Kweli Max Ndiye Yeye: Kwanini Sina Hofu

Kweli Max Ndiye Yeye: Kwanini Sina Hofu

Mwanakijiji wewe una sehemu ya haya yanayoendelea. Pale wapinzani walipolalamika kuwa serikali hii inatupeleka kwenye udikteta, wewe ulikenua meno aisee, nakuchukia kweli: nisamehe tuu, maana siwezi kuzuia chuki yangu kwako. Ulitetea madudu ya JPM tangu mwanzo ya ukandamizaji wa demokrasia nchini. Aisee kwa dhati ya moyo wangu nakuchukia wewe, umekuwa sehemu ya haya tuliyofikia na tunakoenda, huwezi kujivua haya. I hate you. Kutoka kuwa mtu niliyependa kumsoma makala zake mpaka kuwa mtu ninayekuchukia. NAKUCHUKIA NA VIONGOZI WAKANDAMIZI WA CCM ULIOUNGANA NAO KUTUUMIZA. I HATE YOU
Hii comment haitoki kwa GT, kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni, ukipendezwa nayo ni heri kwako, vinginevyo kumchukia mtu kisa yupo tofauti na maoni au mawazo yako ni kukosa busara.
 
Kwani polisi hawafahamu kwamba members wanatumia pen names? Kama ni hilo hawana pa kushika, they need to come up with something else.
Nchi yetu hii maskini, techolojia ya habari iko mbali sana. Halafu eti tunajidai kupata maendeleo, kweli?
Haiwezekani nchi ishindwe kupata taarifa za watumiàji wa chombo kama JF, sasa technologically, polisi wetu wataweza kipi? Kama hawawezi waombe msaada kwa wenzao wa Interpol. Otherwise, ni kujionyesha uwezo Mdogo ktk taaluma hiyo.
 
Max watamwachia hawana ujanja. Hili liwe somo kwa watumiaji wa JF kuweka mijadala ya maana na sio mipasho. I hope people will learn from this. Hili jambo lilitukumba nyuma wakati bado JF ipo changa nakumbuka tulipoteza some members hapa, kuna watu hawastahili kuandika pumba zao humu. Turekebishe na turudishe ile JF ya mijadala, kama unapenda umbeya, mipasho na porojo nenda kwenye sports, mipasho nk. Kwenye mambo ya kuliendeleza taifa letu tuwe more serious zaidi.
 
naona watu wanalia lia tu, nendeni kwenye facts mjadili hoja ... sio viroja ! pamoja na vision nzuri ya jamii forums ila pia ina madhara iliyosababisha kwenye jamii yetu. nyie hamuwezi kujua hizi tuhuma zinazoibuliwa humu ndani zinatumia gharama kiasi gani za serikali kuzikanusha ? ni mangapi hapa yamesemwa ila ikaja kubainika hayakuwa na ukweli ! kama issue ni uhuru wa kujielleza why not facebook,instagram na kwingineko ! je huko watu hawajielezi ? mbona huko hakufungiwi ! Jf ni nzuri ila ni lazima hatua zichukuliwe kuondoa tabia za kihuni zilizoanza kuibukia humu ndani .... na jukumu la serikali ni kusimamia sheria zilizotungwa na bunge ikiwemo sheria ya mitandao. na pia ni jukumu la msingi la kila mtanzaniakuheshimu nakufuata sheria akiwemo jamiiforum na wakurugenzi wake wote. tuache serikali ichukue hatua zinazostahiki
 
Back
Top Bottom