenye hili tatizo kama ulivyolihusisha na unabii wa kiama wa Prophet Muhamad na maandiko hayo hayo ya kinabii pia yamo katika biblia kwa sisi wakristo ambayo yanaashiria hali ya dhiki kuu kuelekea mwisho wa dunia.​
Nashukuru sana ndugu, Afadhali umeelewa makusudio ya maandiko haya. Ubarikiwe sana kiongozi
 
Usilete siasa katika dini yote uliyoeleza hayana ushahidi wa aya wala hadithi.
Dini ya kiislamu imejengwa katika misingi ya kufuata Qu'ran na hadithi za mtume.

Lakini hii thread yako haina ushahidi wowote kutoka katika dini.
Inafahamika kuwa umasikini ni ukosefu wa chakula, makazi, mavazi, huduma za afya na mahitaji mengine ya msingi kwa sababu ya kipato duni. Licha ya fursa zinazopatikana kutokana na maendeleo ya teknolojia, umasikini hivi leo ni moja kati ya matatizo makubwa kabisa yanayoukabili ulimwengu. Katika mabara ya Afrika, Asia, Amerika Kusini na Ulaya Mashariki watu wengi wanahangaika na njaa kila siku.

Kwa sababu ya mgao mbaya wa rasilimali za ulimwengu umasikini umesababisha uwepo mgawanyiko kati ya nchi za kaskazini ya jangwa la sahara ambazo ni za ulimwengu wa kwanza na nchi za kusini maskini ambazo ni za ulimwengu wa tatu.

Ubeberu na Ubepari usio na mipaka unazuia mgawanyo wa kipato ulimwenguni kote na unakwaza maendeleo ya nchi changa na nchi zinazoendelea. Wakati ambapo kuna watu wachache wanaofurahia kipato kinachozidi mahitaji yao, kuna idadi kubwa ya watu wanaohangaika na matatizo ya umasikini na ufukara. Katika Ulimwengu wa leo umasikini umefikia hatua mbaya au kiwango kibaya sana.

Haya yote, Mtume (s.a.w.w) aliyasema juu ya kuongezeka kwa umasikini. ''Umasikini na njaa ni miongoni mwa dalili za kipindi cha kwanza cha zama za mwisho:'' ''Masikini wataongezeka.'' ''Kipato kitagawanywa kwa matajiri tu, hakuna mafao kwa masikini.''

Ni dhahiri kuwa kipindi hicho kilichobashiriwa na Mtume (s.a.w.w) kinawiana na hali ya wakati wetu wa leo. Tukiangalia karne zilizopita tunaona kuwa shida na tabu zilizoletwa na ukame, vita na majanga mengine zilikuwa za muda mfupi na ziliishia katika eneo moja moja. Lakini umasikini na shida za leo ni za kudumu na sugu. Kwa hakika Mola wetu ni Mwingi wa Rehma, yeye hadhulumu watu lakini kwa sababu ya ukosefu wa shukurani wa wanadamu na maovu wanayoyafanya, umasikini na tabu vimeongezeka. Kwa hakika hali ya mambo ya kusikitisha inaonesha wazi kuwa dunia imetanzwa na uchoyo na ubinafsi.


View attachment 2097862
 
oohoo wanaume waislam tutakapo fika pepon tutapewa wanawake mabikraxxx, ohoo peponi kuna mito ya pombe tamu na tuta kunywa na kusaza, oohoooo ………………!
Hayo yanaweza yakawa makusudi ili kuwalingania watu kutekeleza maagizo ya MUNGU, kwa kuwa mwanaadamu kitu chake chenye thamani duniani ni mapenzi na starehe, basi nadharia hizo zinatia msukumo kwa mwanaadamu kumuendea Mwenyezi MUNGU kwa yale aliyo yaamrisha na kuacha aliyo yakataza. Ni kama vile mtoto mdogo kwakuwa anapenda kuangalia tamthilia unaweza kumwambia jitahidi usome ukifaulu vizuri nitakununulia TV yako na kukuwekea chumbani kwako. Japokuwa hii sio mada ningeomba tuachie hapo.
 
Hapana hii si kweli sayansi inathibitisha yale ambayo yalielezwa na dini.
Kwa mfano katika dini ya kiislam inaelezwa kuwa uumbwaji wa mtoto huanza pande la damu kisha pande la nyama na kuvishwa mifupata na kupuliziwa roho.
Haya yote yameelezwa katika Qu'ran na Mtume Muhammad miaka 1444 iliyopita.
Science imetoa majibu mengi sana ya maswali katika dunia ya leo kuliko dini...kimsingi dini ni ulevi kama ilivyo ulevi wa bangi na madawa mengine.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom