Kwanini wananchi wamehamasika sana na BVR?

Kwanini wananchi wamehamasika sana na BVR?

Joined
Jun 9, 2011
Posts
92
Reaction score
53
Umofia Kwenu, Wadau nimetembelea vituo kadhaa vya kujiandikisha naona hamasa imekuwa kubwa, hivi kwanini? watu wanataka mabadiliko? kweli watapiga kura? au wanataka vitambulisho kwa ajili ya kufungua account bank? nashindwa kuelewa.

Nahisi kama lilikuwa chezo ili watu wasijitokeze ili wahafidhina wa CCM ndo wajiindikishe, lakini upepo umebadilika, kila mtu kadhamiria
 
Pamoja na nia nzuri ya kutaka kutimiza haki yetu ya kidemokrasia, lakini uzito zaidi umeelemea kwenye kuwa na utambulisho kwa ajili ya kusajili laini za simu, kufungua 'account bank' na kadhalika. Kwahiyo usishangae upigaji kura ukawa chini ya asilimia thalathini (30%) ya waliojiandikisha.
Kishimbe wa Kishimbe JF MWANZA. (KARIBUNI TUNGANGAMALE KURURUNGANYA!)
 
Umofia Kwenu, Wadau nimetembelea vituo kadhaa vya kujiandikisha naona hamasa imekuwa kubwa, hivi kwanini? watu wanataka mabadiliko? kweli watapiga kura? au wanataka vitambulisho kwa ajili ya kufungua account bank? nashindwa kuelewa, nahisi kama lilikuwa chezo ili watu wasijitokeze ili wahafidhina wa CCM ndo wajiindikishe, lakini upepo umebadilika, kila mv kadhamiria

Mkuu, haha watu wa makerting wanasema ukiona wateja wamekosa hamasa na bidhaa yako basi unatakiwa ufanye STIMULATION AND CONVENTION MARKETING na njia mojawapo ni kubadilisha product features, sasa mkuu hivi vikadi vya sasa ni vizuri(wamebadili features) kuliko vile vya zamani , vijana wa "kwetu" wamevipachika jina viATM. watu wanataka hivyo vikadi na wala sio kupiga kura!
Aione: Mkoroshokigoli
 
Last edited by a moderator:
Maelfu ya watu wasio raia halifu hasa wakimbizi kutoka Burundi wanaojiita waha ndio wanajaza foleni.
 
Ni kweli watu wanavihitaji sana hivyo vitambulisho kwa mambo mengine, ukizingatia kuwa vinatumika sana kwenye kusajili line za simu, kuweka dhamana, kufungua account bank n.k, nilishuhudia pale Iringa watu walikuwa wanakwenda kujiandikisha vijiji vya jirani ili wapate vitambulisho.
 
Hata kama watu wengi nia yao ni kupata vitambulisho tu, bado hizi ni habari nzuri kwa wadau wa Uchaguzi Mkuu. Kama watu wengi wana "vitambulisho" hivyo, ni rahisi kupitia katika kampeni, kuwageuza watu hao wenye "vitambulisho", kuwa wapiga kura. Miaka iliyopita, kutokana na watu wengi kukosa kujiandikisha, wakati wa kampeni mikutano ilikuwa inajaa umati wa watu wasio na kadi za kupigia kura, lakini sasa mikutano itajaa hao wenye "vitambulisho", na baada ya kuhamasika, watakuwa wapiga kura.
 
2004 ilikua hivi watu wengi walijitojeza lakini wapiga kura wakawa wachache, ushawishi wa kupiga kura unategemea nani anagombea lakini ninadhani wapiga kura watapungua zaidi kama EL stagombea.
 
Hilo Halina Ubishi Kwamba Watanzania Wameichoka Ccm Na Njia Ya Kuiondoa Ni Kupiga Kura, Na Hakuna Lingine Na Hii Ni Habari Mbaya Kwa Ccm
 
Mkuu, haha watu wa makerting wanasema ukiona wateja wamekosa hamasa na bidhaa yako basi unatakiwa ufanye STIMULATION AND CONVENTION MARKETING na njia mojawapo ni kubadilisha product features, sasa mkuu hivi vikadi vya sasa ni vizuri(wamebadili features) kuliko vile vya zamani , vijana wa "kwetu" wamevipachika jina viATM. watu wanataka hivyo vikadi na wala sio kupiga kura!
Aione: Mkoroshokigoli

Upo sahihi kabisa mdau,watu wanahitaji kadi na si kwa ajili ya kupiga kura.Kwa usumbufu wanaoupata kwenye kujiandikisha naamini watarudia ya 2010 hawatapiga kura,kwa sababu zoez zima la uandikishaji ni adhabu hata maombi ya VISA ya kwendA USA hayawi vile.Watu wanataka kadi kwa ajili ya matumizi yao ya kila siku kama nyaraka muhimu itakiwayo na mamlaka au taasisi mbalimbali.
 
Umofia Kwenu, Wadau nimetembelea vituo kadhaa vya kujiandikisha naona hamasa imekuwa kubwa, hivi kwanini? watu wanataka mabadiliko? kweli watapiga kura? au wanataka vitambulisho kwa ajili ya kufungua account bank? nashindwa kuelewa.

Nahisi kama lilikuwa chezo ili watu wasijitokeze ili wahafidhina wa CCM ndo wajiindikishe, lakini upepo umebadilika, kila mtu kadhamiria

Kiukweli wengi nikiwauliza huku kitaa wanasema wanataka vitambulisho!
 

Upo sahihi kabisa mdau,watu wanahitaji kadi na si kwa ajili ya kupiga kura.Kwa usumbufu wanaoupata kwenye kujiandikisha naamini watarudia ya 2010 hawatapiga kura,kwa sababu zoez zima la uandikishaji ni adhabu hata maombi ya VISA ya kwendA USA hayawi vile.Watu wanataka kadi kwa ajili ya matumizi yao ya kila siku kama nyaraka muhimu itakiwayo na mamlaka au taasisi mbalimbali.
Watu walivyoichoka CCM,Wamedhamiria kuichinjia Baharini kimyakimya.
 
Watu wanataka vitambulisho ndio maana wako radhi kuvumilia adha zote wakati wa kujiandikisha. Sasa subiri kimbembe siku ya uchaguzi amini nakwambia siku hiyo kama kutakuwa hivi hivi watakao piga kura ni aslimia 25% tu
 
Watu wanataka vitambulisho ndio maana wako radhi kuvumilia adha zote wakati wa kujiandikisha. Sasa subiri kimbembe siku ya uchaguzi amini nakwambia siku hiyo kama kutakuwa hivi hivi watakao piga kura ni aslimia 25% tu
Sidhani kama nia yao ni kitambulisho watu wanataka mabadiliko tena wakati uu vijana ni wengi sana. Watu siku hizi wamebadilika sana tofauti na zamani
 
Tumeambiwa bila kupiga kura hakuna mabadiriko tulifanya makosa 2010 kwa kutopiga kura.tumeelewa maana na umuhimu wa upinzani bungeni
 
Back
Top Bottom