Kweli Watanzania wameichoka CCM

Kweli Watanzania wameichoka CCM

jebibay

JF-Expert Member
Joined
Nov 3, 2012
Posts
1,431
Reaction score
642
Jana ilitokea nikawa naangalia kipindi cha TV (TBC1), nadhani kinaitwa Tuambie or Niambie sikumbuki sawa sawa. Kipindi kilikuwa kinahusu sheria hii mpya ya uhalifu wa mitandaoni na studio kulikuwa na wageni watatu (Mwanasheria kutoka Wizara ya Mawasiliano, Mratibu wa mambo ya mtandao kutoka polisi na mgeni mwingine mmoja).

Akatokea mwananchi mmoja akapiga simu akauliza hatua ambazo anatakiwa kuzifuata ikiwa atapata ujumbe wa kuudhi au matusi kwenye simu yake. Akasema kwa mfano wakati wa campaign za uchaguzi wa mwaka huu ikitokea akapata ujumbe wa kuudhi kwamba "Chagua CCM" achukue hatua gani kushughulika na ujumbe huu wa maudhi kwake ?!

Yaani imefikia hata ujumbe wa campaign wa CCM wengine wanachukulia kwamba ni ujumbe wa kuudhi (kama matusi vile)!.

Kweli watu wana hasira na CCM !
 

Attachments

  • 1431691790768.jpg
    1431691790768.jpg
    8.4 KB · Views: 2,973
ah hahaha haaaa hahaaaa, ni kweli maana sheria haijatafsiri kitu kibaya ni kwa kiasi gani
hivyo yoyote anayeona hajafurahishwa nacho anaweza akashitaki
 
hahahaaaa...ila hii sheria sijaelewa kwa nini imekaa upande mmoja,yani hata mahakama iko upande wao..i wish ningejua ningeangalia hicho kipindi ili nione mtazamo wao walioitengeneza
 
Jana ilitokea nikawa naangalia kipindi cha TV (TBC1), nadhani kinaitwa Tuambie or Niambie sikumbuki sawa sawa. Kipindi kilikuwa kinahusu sheria hii mpya ya uhalifu wa mitandaoni na studio kulikuwa na wageni watatu (Mwanasheria kutoka Wizara ya Mawasiliano, Mratibu wa mambo ya mtandao kutoka polisi na mgeni mwingine mmoja).

Akatokea mwananchi mmoja akapiga simu akauliza hatua ambazo anatakiwa kuzifuata ikiwa atapata ujumbe wa kuudhi au matusi kwenye simu yake. Akasema kwa mfano wakati wa campaign za uchaguzi wa mwaka huu ikitokea akapata ujumbe wa kuudhi kwamba "Chagua CCM" achukue hatua gani kushughulika na ujumbe huu wa maudhi kwake ?!

Yaani imefikia hata ujumbe wa campaign wa CCM wengine wanachukulia kwamba ni ujumbe wa kuudhi (kama matusi vile)!.

Kweli watu wana hasira na CCM ![/QUO
Mdau umenichekesha sana, kiukweli wakati wa uchaguzi huwa kuna meseji za kukera sana nakumbuka 2010 zilikua zinaingia sana kwenye simu yangu. Pamoja na hayo hata haya makampuni yana sms za kukera pia.
 
Kuna vijana juzi walipeana adhabu kama mmoja atashindwa kutimiza majukumu waliyowekeana, moja ya adhabu yao ni kuvaa Tshirt na kofia ya CCM kwa siku nzima ama fine ya 100,000/-.

Cha ajabu vijana wengi walikubali kulipa hiyo fine.
 
Jana ilitokea nikawa naangalia kipindi cha TV (TBC1), nadhani kinaitwa Tuambie or Niambie sikumbuki sawa sawa. Kipindi kilikuwa kinahusu sheria hii mpya ya uhalifu wa mitandaoni na studio kulikuwa na wageni watatu (Mwanasheria kutoka Wizara ya Mawasiliano, Mratibu wa mambo ya mtandao kutoka polisi na mgeni mwingine mmoja).

Akatokea mwananchi mmoja akapiga simu akauliza hatua ambazo anatakiwa kuzifuata ikiwa atapata ujumbe wa kuudhi au matusi kwenye simu yake. Akasema kwa mfano wakati wa campaign za uchaguzi wa mwaka huu ikitokea akapata ujumbe wa kuudhi kwamba "Chagua CCM" achukue hatua gani kushughulika na ujumbe huu wa maudhi kwake ?!

Yaani imefikia hata ujumbe wa campaign wa CCM wengine wanachukulia kwamba ni ujumbe wa kuudhi (kama matusi vile)!.

Kweli watu wana hasira na CCM !

