MCHUNGUZI HURU kuna kitu unakosa na kitu unajishaulisha,hebu nikuulize
wewe huo urefu ulijipa ulijichagulia uwe mrefu?
hivi hujui kuwa uwezekano wa hata wewe kuwa mfupi ulikuwepo ikiwa aliyekutokeza angetaka iwe hivyo na hata akitaka kwa wakati huu unaweza kuwa mfupi?
kwa nini unawadharau watu wafupi?
nini kinakufanya wewe uwe wa pekee na hao wafupi uwaone wasio na maana?
au unaweza kunipa utofauti au umaana au upekee ulionao tofatui na hao wafupi?
urefu wako umekuongezea siku za kuishi?ukoo wenu wote ni warefu?
mkuu hii ni dunia tu na kuna mambo yako nje ya uwezo wa kila mmoja wetu,kuna mambo ambayo watu hawapendi kuwa nayo ila kwa kuwa hawana mamlaka juu ya hayo wanakaa tu kimya wakiugulia kivyao,kwa hiyo kama umejaaliwa uzuri,urefu wa haja mshukuru muumba wako na uwasikitikie hao ambao hawakujaaliwa na sio kuanza kuwanyanyapaa na kuwachambuachambua,hata wao hawakupenda kuwa hivyo walivyo wamejikuta tu.
mwisho mkuu dunia ni tambala bovu na ni uwanja wa fujo pia hayupo komandoo wa dunia unamjua wastara?zamani alikuwaje na sasa yukoje,hii ni dunia tu mkuu leo mrefu kesho mfupi kama njiti ya kiberiti,dunia ina mengi aksidenti magonjwa na makorokoro kibao ambayo si mimi wala nani aweza kuyazuia yanatokea tu na kwa wakati wowote mkuu,take care.