Elections 2010 Kwenye hili, Pinda ameniacha kwenye mataa.............

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,422
911,172
Jana kwenye hotuba yake ya kulishukuru Bunge, Mheshimiwa Mizengo Kayanza Pinda alitoa changa moto ambayo alidai ndiyo yenye uwezekano mkubwa wa kumkomboa mkulima, mfugaji na mvuvi mdogo mdogo hapa nchini chini ya sera ya "Kilimo kwanza"...............

Alidai Bunge libuni mikakati ambayo itafanikisha azma hiyo ya kumletea mnyonge wa Tanzania maendeleo ya haraka haraka...........................

Hapo Mheshimiwa Pinda ndipo aliponiacha kwenye mataa.........maendeleo ya Mtanzania huyo ambaye anamwita ni mnyonge yataanza pale ambapo amewezeshwa kujichagulia viongozi wake mwenyewe bila ya kuingiliwa na dola...........................

Kwa hiyo kama Mheshimiwa Pinda ni mkweli ataanza kwa kufanyia kazi malalamiko ya Chadema ya kutaka uchaguzi wa Uraisi uchunguzwe na Tume huru ambayo itateuliwa na Bunge letu ili kujua kama kweli kulikuwa na tofauti kati ya kura za Uraisi zilizohesabiwa vituoni na zile ambazo NEC ilizitangaza.....................

Bila ya kufanya hivyo sera ya CCM ya kilimo kwanza itakuwa ni sera ya wakubwa tu kama tulivyoona kwenye matrekta ambapo tumejionea wanajeshi wa ngazi za juu ndiyo wamekumbatia tenda za kuuza matrekta bomu kwa wakulima...............

Matrekta hayo sasa hivi hayana wakuyatumia kwa sababu ni madogo na yameshindwa kuhimili vishindo vya kulima........Hivi sasa waliyoyanunua hawawezi kurudisha mapesa waliyokopa kutokana na mitaji hiyo kushindwa kulima na kuleta uzalishaji................................

Na ugumu hapo unakuwa ni vipi wananchi hao hao wataweza kuiondoa madarakani serikali hii ambayo yaelekea ipo mstari wa mbele kuwafurahisha wakubwa serikalini kulikoni mkulima, mfugaji au mvuvi huyu wamwitaye ni mdogo mdogo?

Kwenye uvuvi badala ya kumkamata mtengeneza na muuza nyavu ni mvuvi mdogo mdogo ndiye ananyang'anywa hata kila kidogo alichonacho.................Kweli kwa utani utani huu mnyonge wa nchi hii analo bao hapo?

Mheshimiwa Pinda acha unafiki na uwe mkweli....................
 
kaka pinda ndo mtendaji mkuu wa serikali sasa ngoja tuone ata fanya nini katika bunge hili lililojaa vijana kama akina tundu lisu wenye hoja makini na yakinifu
 
kaka pinda ndo mtendaji mkuu wa serikali sasa ngoja tuone ata fanya nini katika bunge hili lililojaa vijana kama akina tundu lisu wenye hoja makini na yakinifu

Nimjuavyo Pinda atapwaya sana..................................
 
Kali ni unapotaka kukamua juice ya machungwa kutoka kwenye limao. HAPO KAZI IPO, Mtoto wa mkulima ana nia ila njia ya kupitishia nia zake na kutekeleza imesonga mbaya. Hakuna kitu tutakachoshuhudia
 
Hata kama Pinda anataka kufanya vitu vuikunbwa kwa serikali hii atachemsha, kwa sababau hajaandaliwa kuwa raisi
 
Jamani naomba tuwe na fikra chanya, Pinda ametoa changamoto na ni wajibu wa wabunge na watendaji wengine wa kisiasa kuhakikisha mwananchi wa kawaida anakombolewa, tukimuachia Pinda peke yake hakika hakuna litakalotokea, tena alitaka bunge liwe kali, kama tumemuelewa wote maana yake wamsaidie kuiwajibisha serekali katika utendaji wako; hofu ni kwamba bunge lina wazee na wana ccm zaidi ya 240, je watashirikiana na wenzao wa chadema kumkomboa mwananchi!? Binafsi sina mashaka na Pinda ila kile kikundi kilicho nyuma ya pazia(mafisadi) ndio kinatibua, bunge likiwa kali mwananchi atakombolewa tu!:yield:
 
  • Jamani naomba tuwe na fikra chanya, Pinda ametoa changamoto na ni wajibu wa wabunge na watendaji wengine wa kisiasa kuhakikisha mwananchi wa kawaida anakombolewa, tukimuachia Pinda peke yake hakika hakuna litakalotokea, tena alitaka bunge liwe kali, kama tumemuelewa wote maana yake wamsaidie kuiwajibisha serekali katika utendaji wako; hofu ni kwamba bunge lina wazee na wana ccm zaidi ya 240, je watashirikiana na wenzao wa chadema kumkomboa mwananchi!? Binafsi sina mashaka na Pinda ila kile kikundi kilicho nyuma ya pazia(mafisadi) ndio kinatibua, bunge likiwa kali mwananchi atakombolewa tu!:yield:​




    progress.gif



Haya hayawezekani kwa sababu serikali iliyoingia madarakani siyo chaguo letu........sasa inamwongoza nani?
 
hivi kama asinge chaguliwa tanzania ingemkumbuka kwa lipi? i mean jambo ambalo seriously alilisimamia na kuwa na positive impact
 
Kwanza hata yeye anajua kabisa JK hakumtaka ndo maana akashindwa kupeleka jina asubuhi. Hii imelazimishwa ili kuua soo ya 6 maana bado donda lilikuwa halijapona. Kumweka waziri mkuu mwingine ni sawa na kuchoma kisu kwenye donda ambalo bichi. Yeye ajipange kivyake maana hata akimaliza miaka 5 Mungu atakuwa anampenda sana.
 
ACHA WAJIKOSHE, ILA WAFAHAMU watanzania wamekua na uelewa mkubwa, hivyo huwezi kuwadanganya kwa pipi kama watoto
 
Watanzania wachache wanaompigia debe Pinda nawaona ni watu wa ajabu. Kama umepewa Uwaziri mkuu na kutokana na uwezo ulionao kwa nini bado unalilia nyau kila siku? Hawanisikilizi nia yangu ni nzuri etc. Huu ni ujinga kama sera zake hawazitaki kwa nini anang'ang'ania kuendelea kwenye hicho cheo? Simba mwenda pole iko ngonjwa. Pinda ni mwizi kama rais wake wote wanatetea ufisadi uliowaweka pale kutafuna pesa ya walipa kodi ...... ..... kama yeye sio mwizi awashughulikie mafisadi na genge lao la wahuni EL, Chenge, RA, Manji, Dau etc. kwenye matendo yake.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom