Setfree
JF-Expert Member
- Dec 25, 2024
- 5,527
- 7,121
Mara nyingi, tumekuwa tukisikia taasisi za kijamii, wanaharakati, wananchi nk wakiilaani nchi fulani au viongozi wa kisiasa kwa madai kwamba wamekosea au kutenda jambo linalowaletea maumivu.
Wakati mwingine watu wenye dini nao husikika wakitamka maneno ya laana dhidi ya wale wanaoona wamekosea. Na wengine huwaombea wakosaji wapatwe na mabaya kama kifo, magonjwa au ajali. Kwanini mara nyingi, laana hizo hazitimii au haziwapati wanaolaaniwa?
Sababu kubwa ni kwamba Mungu hapendi tuwalaani wenzetu. Maandiko yanasema hivi katika Warumi 12:14
"Wabarikini wale wanaowaudhi, barikini wala msilaani..” Tafsiri nyingine ya andiko hilo inasema: "Watakieni baraka wote wanaowadhulumu nyinyi; naam, watakieni baraka na wala msiwalaani."
Maneno ya laana yanajenga mazingira ya kisasi, chuki, na kutotubu. Lakini baraka—hata kwa maadui—hufungua mlango wa neema, uponyaji, na mageuzi ya kweli. Mungu hajihusishi na laana zinazotokana na hasira za kibinadamu.
Laana inayotoka kwa mtu asiyeongozwa na Roho wa Mungu, haipati kibali kwa Mungu, ndio sababu laana nyingi za watu haziwapati wanaolaaniwa.
Kama kuna nchi inayolaaniwa sana ni Israeli. Lakini badala ya kulaanika, tunaona ikiendelea kustawi. Na wanaoilaani wenyewe ndio wanapatwa na mabaya!
Wakati mwingine watu wenye dini nao husikika wakitamka maneno ya laana dhidi ya wale wanaoona wamekosea. Na wengine huwaombea wakosaji wapatwe na mabaya kama kifo, magonjwa au ajali. Kwanini mara nyingi, laana hizo hazitimii au haziwapati wanaolaaniwa?
Sababu kubwa ni kwamba Mungu hapendi tuwalaani wenzetu. Maandiko yanasema hivi katika Warumi 12:14
"Wabarikini wale wanaowaudhi, barikini wala msilaani..” Tafsiri nyingine ya andiko hilo inasema: "Watakieni baraka wote wanaowadhulumu nyinyi; naam, watakieni baraka na wala msiwalaani."
Maneno ya laana yanajenga mazingira ya kisasi, chuki, na kutotubu. Lakini baraka—hata kwa maadui—hufungua mlango wa neema, uponyaji, na mageuzi ya kweli. Mungu hajihusishi na laana zinazotokana na hasira za kibinadamu.
Laana inayotoka kwa mtu asiyeongozwa na Roho wa Mungu, haipati kibali kwa Mungu, ndio sababu laana nyingi za watu haziwapati wanaolaaniwa.
Kama kuna nchi inayolaaniwa sana ni Israeli. Lakini badala ya kulaanika, tunaona ikiendelea kustawi. Na wanaoilaani wenyewe ndio wanapatwa na mabaya!