Kwenye Haki za Wanyonge, Magufuli ni Kama Khalifa Mkuu Harun El Rashid wa Alfu Lela Ulela!.

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,507
113,628
Wanabodi,

Hili ni bandiko la simulizi ya Kayafa Mkuu wa Bhaghdad enzi za simulizi za Alfu Lela Ulela, Khalifa Harun El Rashid, lengo likiwa ni kuwahamasisha wana jukwaa kuwa kwenye mazuri tupongeze, kwenye mabaya tukosoe na kwenye maovu tulaani, hivyo linapokuja suala la haki bin haki zikiwemo haki za wanyonge, naombeni muungane nami kumpongeza kwa dhati, rais wetu Dr.John Pombe Joseph Magufuli kwa kuwa ni mtetezi wa kweli wa haki za wanyonge.
Naomba kabla sijakisema nilichokusudia, kwanza soma hii simulizi hapa chini
Baada ya simulizi hiyo, sasa shuhudia kitu kilichofanyika jana kwa huyu mwanamke mjane, halafu angalia rais Magufuli alifanya nini.
Kitendo alichokifanya jana rais Magufuli cha kumsikiliza yule mwanamke ndicho alichokifanya Kayafa Mkuu Khalifa Harun el Rashid kwa yule mwanamke mjane masikini, na kiukweli kitendo kile kimenigusa sana, angekuwa mwingine, angeachia yule mwanamke mjane ashughulikiwe kikamilifu na vyombo vya dola na isingekuwa rais kumkomboa, hapo ambapo angelalia usiku wa jana, ni Mungu tuu pekee ndiye angejua kilichomkuta!, sijui hata kama angefika asubuhi salama, maana hawa polisi wetu sometimes, ni machoni tuu ndio kama watu, lakini mioyoni mwao ni wanyama kabisa!, ma beast ya ajabu!.

Kilichofanyika jana kinatoa somo kubwa sana kwa wanawake wengine na wanyonge wanaoteswa kwa kukosa haki, jinsi yule mama alivyoonyesha ujasiri na ushujaa kudai haki mbele ya rais ni uthibitisho kuwa haki hailetwi kwenye kisahani cha chai, haki inadaiwa kwa nguvu zote, na ikibidi inapiganiwa, hata kuweza kukifikia mahali, unaweza kujikuta uko tayari kufa kwa kuutoa uhai wako kupigania haki, watakaofaidika ni watoto wako na watoto wa watoto wako!. Hivyo linapokuja suala la kupigania haki, kutetea haki, hata sisi jf, tusiwe na mswalie Mtume na mtu yoyote mminyaji haki, tupiganie haki zetu kwa nguvu zote!.

Mnaweza kujiuliza hivi kweli ni Magufuli huyu huyu dikiteta, sasa ndiye mlinzi wa haki za wanyonge?!, sasa inawezekanaje mtu huyo huyo ni mtetezi wa haki za wanyonge kwa upande mmoja, lakini hapo hapo akawa ni ndiye mminyaji mkubwa wa haki za kisiasa?!.

Usikute inawezekana, ameamua kuminya demokrasia na haki za kisiasa, kwa sababu, hao political players, mnaowadhania ni wanasiasa wa kweli, kumbe Magufuli amewashitukia kuwa sio wanasiasa chochote, wala lolote bali ni wapiga dili tuu za kisiasa, kwa mgongo wa siasa, if that is the case, then, kwa vile Magufuli ameamua kuwashughulikia wapiga dili wote, then, ni wapiga dili wote wanashughulikiwa, hadi wapiga dili za kisiasa!, hivyo kuhalalisha kuminywa kwa demokrasia, kuvunja katiba kwa kupiga marufuku mikutano ya kisiasa kwa sababu hao wanasiasa wote wa vyama vingine, kwake ni wapiga dili tuu, wanasiasa wa ukweli ni CCM tuu pekee!. Tumshukuru pia kwa hatua hii ya kuwashtukia wanasiasa wapiga dili za kisiasa waliokuwa wanawapamatumaini Watanzania kuwa kuna siku moja CCM itaondolewa madarakani, kumbe walikuwa wanatuingiza chaka!. Ukweli ni kuwa CCM, itatawala milele!. Ndicho chama pekee chenye hati miliki ya kutawala Tanzania, hivyo Magufuli analisimamia hili kuhakikisha CCM haisumbuliwi na haibughudhiwi!.

