jerryempire
JF-Expert Member
- Jan 4, 2017
- 5,128
- 8,648
Habari,
Leo ningependa kushare nanyi kitu kidogo hasa kupitia mahusiano jambo ambalo sikuwahi kabla huenda nikapata ushauri na hata wengine kujifunza.
Kitabia naweza kusema ni moja kati ya wale wanaume ambao ukiwa nae una uhakika wa kuwa upo salama na upo peke yako.
Kwani uwapo na mahusiano nami uko huru kuja muda wowote kwangu kuhusu simu hata ukisema uondoke nayo we nenda nayo inshort ni muwazi mno,yote inatokana na maisha niliyoyaishi ya bila wazazi especially kwenye uyatima,hivyo nimekuwa nikithamini mno mahusiano ambayo nitaingia kwani huwa nawaonea mno huruma wanawake hasa ukizingatia tabu alizozipata mama yangu kabla ya kufariki nikiwa na miaka 7.
Hivyo nilijiapiza kuwa sitaumiza mwanamke au kumnyanyasa na niliweka kiapo kama nitapata mtoto sitopenda aishi maisha kama niliyoyaishi mimi.
Miaka mitano nyuma nilifanikiwa kuanzisha mahusiano na msichana kutoka mkoa wa Mbeya,kiukweli nilitokea mno kumpenda na nilikuwa loyal kwenye mapenzi yetu,baada ya miezi 6,tulifanikiwa kufungua biashara ya duka.
Biashara ilikwenda vizuri kutokana na uzoefu nlokuwa nao katika biashara,biashara ilivyokuwa nzuri nikapata bahati ya kwenda kujiongeza kielimu huku nikimuacha mwenzangu aendelee na biashara kwa minajili ya nikimaliza mwaka wa kwanza nikirudi tumalizie hatua nyingine za posa.
Kufupisha tu story ndani ya ile miezi minne ya mwanzo mwenzangu alikuwa ameanza kubadilika mno kiasi kilichoanza kunipa mashaka likizo ya kwanza ilipokwisha nilivyorudi hakuwa yule ambae ninamfahamu kimavazi na hata tabia.Kama mwanaume machale yakanicheza katika kuchunguza chunguza nikagundua kuwa mwenzangu tayari yupo na mtu mwengine nilimtafuta nikaongea nae kuhusu hilo alikataa kata kata pia akawa na jeuri mie bkasema siyo mbaya nikapotezea.
Likizo ilivyokwisha nikarudi zangu masomoni,miezi miwili baada ya kurud masomoni akawa hapatikani wala hana mawasiliano na mimi,Nilivyorudi nikakuta mali za duka zote zimeuzwa kiwanja tulichonunua kauza inshort alikuwa ameuza investment zote tulizokuwa tumeanzisha pamoja.
Hakika nilikonda na kutokea kukonda mno maana nilihisi future yangu imeharibika kabisa zaidi nilipopata habari kuwa anaishi na mwanaume mwengine na ni mjamzito,kutokana na company niliyokuwa nayo kwa dada zangu na hata familia niliteseka na nikakaa sawa nikaamua ku move on.
Aliendelea na maisha yake nami nikaendelea na maisha yangu hadi siku ya juzi nilipokutana nae kariakoo akiuza nyanya na mtoto mgongoni kariakoo.
Sikubahatika kumuona ila yeye ndiye aliyeniona kiukweli alikuwa akilia mno na kuwa kama movie pale sokoni huku akinisihi nimsamehe,kwa ambae ananifahamu ni mtu mwenye huruma mno lakini kila alivyokuwa akilia na kuniomba msamaha nilikuwa namuona kama katuni mbele ya macho yangu watu walinisihi sana nimchukue tukae sehemu tuongee ili kuepusha ile aibu pale,nikafanikiwa kumchukua mpka kwenye kimgahawa hakika aliyapitia mengi sana mateso na hata misukosuko na huyo aliyekuwa nae.
Baada ya maelezo mengi nilimsamehe na aliniomba turudiane tuwe kama mwanzo,Baada ya kuona yuko serious na hilo la kurudiana nikamuomba niende mara moja toilet nilivyofika toilet kuna jamaa nikamuagiza ampelekee elf 10 pale alipo ili alipie bili ya chakula mimi nilivyompotea wala hakujua wala sikumuaga.Kiuchumi siko vizuri sana but huwa najiuliza tu ni kwanini dada zetu mnapopata wabaume wenye mapenzi ya dhati huwa mnatuona kama wajinga?
