Kweli serikali ya sasa ni legelege

Balozi Chriss

Senior Member
Jan 21, 2011
153
16
Leo usiku katika kipindi cha "Usiku wa habari" kupitia televisheni TBC walikuwa wameandaa habari inayohusu ujenzi wa shule za sekondari huko Kinondoni(Kimara) Dar es Salaam.
Nilitamani kuanza safari ya kwenda Ikulu kumwambia Baba Riz awashe Tv ili aone ni kwa jinsi gani serikali yake imeoza sana.Yaani wakandarasi wa wilaya wanafisadi pesa mpaka ujenzi umeshindwa kamilika.Wanafuzi wale takribani 1000 inabidi waingie shule kwa mtindo wa zamu(shift).Doh madarasa wanayotumia kwa sasa ni vyumba 3 na tena havina sakafu ni vumbi tele .
Jamani watanzania wenzangu haya mambo ya utendaj ya hii serikali sio ya kufumbia macho.
Nawasilisha hoja....
 
Back
Top Bottom