Kweli Mungu hana upendeleo?

Kweli Mungu hana upendeleo?

Rehema na huruma ya Mwenyezi Mungu haimaanishi kwamba dunia itakuwa mahali pasipo na majaribu. Maisha ya duniani yameumbwa kuwa na furaha na huzuni, afya na maradhi, utajiri na umasikini. Hali hizi huwa sehemu ya mtihani wa maisha ya mwanadamu, si ishara kwamba Mungu amekosa huruma. Rehema yake inaonekana kwa kuwapa wanadamu uhai, akili ya kutambua mema na mabaya, na nafasi ya kubadilika kila siku.

Kuhusu watu kuteseka kwa sababu ya matapeli wanaotumia jina la Mungu, hilo mara nyingi si kimya cha Mungu bali ni matokeo ya matendo ya binadamu wenyewe. Mwanadamu amepewa uhuru wa kuchagua; anaweza kufanya mema au mabaya. Watu kama wanaotumia dini kujinufaisha wanatumia vibaya uhuru huo, na dhuluma hiyo hubeba matokeo yake. Hivyo, udanganyifu wa mtu kama Josephat Gwajima Mwamposa au mtu mwingine yeyote anayehusishwa na kashfa za kutumia dini hauwezi kuwa kipimo cha huruma ya Mungu, bali ni kipimo cha tabia ya mwanadamu.

Kwa hiyo mateso mengi tunayoyaona duniani mara nyingi yanatokana na udhaifu, tamaa, na ujinga wa wanadamu, si kwa sababu Mungu hana huruma. Ndiyo maana historia inaonyesha pia kuwa pamoja na mateso, bado kuna watu wanaopona, wanasaidiana, na wanapata farajahayo nayo ni sehemu ya rehema inayodhihirika katika maisha.
Ni nani aliyeumba uovu kwa mara ya kwanza kabisa?
 
Back
Top Bottom