Tambueni wengine tupo hivyo sababu ya maisha tuliyoyaishi.
Leo ningependa kushare nanyi kitu kidogo hasa kupitia mahusiano jambo ambalo sikuwahi kabla huenda nikapata ushauri na hata wengine kujifunza.
Kitabia naweza kusema ni moja kati ya wale wanaume ambao ukiwa nae una uhakika wa kuwa upo salama na upo peke yako.
Kwani uwapo na mahusiano nami uko huru kuja muda wowote kwangu kuhusu simu hata ukisema uondoke nayo we nenda nayo inshort ni muwazi mno,yote inatokana na maisha niliyoyaishi ya bila wazazi especially kwenye uyatima,hivyo nimekuwa nikithamini mno mahusiano ambayo nitaingia kwani huwa nawaonea mno huruma wanawake hasa ukizingatia tabu alizozipata mama yangu kabla ya kufariki nikiwa na miaka 7.
Hivyo nilijiapiza kuwa sitaumiza mwanamke au kumnyanyasa na niliweka kiapo kama nitapata mtoto sitopenda aishi maisha kama niliyoyaishi mimi.
Miaka mitano nyuma nilifanikiwa kuanzisha mahusiano na msichana kutoka mkoa wa Mbeya,kiukweli nilitokea mno kumpenda na nilikuwa loyal kwenye mapenzi yetu,baada ya miezi 6,tulifanikiwa kufungua biashara ya duka.
Biashara ilikwenda vizuri kutokana na uzoefu nlokuwa nao katika biashara,biashara ilivyokuwa nzuri nikapata bahati ya kwenda kujiongeza kielimu huku nikimuacha mwenzangu aendelee na biashara kwa minajili ya nikimaliza mwaka wa kwanza nikirudi tumalizie hatua nyingine za posa.
Kufupisha tu story ndani ya ile miezi minne ya mwanzo mwenzangu alikuwa ameanza kubadilika mno kiasi kilichoanza kunipa mashaka likizo ya kwanza ilipokwisha nilivyorudi hakuwa yule ambae ninamfahamu kimavazi na hata tabia.Kama mwanaume machale yakanicheza katika kuchunguza chunguza nikagundua kuwa mwenzangu tayari yupo na mtu mwengine nilimtafuta nikaongea nae kuhusu hilo alikataa kata kata pia akawa na jeuri mie bkasema siyo mbaya nikapotezea.
Likizo ilivyokwisha nikarudi zangu masomoni,miezi miwili baada ya kurud masomoni akawa hapatikani wala hana mawasiliano na mimi,Nilivyorudi nikakuta mali za duka zote zimeuzwa kiwanja tulichonunua kauza inshort alikuwa ameuza investment zote tulizokuwa tumeanzisha pamoja.
Hakika nilikonda na kutokea kukonda mno maana nilihisi future yangu imeharibika kabisa zaidi nilipopata habari kuwa anaishi na mwanaume mwengine na ni mjamzito,kutokana na company niliyokuwa nayo kwa dada zangu na hata familia niliteseka na nikakaa sawa nikaamua ku move on.
Aliendelea na maisha yake nami nikaendelea na maisha yangu hadi siku ya juzi nilipokutana nae kariakoo akiuza nyanya na mtoto mgongoni kariakoo.
Sikubahatika kumuona ila yeye ndiye aliyeniona kiukweli alikuwa akilia mno na kuwa kama movie pale sokoni huku akinisihi nimsamehe,kwa ambae ananifahamu ni mtu mwenye huruma mno lakini kila alivyokuwa akilia na kuniomba msamaha nilikuwa namuona kama katuni mbele ya macho yangu watu walinisihi sana nimchukue tukae sehemu tuongee ili kuepusha ile aibu pale,nikafanikiwa kumchukua mpka kwenye kimgahawa hakika aliyapitia mengi sana mateso na hata misukosuko na huyo aliyekuwa nae.
Baada ya maelezo mengi nilimsamehe na aliniomba turudiane tuwe kama mwanzo,Baada ya kuona yuko serious na hilo la kurudiana nikamuomba niende mara moja toilet nilivyofika toilet kuna jamaa nikamuagiza ampelekee elf 10 pale alipo ili alipie bili ya chakula mimi nilivyompotea wala hakujua wala sikumuaga.Kiuchumi siko vizuri sana but huwa najiuliza tu ni kwanini dada zetu mnapopata wabaume wenye mapenzi ya dhati huwa mnatuona kama wajinga?
Tambueni wengine tupo hivyo sababu ya maisha tuliyoyaishi.