usawa wa kulia
'To generalize is to be an idiot', unaposema mnakatwa fedha halafu mnapewa huduma mbovu, ni wewe na nani? Wa wapi? Toka lini? Huduma gani mbovu uliyopata? asehemu gani ulikopatia hiyo "huduma mbovu"?
Sasa ;
You should understand hizo kadi zinatofautiana; utaona brown card, green card, hivyo huduma ziko restricted kulingana na aina ya kadi.
Ingawaje unaona fedha unayokatwa ni "kubwa" bado sidhani kama inakidhi matibanu/ huduma za afya unayopata, Say unakatwa 75,000/= or 100,000/=Tshs na una dependants kadhaa! Hivi unafikiri hiyo inatosha hata kwa mwezi (say consultation ya familia nzima)?, sawa naelewa si kila mwezi mtaugua au mtafanya check up!
Umekwisha fikiria vipi kuhusu dawa za milioni tisa hadi ishirini na saba za saratani? vipi kuhusu dialysis? Umekwisha fikiria kuhusu vipimo vikubwa kama MRI na CT Scan, umekwisha fikiria operation hasa ulimwengu huu wa ajali kila leo?
Umefikiria kuhusu watu wenye magonjwa ya muda mrefu na yenye kuhitaji dawa mf. Shinikizo la damu (Hypertension/High Blood Pressure), Kisukari/Diabetes, Magonjwa ya mifupa, figo n.k then ulinganishe na hicho kiasi "kikubwa" unachodhani unakatwa?
I agree with you, kuwa kadi wakati fulani haisaidii (lakini issue hapa si upatikanaji wa huduma kwa kadi, ila ni huduma zenyewe), mfano hospitali ndogo, Vituo vya afya n.k.
Pia kuna baadhi ya dawa huduma (vipimo na dawa) HAVIPASWI kuwa katika sehemu hizo(health centre, hospitali ndogo) na hata kama daktari akiandika utarudishwa tu.
Mfuko wa bima ya taifa (NHIF), huchelewesha malipo kwa vituo vya afya na hospitali (isipokuwa kwa hospitali "kubwa"), sasa ucheleweshwaji huu, humuathiri mteja kwa madaktari/ watoa huduma kuwaepuka wateja/ wagonjwa kwa kuwa pesa yao hucheleweshwa pia.
Sasa restriction, hizi ndizo zenye kuleta usumbufu, lakini it is 'insane' dunia ya leo kukaa bila bima, hasa ya afya.