Kweli maisha magumu konda amliza babu

Rufiji dam

JF-Expert Member
Feb 20, 2020
3,804
8,797
Uenda wenye mamlaka wameamua kuziba masikio. Ukweli hali ya maisha ni magumu sana. Nikiwa katika safari za jiji la CPM katika matumizi ya usafiri wa umma japo unamilikiwa na wapemba na wachaga. Nilikaa na mzee wa makamo kama 65 mpk 70 umri wake, mwenye dhamana ya kukusanya pesa akaanza kuitisha wito wake mimi nikatoa 500 yangu hakuna kudaiana baba yangu akatoa Ulimboka mwekundu wa msimbazi 10 konda akasema nitakuletea chenji yako. Basi ni haya makubwa Hicha sijui. Tunaunguruma kona za Goba kuisaka mbezi sijui zile kona zililala na akili ya konda. Mzee akadai rejesho lake la chenji konda aligoma katu. Naweza kusema ni mkosi mzee akaanza kulia kwa hasira pamoja na utetezi toka kwangu na kiti cha nyuma konda alikaza hasa kuwa mzee hana anachodai. Ndani ya basi kukatokea shuhuda kuwa haya mabasi makubwa wahudumu wake ni wezi sana hasa njia za Mbagala na Gongolamboto. Ila pamoja kugoma kwake tukaja kumshinda konda ikabidi amlipe mzee wa watu ila chozi kalitoa. Nikasema kweli maisha magumu zama zile mtu mzima kulilia ten ni nadra sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna siku nilipiga tungi asubuhi ya saa moja kabla sijaenda Job, nimepiga zangu nkaridhika nikaenda panda daladala, konda kadai Hela nikampa ten,
Sasa si nkasahau kudai chenji nkashuka kufika mbele mbele huko nakumbuka kurudi kituoni gari siikumbuki na magari muda huo pia ni mengi ilibidi nigeuze zangu mzee, lakini karoho kaliniuma ten asubuh asubuhi imeenda na water 💦 😴😴
 
Mkuu kudhulumiwa haki yako hata ingekua buku inauma sana. Wala haijalishi kua unacho au huna, maisha magumu au mepesi. Pia huyo Mzee kalizwa na mengi maana tafsiri ya kilio chake yaweza kua ni masikitiko yake kwa kuitwa muongo na huyo konda ambaye yawezekana ni kama mwanae au mjukuu wake kabisa

Mo Dewji au Bahresa na utajiri wao watoe kwa mfano shilingi elfu tano kwenye kuhitaji huduma fulani halafu umwambie hajatoa hela kisha unataka afurahi na kukuchekea kisa maisha kwake ni mepesi! Hapana mkuu
 
Kuna haja gani ya kuandika ulimboka mwekundu!!!??
kwanini usiandike kiwango cha fedha kwa lugha sahihi!
unadhani wote wanajua ulimboka mwekundu ni kitu gani.....
boresha uandishi wako
 
Kuna siku nilipiga tungi asubuhi ya saa moja kabla sijaenda Job, nimepiga zangu nkaridhika nikaenda panda daladala, konda kadai Hela nikampa ten,
Sasa si nkasahau kudai chenji nkashuka kufika mbele mbele huko nakumbuka kurudi kituoni gari siikumbuki na magari muda huo pia ni mengi ilibidi nigeuze zangu mzee, lakini karoho kaliniuma ten asubuh asubuhi imeenda na water 💦 😴😴
Tungi asubuhi saa moja kabla kwenda job? Asee mimi hata unipe na hela bado sijakubali kunywa pombe asubuhi hata kama siku hiyo sitoki nyumbani.
 
Tungi asubuhi saa moja kabla kwenda job? Asee mimi hata unipe na hela bado sijakubali kunywa pombe asubuhi hata kama siku hiyo sitoki nyumbani.
Yan mimi time yoyote napiga maji, naweza amka usiku saa saba au saa nane nkafungua chupa yangu nkanywa mdogo mdogo, huku nashushia na cigar mpaka majogoo, 🤒🤒
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom