Wamama wengi wapo hivyo(unless wawe wameshamkubali au wameshamtambua na kumuamini mwanamke kabla), mara nyingi husema subiri mtoto azaliwe tukamtazame kwanza.
Kuna mshkaji mmoja alimbishia mama yake, akakubali mimba,mtoto alivyozaliwa mama yake akaenda kumtazama mtoto akamwambia mshkaji mtoto yule sio wako, jamaa akawa mbishi. Siku moja jamaa kaenda kumchukua mtoto(baada ya mwaka mmoja) kaenda nae home kwao, mama yake akaanza kugomba, nimekwambia mtoto sio wako bado tu hunisikilizi. Mama akamchukua mshkaji na mtoto akawapeleka kucheki dna kama zina match. Baada ya siku chache majibu kuja yanaonyesha mshkaji uwezekano wa yeye kuwa biological father wa yule mtoto ni finyu mno, hivyo mtoto sio wake.
Mshkaji anampigia demu kumwambia matokeo ya dna test, demu anaanza kumgombeza mshkaji, si nilikukataza mambo ya dna kwa nini umeenda kucheki, ina maana huniamini, mwanaume gani hajiamini, inatakiwa ujiamini, kwanza mlete huyo mtoto na unieleze ni kwa nini umeenda kucheck dna.