Kwa upande wa rais Magufuli ameendelea kuthibitisha kuwa, when it comes kwenye manyanyaso ya wanyonge, yeye ni mtu wa watu, he is simply, a man of the people. Kama akiendelea hivi na kisha Roho wa Mungu wa kweli, akamuingia na kuachana na udikiteta wake wa asili, ambao ni kama ushetani fulani, na akazirudisha haki zote za msingi zilizoainishwa kwenye katiba yetu, mnaweza kushangaa by 2025 akawa kama ndiye Mfalme Suleman wa Tanzania!, hivyo Watanzania tukapiga kelele za kubadili katiba Magufuli aendelee milele na milele mpaka pale Mungu atakapoona inatosha na kumuita kwake!.

NB. Kwa pongezi hizi simaanishi kuwa sasa rais Magufuli ndio ghafla kageuka kuwa malaika!. No, kama rais Magufuli ni dikiteta, pamoja na wema wake huu, bado ni dikiteta vile vile, ila ni dikiteta mzalendo mwenye huruma fulani kwa watu fulani, lakini ni katili kwa wengine wakiwemo wapiga dili!.

Hongera sana kwa Rais wetu mpendwa, Dr. John Pombe Joseph Magufuli, jana umeonyesha utu wa hali ya juu sana kumsikiliza yule mama mjane, na unastahili pongezi za dhati kutoka kwa wapenda haki wote, tunakuomba ujue tuu kuna makumi kwa mamia na maelfu ya Watanzania masikini wa kutupwa ambao wamedhulumiwa haki zao, na hawana courage kama ya huyo mama kukufikia, wengine hawa hata access ya kusikilizwa na wasaidizi wako, kuna mamia wanaozea magerezani kwa kesi za kubambikiwa, kuna mamia ni mahabusu wakuozea magerezani kwa kisingizio upelelezi haujakamilika mfano mzuri ni ni yule wakili wa Arusha Medium Mwale, huu ni mwaka wa 7 yuko mahabusu kwa kosa ambalo adhabu yake ni faini na kufungo cha mwaka mmoja!.

Tunakuomba huruma yako kwa wanyonge wanaonyimwa haki zao, ielekeze kwa wasaidizi wako ili Watanzania wote watendewe haki na sio kusubiri hadi kilio kikufikie wewe. Angazia watuhumiwa wa kesi za uhujumu, fuatilia uone ni wangapi wanaozea mahabusu kwa miaka na miaka bila hata kesi kuanza kusikilizwa. Justice delayed ni justice denied.

Mungu ibariki Magufuli aendelee kuhakikisha hata masikini na wanyonge, wanatendewa haki.
Mungu Ibariki Tanzania.

Paskali
Rejea

Rais Magufuli ni Simple, Genuine & Down To Earth-He is Simply A Man of The People!

Magufuli Kama Nyerere: Ni Mtu wa Watu, Hapapasi, Hamung'unyi, Ni Kazi Tuu, Ila Pia sio Kama Nyerere!

Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata!. Atakayeleta Fyoko, Ataisoma Namba!.

Kwa Kasi hii ya Magufuli, kuna haja Kufanya Uchaguzi wa Rais 2020?
 
Paskali ww ni msomi.Mm nahisi kwa tukio la huyu mama tusiwe wepesi wa kutoa suluhu kwamba kuna haki ananyimwa.Kote alikoanzia hawawezi kuwa na roho ngumu ya kupoteza haki.Vumilia tupate ukweli na nadhani ww mwenyewe unaweza rudi hapa na kututahadharisha kwamba si wote watoao machozi huwa ndo wafiwa.Tuachie mahakama zetu zifanye kazi.
 