Ungetusaidia kama ungetuwekea jibu walilomptia huyo muuliza swali, ili tuweze kufahamu hatua za kuchukuwa pindu tutakapopata huo ujumbe wa kuudhi wa CHAGUA CCM.
 
Kusema kweli mtu akikuambia "Chagua ccm", atakuwa amekutukana tusi la kudhalilisha kuliko uzito wa matusi yote duniani ukiyajumulisha.

Huyo lazima ushughulike naye!.
 
Jana ilitokea nikawa naangalia kipindi cha TV (TBC1), nadhani kinaitwa Tuambie or Niambie sikumbuki sawa sawa. Kipindi kilikuwa kinahusu sheria hii mpya ya uhalifu wa mitandaoni na studio kulikuwa na wageni watatu (Mwanasheria kutoka Wizara ya Mawasiliano, Mratibu wa mambo ya mtandao kutoka polisi na mgeni mwingine mmoja).

Akatokea mwananchi mmoja akapiga simu akauliza hatua ambazo anatakiwa kuzifuata ikiwa atapata ujumbe wa kuudhi au matusi kwenye simu yake. Akasema kwa mfano wakati wa campaign za uchaguzi wa mwaka huu ikitokea akapata ujumbe wa kuudhi kwamba "Chagua CCM" achukue hatua gani kushughulika na ujumbe huu wa maudhi kwake ?!

Yaani imefikia hata ujumbe wa campaign wa CCM wengine wanachukulia kwamba ni ujumbe wa kuudhi (kama matusi vile)!.

Kweli watu wana hasira na CCM !

Chama kimoja kukaa madarakani kwa zaidi ya miaka 50 lazima kitachukiwa hata kama kitajitahidi kutenda mema. Watu wangependa waoine mabadiliko. CCM kinaweza kikajinasibu kwa kujenga barabara nyingi za lami, lakini swali zina ubora kiasi gani. Kabla hatujapongeza juhudi hizo za serikali tujiulize, je barabara hizi zimejengwa kwa pesa zetu au kwa mikopo? Kama kwa sasa deni linakaribia trillion 40 kutoka trillioni 7 wakati serikali ikiingia madarakani hatuna sababu kubwa ya kupongeza. Baba akijenga nyumba nyingi kwa fedha ya kukopa kutoka benki watoto wake hawana sababu ya kushangilia kwani iko siku akishindwa kulipa deni zitapigwa mnada. Huwezi kushangilia kujenga nyumba nyingi za kisasa wakati hati za nyumba hizo hunazo. Nyumba ni hati, kama huna hati nyumba hiyo si ya kwako. Tutafakari.
 
Kuna vijana juzi walipeana adhabu kama mmoja atashindwa kutimiza majukumu waliyowekeana, moja ya adhabu yao ni kuvaa Tshirt na kofia ya CCM kwa siku nzima ama fine ya 100,000/-.

Cha ajabu vijana wengi walikubali kulipa hiyo fine.
Hata mimi nalipa hio faini
 
Chama kimoja kukaa madarakani kwa zaidi ya miaka 50 lazima kitachukiwa hata kama kitajitahidi kutenda mema. Watu wangependa waoine mabadiliko. CCM kinaweza kikajinasibu kwa kujenga barabara nyingi za lami, lakini swali zina ubora kiasi gani. Kabla hatujapongeza juhudi hizo za serikali tujiulize, je barabara hizi zimejengwa kwa pesa zetu au kwa mikopo? Kama kwa sasa deni linakaribia trillion 40 kutoka trillioni 7 wakati serikali ikiingia madarakani hatuna sababu kubwa ya kupongeza. Baba akijenga nyumba nyingi kwa fedha ya kukopa kutoka benki watoto wake hawana sababu ya kushangilia kwani iko siku akishindwa kulipa deni zitapigwa mnada. Huwezi kushangilia kujenga nyumba nyingi za kisasa wakati hati za nyumba hizo hunazo. Nyumba ni hati, kama huna hati nyumba hiyo si ya kwako. Tutafakari.
Issue sio ubora, issue ni fedha zilizotumiwa kujenga zimetoka wapi?.........Jibu ni Mkopo.......Kama ni mkopo, uliidhinishwa na bunge kama sheria inavyosema?

Jibu ni hapana, kwa nini hazikuidhinishwa? Jibu ni kwamba mikopo ni aina mpya ya UFISADI, no body knows how much kimekopwa, kwa ajili gani na kutoka vyanzo vipi........Deni la taifa sasa lipo kwenye Tsh trilioni 30+. kwa mwendo huu CCM itaikabidhi nchi kwa waliowakopesha muda si mrefu.
 
Watu hawahitaji kabisa ccm kuisikia na hata hao watumishi wao wanalijua hilo.
 
Back
Top Bottom