The Father of All
JF-Expert Member
- Feb 26, 2012
- 10,959
- 13,424
Ukiwasikiliza wagombea wetu hasa wa urais ambao ni wa chama kimoja japo wanajionyesha kama wanapingana wakati lao moja, huoni sera zaidi ya sura. Wakiahidi, unashindwa kuelewa kama ni nani kati ya mataahira kati yao na wapiga kura.
Mgombea wa urais anakwambia nitafanya hili au lile bila kuonyesha atalifanyaje. Yupo aliyeahidi kufuga mamba eti kuwala mafisadi wakati mwenye ukimuona ni mtoto wa fisadi wa zamani na unashangaa kama zimo au hamnazo. Kwa habari zaidi, BONYEZA HAPA.
Nafikiri na kuwaza kimya kimya baba yenu.