Pascal Shemeji yangu ambaye eti nasikia jina lako ni NJAA wakati wapwa zangu na mdogo wangu wala mpaka wasaza huko kwa makao yako!Leo nitatofautiana na wewe,nimekaa nikajiuliza maswali mengi na kukosa majibu:
1.Kama huyu Mama alikuwa na miradhi iliyoandikwa na Mumewe nani alibadili miradhi hii??
2.Kwa sheria za Kiislamu zinasemaje??Je,kesi yake iliamriwa kwa sheria zipi??Je Kulingana na matakwa ya sheria za kiislamu yametimilika yote??
3.Miaka 10 alikuwa anahangaika kupata haki yake kwanini hakufanya alichofanya jana??
4.Je ni kweli Hukumu ziko mbili??
5.Hii ya madawa ya kulevya imeingiaje pale ilhali anadai Mirathi na si issue ya Madawa ya kulevya??.
6.Kama IGP,AG,RPC,Judge Mkuu,DPP na Waziri wa Sheria wote wanajua kesi hii ilikuwaje watu wote hawa wakashirikiana kutompa huyu Mama haki yake??Jamani kwa jinsi ninavyoujua utendaji kazi wa kupenda SIFA hili ilikuwaje lisishughulikiwe hata na Mkuu wa Wilaya au Mkuu wa Mkoa kabla halijafika jana uwanjani??

Shemeji yangu nimeona kama picha fulani hivi isiyo na sterling,maswali ni mengi kuliko majibu.Ngoja tuusubiri ukweli isisje ikawa tunapotezea ili Kaka yako aonekane ni yule Hakimu muovu aliyempa haki yake Mjane aliyemlilia kwa siku nenda rudi.

Shemeji in short na nusa harufu ya moshi wa BANGI.
 
Aliona rais ndo angemsikiliza, maana yake ni kwamba wateule wa rais na mahakama hazitoi haki kwa sababu ya kuangaliana usoni. Wapo wengi wenye malalamiko kama hayo na hawawezi kumuona rais au wanaona aibu kujitokeza mbele ya Camera za wanahabari lakini hiyo haiondoi kiu ya haki zao. Mifumo ya utoaji haki nchini ni mibovu, na rais alitakiwa amhoji yule mwanamke aseme matatizo aliyoyapata kufuatilia haki yake.
 
Mkuu huyo ndiye JPM masifa

1. Kama anajua mapungufu ya mahakama na jeshi la polisi mbona hatua muafaka hajazichukua ?

2. inakuwaje anazlitumia mahakama na jeshi la polisi hizo hizo kukandamiza haki?

3. Wakristo wana hadithi hiyo hiyo ni moja ya hekima za Mfalme Suleiman. Kwa tafakuri yangu yule mama masikini ndiye jasiri ana hekima busara kiasi cha kumshawishi Khalifa.

4. Mfumo uliozaa maovu hauna namna ya kujisafisha. Magu anafaidika na mfumo wakiovu; watawaliwa wote hatuwezi fika mbele yake kwa matatizo ya kimahakama na uonevu wa jeshi la polisi.

MAGU HASTAHILI CHEMBE YA KUSIFIWA.
 
paskali post zako kuanzia 2015 way back zilikua za ukweli sana lakini za kipindi hiki zimejaa unafiki na kujipendekeza badilika brother achana na huo upuuzi protect your integrity cause huyo unaejipendekeza kwake doesn't give a https://jamii.app/JFUserGuide about you kujipendekeza na unafiki sio tabia za kiume #no offense#don't get it twisted
 
Mkuu Mkulungu Mkuyengo, mimi ni binadamu, na huma beings wote, are not static, they are dynamic, and hence they change with time, for the better or for the worse na mimi vivyo hivyo ninakwenda nikibadilika, au for the better, or for the worse!.

Kwa wanye uwezo wa kunisoma kijuu juu kama wewe, utaniona nimebadilika, hivyo you are very right kusema I have changed for the worse!. Lakini kwa wenye uwezo wa kusoma na kuzama deep in between the lines, na kubaini the motive behind, wanajua Paskali ni yule yule juzi, jana na leo, and has changed for the better!.

Tofauti yangu kubwa na members wengi humu jf, wengi wetu wamechagua upande, wakiamua kuponda wao ni kuponda tuu mwanzo mwisho, hata mtu afanye mazuri vipi wao wataponda tuu!. Mimi sina upande, nasimama kwenye kwenye ukweli na haki bin haki, kwenye mazuri napongeza, kwenye mabaya nakosoa, na kwenye maovu, nalaani!.

