Kwenye awamu ya 5 viongozi wote Wastaafu na waliokuwa madarakani mawasiliano yao yalidukuliwa na kuanikwa hadharani. Faragha zao zilipuuzwa

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,730
218,304
Tunaendelea na mada zetu za mwezi huu ambao ni mwezi wa Mungu .

Kwenye uongozi wa awamu ya 5, haki za kikatiba, ikiwemo haki ya faragha ilipuuzwa , viongozi wote wa sasa na wastaafu , wakiwemo hata raia wa kawaida waliotiliwa shaka, hasa wale wanaotumia mawasiliano ya Kitanzania walidukuliwa, Taarifa zinaeleza kwamba hawa akina Nape, Membe, Kinana na Makamba ni wachache katika wengi waliodukuliwa, faragha za watu zilianikwa na wadukuaji waliotumwa, simu zote za familia za viongozi na wajukuu zao zilidukuliwa, unaambiwa ilikuwa aibu, maana udukuzi huo ulikuwa wa kishamba sana, kiasi cha kudukua hata waliokuwa wanaongea mambo yao na mahawara zao au michepuko yao, hivi unamdukua mtu anayeongea na hawaraake ili upate nini?

JamiiForums-787880945.jpeg

Ukitaka kuthibitisha hilo fuatilia nyuzi za Cheusi Mangala, ambayo tunadhani ilikuwa ID ya wadukuzi wenyewe au mtu wa karibu na wadukuzi ama labda msamaria mwema, huyu ndiye aliyeanika udukuzi wote hapa JF

Udukuzi ule zaidi ya kudhalilisha viongozi waliotajwa haukuwa na tija yoyote kwenye Taifa , hakuna hata mmoja kati ya waliodukuliwa aliyeonyesha uhaini wowote. Hoja zao nyingi walizodukuliwa nazo zilikuwa ni za mshangao tu wa namna nchi inavyoendeshwa kishamba, badala ya kuwadhalilisha wadukuliwa, hoja zao zilipaswa kutumia kujisahihisha.

NITASEMA KWELI DAIMA FITINA KWANGU MWIKO
 
uongo na upotoshaji una haribu hadhi na kushusha heshima na utu wako 🐒

zaidi sana unaharibu image na status ya taasisi yako mbele za jamii, unaikosesha kuaminika 🐒

hata hivyo ni hii dalili bayana iliyokomaa tena iliyokomaa kabisaa, ya kukosa hoja, kukosa sera, Lakini na kupoteza uelekeo na dira kung'ag'ana na masuala ambayo hayana umuhimu wowote wala hayasaidi kukuongezea chochote 🐒

umaskini wa hoja, fikra na sera ni uraibu unaotia huruma sana mbele ya jamii 🐒
 
uongo na upotoshaji una haribu hadhi na kushusha heshima na utu wako 🐒

zaidi sana unaharibu image na status ya taasisi yako mbele za jamii, unaikosesha kuaminika...
Je, kuna uongo wowote kwenye andiko hili?
 
Ninakuonya! Ulikotoka ni mbali sana, umekuwa mtu mhimu sana hapa kwa nyakati tofautofauti, kwa sasa hadhi yako inashuka sana

Umekuwa na nyuzi za kijinga mno, sielewi iwapo na wewe ulipigwa zile chanjo za Korona, walio wengi wameendelea kuchizika
Nitasema kweli daima fitina kwangu mwiko .

Ambacho umesahau ni hiki , sijawahi kuogopa vitisho .
 
Ninakuonya! Ulikotoka ni mbali sana, umekuwa mtu mhimu sana hapa kwa nyakati tofautofauti, kwa sasa hadhi yako inashuka sana

Umekuwa na nyuzi za kijinga mno, sielewi iwapo na wewe ulipigwa zile chanjo za Korona, walio wengi wameendelea kuchizika
umaskini wa fikra mpya ni kitu mbaya sana 🐒
 
Back
Top Bottom