Kwanini Wanafunzi Wanaosoma Shule za Masista Wanawaona Masista Kama Makatili Sana Wasiofaa

Filosofia ya Rorya

JF-Expert Member
Sep 20, 2021
3,214
3,587
Uchunguzi wangu umebaini kuwa asilimia kubwa sana ya wanafunzi waliosoma shule za Masista hawawapendi Watawa hao na wala hawapendi kurudi kusoma shule hizo.

Aidha, wengi wa wanafunzi hao wanawapenda sana Ma-father (Mapadre) kuliko Masista.

Utasikia baadhi ya wanafunzi hususan wa kike wakisema "sina hamu na mtu anayeitwa Sister na wala sitamani kumuona kwa macho yangu kama siyo kukutana naye kwenye maisha yangu mazima, hata kwenye Misa nikienda sitamani kuwaona"

Mwanafunzi mmoja alimwambia mzazi wake kuwa "mimi siendi tena F5 shule ya Masista, ukilipa ada huko basi kasome mwenyewe, siyo mimi"

Humu jamvini kuna wadau waliosoma seminari na seminari ndogo za Kikatoliki tunaomba kupata maarifa kwenu yatayojibu maswali haya:
1. Mnadhani tatizo ni nini?

2. Kipi kibadilike kwa Masista au hata kwenye mtaala wa kuwaandaa Masista?

3. Je, Masista ni walezi wazuri au wabomoaji wazuri?

4. Kwanini Masista kama watumishi wa Mungu waonekane hawafai?

5. Ma-father wana kipi ambacho Masista hawana?

6. Kama Kanisa ni moja, shule moja kwanini mifumo ya malezi iwe tofauti kati ya Ma-father na Masista?

Tujadili kwa nia ya kupata maarifa yenye ufumbuzi na faida kwetu na kizazi kijacho.
 
Kwa inavyosemekana, mwanamke yeyote ambaye hajazaa au hazai na pengine ameshapita umri wa kuzaa, mara nyingi huwa ana tatizo la kisaikolojia. Kwahiyo pamoja na hizo shule kuwa strict lakini kuna vitu vingine vidogo vidogo huwa ni vya kupotezea kama mama au mzazi au mlezi. Sasa masista ni walezi tu, sio mama wala wazazi. Na ukikuta sista ni mkatili ni mkatili haswa. Ukimkuta anawahenyesha watoto wa kike ndo utaelewa. Kuna sista mmoja alitulea kidogo tukiwa wadogo ni rafiki wa mama yangu, alikuwa ni katili balaa. Nadhani mwanamke ameumbwa afanye mapenzi maishani, hii ya kukaa bila kupewa dude inawaletea stress za kufa mtu, matokeo yake wanazimalizia kwa watoto wa watu.
 
Mimi nimesoma shule yenye masista,

Nitawaambia niliyoyaona tu, kujumuisha watu siwezi.

Masista wa nchi za nje walikua wanajali sana, walikua hawachapi na wakikukuta unachapwa wanakutetea.

Na mapadri hivyo hivyo....

Ila sasa kuna huyo matron, ni mtanzania alikua sister, alikua mkali sana mpaka wanafunzi walimbaka...

Na hata mama yangu alisoma shule ya masista wakitanzania anasema ni wakatili sana.
 
Uchunguzi wangu umebaini kuwa asilimia kubwa sana ya wanafunzi waliosoma shule za Masista hawawapendi Watawa hao na wala hawapendi kurudi kusoma shule hizo.

Aidha, wengi wa wanafunzi hao wanawapenda sana Ma-father (Mapadre) kuliko Masista.

Utasikia baadhi ya wanafunzi hususan wa kike wakisema "sina hamu na mtu anayeitwa Sister na wala sitamani kumuona kwa macho yangu kama siyo kukutana naye kwenye maisha yangu mazima, hata kwenye Misa nikienda sitamani kuwaona"

Mwanafunzi mmoja alimwambia mzazi wake kuwa "mimi siendi tena F5 shule ya Masista, ukilipa ada huko basi kasome mwenyewe, siyo mimi"

Humu jamvini kuna wadau waliosoma seminari na seminari ndogo za Kikatoliki tunaomba kupata maarifa kwenu yatayojibu maswali haya:
1. Mnadhani tatizo ni nini?