Paskali
 
Ng'wana wane Mayalla usibetweke na sarakasi za msukuma mwenzio, huyu jamaa hana la maana katika hili zaidi ya kutaka kujiongezea ratings. wewe ni broadcaster unajua nini umuhimu wa ratings katika television. Huyu ni mtu aliyewaambia wahaya kule Bukoba watafute njia kujijengea nyumba zao wakati ambao walitaka msaada kutoka serikalini (usisahau walichangiwa na ndugu zao watanzania na pesa yao ikapigwa na serikali inayozuia ma deal) . Huyu ni mtu aliyemwambia Mbunge na muwakilishi wa wana Bukoba mjini aliyemuomba rais awasaidie wahanga wa tetemeko kwa kuwapunguzia gharama za vifaa vya ujenzi (hapa Lwakatare alichokiomba ni serikali ku subsidise gharama za vifaa vya ujenzi) matokeo yake alikejeliwa. Halafu unaniaminisha kuwa huyu ni mtetea wanyonge labda wanyonge wa Chato. Mayalla ujue huyu jamaa amejaa misifa tu ni Mbowe peke yake anayemuweza huyu jamaa. Mbowe anamvika kilemba cha ukoka na kwa kutojielewa Magufuli anaingia king, ndiyo uzuri wa kuingia mjini mapema unavyomsaidia Mbowe. Magufuli ni chunusi mkubwa kwa hii nchi hana hata maana kabisa na wala hana hata mapenzi wa hili Taifa na watu wake.

Japo Bush alikuwa hamnazo lakini alijitahidi kuwasaidia wahanga wa Mississippi lakini huyu jamaa kwanza hakufika katika maeneo ya maafa na hatujui nini kilimzuia kufika hapo. Mafuriko ya marekani Obama aliacha kampeni na alienda kuungana na wahanga, Mafuriko ya England David Cameron na Prince Charles walienda kuungana na wahanga na kuwafariji walijeruhiwa. Tetemeko la Italy waziri mkuu wa Italy alifika sehemu ya tukio na hao wote waliwahakikishia waathirika kuwa serikali itawasaidia kujenga miundo mbinu na majengo yaliyoathirika na maafa. Hapa kwetu Rais kaenda baada ya hata watu waliokufa walianza kuoza na ujumbe aliokwenda nao ni acheni wafu wajizike wenyewe halafu leo unataka tumpongeze kwa huyu mama na nina imani kubwa aliwekwa pale kama sarakasi ama maigizo.

Pascal nilidhani wewe ni mtu ilye elimika ungeweza kutambua ukweli na utapeli wa huyu msukuma mwenzio. kama ninyi waandishi na ma Broadcaster mnahadaiwa kirahisi je sisi wengine ambao hatuna hizo fani itakuwaje????????

