Dkt. Gwajima D
Minister
- Nov 28, 2015
- 1,706
- 8,657
Salaam.
Natambua kabisa wapo Mama na Baba wa Kambo ambao, wana upendo na wamekuwa watu wema kwa watoto wanaowalea wakiwemo yatima. Hakika, wanastahili Pongezi.
Wapo sasa wale Baba na Mama wa Kambo ambao, daaaaah... wamekuwa mwiba kwa watoto wanao walea wakiwemo yatima.
Hapa nimepokea kisa kati ya visa vingi kutoka kijiji kimoja huko mkoani kuwa, mtoto yatima anayelelewa na mama wa kambo alichukua vitu kidogo tu kuchezea kama mtoto tu. Baada ya mama kurudi, mtoto alipigwa sana ikafikia hatua hadi akachomwa kwa moto katika maeneo mbalimbali mwili. Nimeelekeza wafuatiliwe watiwe nguvuni.
Haya, hebu Baba na Mama wa Kambo kokote mliko wale ambao, mnatesa na kunyanyasa watoto mlioaminiwa kuwalea, mtajisikiaje kushtakiwa?
Kwa kifupi, natoa wito kwa jamii eneo hili pia limulikwe vilivyo tafadhali. Mulikaaaaa fichua uovu aina zote.
Wizara ya Maendeleo na Ustawi wa Jamii sasa tunafikika hadi vijijini hata kwa wenye simu za kitochi nao wakiandika ujumbe tunapata mara moja na hatua tunachukua na mtoa taarifa analindwa.
Tuendelee kushirikiana, bado kidogo ukatili utakuwa kwa heri.
Tunasonga mbele na FAHAMU ELIMIKA CHUKUA HATUA [FAECH].
07 JULAI, 2025.
Natambua kabisa wapo Mama na Baba wa Kambo ambao, wana upendo na wamekuwa watu wema kwa watoto wanaowalea wakiwemo yatima. Hakika, wanastahili Pongezi.
Wapo sasa wale Baba na Mama wa Kambo ambao, daaaaah... wamekuwa mwiba kwa watoto wanao walea wakiwemo yatima.
Hapa nimepokea kisa kati ya visa vingi kutoka kijiji kimoja huko mkoani kuwa, mtoto yatima anayelelewa na mama wa kambo alichukua vitu kidogo tu kuchezea kama mtoto tu. Baada ya mama kurudi, mtoto alipigwa sana ikafikia hatua hadi akachomwa kwa moto katika maeneo mbalimbali mwili. Nimeelekeza wafuatiliwe watiwe nguvuni.
Haya, hebu Baba na Mama wa Kambo kokote mliko wale ambao, mnatesa na kunyanyasa watoto mlioaminiwa kuwalea, mtajisikiaje kushtakiwa?
Kwa kifupi, natoa wito kwa jamii eneo hili pia limulikwe vilivyo tafadhali. Mulikaaaaa fichua uovu aina zote.
Wizara ya Maendeleo na Ustawi wa Jamii sasa tunafikika hadi vijijini hata kwa wenye simu za kitochi nao wakiandika ujumbe tunapata mara moja na hatua tunachukua na mtoa taarifa analindwa.
Tuendelee kushirikiana, bado kidogo ukatili utakuwa kwa heri.
Tunasonga mbele na FAHAMU ELIMIKA CHUKUA HATUA [FAECH].
07 JULAI, 2025.