Mungu Ibariki Tanzania
 
Ng'wana wane Mayalla usibetweke na sarakasi za msukuma mwenzio, huyu jamaa hana la maana katika hili zaidi ya kutaka kujiongezea ratings. wewe ni broadcaster unajua nini umuhimu wa ratings katika television. Huyu ni mtu aliyewaambia wahaya kule Bukoba watafute njia kujijengea nyumba zao wakati ambao walitaka msaada kutoka serikalini (usisahau walichangiwa na ndugu zao watanzania na pesa yao ikapigwa na serikali inayozuia ma deal) . Huyu ni mtu aliyemwambia Mbunge na muwakilishi wa wana Bukoba mjini aliyemuomba rais awasaidie wahanga wa tetemeko kwa kuwapunguzia gharama za vifaa vya ujenzi (hapa Lwakatare alichokiomba ni serikali ku subsidise gharama za vifaa vya ujenzi) matokeo yake alikejeliwa. Halafu unaniaminisha kuwa huyu ni mtetea wanyonge labda wanyonge wa Chato. Mayalla ujue huyu jamaa amejaa misifa tu ni Mbowe peke yake anayemuweza huyu jamaa. Mbowe anamvika kilemba cha ukoka na kwa kutojielewa Magufuli anaingia king, ndiyo uzuri wa kuingia mjini mapema unavyomsaidia Mbowe. Magufuli ni chunusi mkubwa kwa hii nchi hana hata maana kabisa na wala hana hata mapenzi wa hili Taifa na watu wake.
Japo Bush alikuwa hamnazo lakini alijitahidi kuwasaidia wahanga wa Mississippi lakini huyu jamaa kwanza hakufika katika maeneo ya maafa na hatujui nini kilimzuia kufika hapo. Mafuriko ya marekani Obama aliacha kampeni na alienda kuungana na wahanga, Mafuriko ya England David Cameron na Prince Charles walienda kuungana na wahanga na kuwafariji walijeruhiwa. Tetemeko la Italy waziri mkuu wa Italy alifika sehemu ya tukio na hao wote waliwahakikishia waathirika kuwa serikali itawasaidia kujenga miundo mbinu na majengo yaliyoathirika na maafa. Hapa kwetu Rais kaenda baada ya hata watu waliokufa walianza kuoza na ujumbe aliokwenda nao ni acheni wafu wajizike wenyewe halafu leo unataka tumpongeze kwa huyu mama na nina imani kubwa aliwekwa pale kama sarakasi ama maigizo.
Pascal nilidhani wewe ni mtu ilye elimika ungeweza kutambua ukweli na utapeli wa huyu msukuma mwenzio. kama ninyi waandishi na ma Broadcaster mnahadaiwa kirahisi je sisi wengine ambao hatuna hizo fani itakuwaje????????
Mungu Ibariki Tanzania
 

Binafsi siamini katika kutafuta suluhu ya matatizo kama hayo kwenye mikutano ya hadhara. Hii naifananisha ni ile mikutano ya Mh. Makonda akiwa ziarani DSM. Kwa maoni yangu kuomba majibu hadharani kama ilivyofanyika haiwezi kuleta suluhu ya mara moja na IGP alijitahidi sana kuchagua cha kusema na cha kuacha na maneno ya kutumia. Suala kama la yuele mama ni mtambuka. Linagusa maeneo maengi sana. Kuna cha kujifunza kutokea kwenye mifano kama ya handling ya issue ya Faru John. Haikuwa na haraka kuitisha press conference kuweka tuhuma wazi kabla ya uchunguzi wa umakini ziadi kabla ya viongozi kutoa matamko.
 
Pascal nakuomba jaribu kusoma mchango wa mawazo aliyoutoa Tetty.Tetty kaeleza vizuri sana na kaangalia mbali sana.Kwani watu wote hao Tetty aliyowataja kwa nyazifa zao lazima ujue kuna shida mahali.Usikute huyo mama ndiye anayetaka kudhulumu haki wenzake.Kwanza jiulize alipataje namba ya Mh Raisi na kumtumia Msg.Ameweza kuonana na AG na Waziri wa katiba na Sheria na kudai wameshindwa kumsaidia.Pascal naomba kabla hujafanya uchunguzi wa kina kuhusu jambo hili hukupaswa kuandika uliyoandika.Sikuzote nimekuwa naunga mkono habari unazoleta lakini kwaleo naomba nitofautiane nawe.
 
Kwa mtu aliyemsikiliza IGP kwenye hii issue alipata mashaka sana kuhusu huyu mama. Hii issue ilikuwa kwenye finder tips za Mangu maana yake aliifanyia kazi na ilifuatiliwa sana. Kwa hali ya kawaida ni ngumu sana watu wote waliotajwa ku -conspire against huyu mama tena kwa issue iliyotoka kwa mtu wa caliber na tabia za Mh. Rais. Mimi naamini IGP alitumia busara kuliongelea hilo katika mazingira hayo aliyolazimika kuliongelea tena bila kutarajia. Tusubiri maana yameshaanza kujitokeza mane maneno yanayoleta mashaka lakini tusubiri taarifa rasmi. Na nyie wenye hivi vi house vidogo vidogo muwe mnaacha will.
 

Msiwe na akili nzito. Magufuli kampatia mama nafasi ya kujieleza. Magufuli hakutosa maamuzi bali maelekezo kwa vyombo na ngazi husika kufuatilia suala hilo. Asingemsikiliza mmngemnanga wiki nzima humu.Kamsikiliza bado mnakosoa. Watu gani nyie?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…