2. Kipi kibadike kwa Masista au hata kwenye mtaala wa kuwaandaa?

3. Je, Masista ni walezi wazuri au wabomoaji wazuri?

4. Kwanini Masista kama watumishi wa Mungu waonekane hawafai?

5. Ma-father wana kipi ambacho Masista hawana?

6. Kama Kanisa ni moja, shule moja kwanini mifumo ya malezi iwe tofauti kati ya Ma-father na Masista?

Tujadili kwa nia ya kupata maarifa yenye ufumbuzi na faida kwetu na kizazi kijacho.
1. Mimi nimesoma seminari ya Maua.
2. Kuna mambo mengi tulikuwa haturuhusiwi kufanya ambayo katika shule nyingine yalikuwa ya kawaida. Mfano, sisi hatukuruhusiwa kulala wanafunzi wawili kitanda kimoja, lakini nilikuwa nasikia kuna baadhi ya shule wanafunzi walikuwa wanaruhusiwa.
3. Sisi hatukuruhusiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na wasichana, isipokuwa tuliruhusiwa kuwa marafiki wa kawaida wa kutembeleana na hata kusaidiana masomo. Shule nyingine mtu akiwa na girlfriend au boyfriend siyo issue.
4. Sisi tulikuwa na wastani fulani wa kufaulu na kama mwanafunzi alishindwa kufikisha huo wastani (generally siyo kwa bahati mbaya) alishauriwa atafute shule nyingine na mwalimu wetu mkuu alikuwa akiwatafutia wanafunzi wa aina hiyo nafasi katika shule nyingine ambapo surprisingly walioenda kusoma huko walifaulu vizuri pia.
5. Wasichana wengi wanataka kuwa 'handled softly' hata pale ambapo ni kwa faida yao. Masista wamefundishwa kuvumilia magumu na hata ku'suspend' baadhi ya mambo kwa sababu ya masomo na kufaulu vizuri darasani. They are for the good of girl students.
6. Vision ya wasichana walio wengi ni kusoma huku una boyfriend anayekuletea vitu na hata kiwezekana anayekupeleka sehemu weekend hata kulala huko na kurudi after one or two or three days. Masista hawawezi ku'entertain' jambo kama hilo kwa sababu kwanza itakuwa scandal kwao na pia siyo njia ya kumsaidia mtoto wa kike afanikiwe katika maisha yake. Kama anataka kufanya anayotaka asubiri akienda likizo (madudu yote anayotaka afanye huko na baada ya likizo ayaache hukohuko).
7. Katika mazingira haya ambayo wasichana wanatambiana nani ana 'vitu vikali' zaidi na wenzao katika shule ambazo mambo yanajiendeaendea tu, lazima wasichana waone kama wanabwa unfairly.
8. Lakini hata shule ambazo si za masista ambazo zina masharti magumu kwa wasichana ufaulu wao huwa ni mzuri sana na hata hizo shule wasichana wanaopenda mambo 'soft soft' hawazipendi pia.
9. Kusema masista kwa vile hawazai ni wakatili ni 'bullshit' kwa sababu wazazi wanazaa ni wakatili pia na baadhi yao hata wanaua watoto wao. Ukatili siyo attribute ya sista. Ndivyo binadamu tulivyo. Na haiwezekani hata kama kuna sista katili ikawa shule nzima masista wakawa wakatili na kwa vile wazazi hutafiti kwanza shule gani nzuri inayowafaa watoto wao hawawezi kumpeleka shule ambayo wanajua masista ni wakatili na hakuna shule kama hiyo. Hii is a 'mind invention' - taja shule ambayo masista ni wakatili na wazazi wamepeleka watoto wao huko kama ipo.
10. Utafiti wako ulioufanya pengine uliufanya kwa wale ambao wana negative attitude na masista kwa sababu kuna wasichana wengine na hata watu wazima ambao walisoma shule za masista wanaona kwamba walipata msingi mzuri wa elimu na maisha na wanashukuru kwamba walipata nafasi kusoma katika hizo shule.
 
Masista wako straight kwenye kusimamia maadili ya wanafunzi, hasa wa kike, na hiyo ndio sababu ya kuwajengea discipline inayowapa ufaulu wanaoturingishia huku mitaani, lakini kwasababu akili zao bado ndogo hawajui hili.

Kama walitaka uhuru wangeenda shule nyingine mbona zipo nyingi tu, wazazi ndio wanajua wapi wapeleke watoto wao kwa ajili ya kuwajengea maisha ya baadae, wakati watoto kwa sababu ya age wanawaza vitu vya kitoto toto tu.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Uchunguzi wangu umebaini kuwa asilimia kubwa sana ya wanafunzi waliosoma shule za Masista hawawapendi Watawa hao na wala hawapendi kurudi kusoma shule hizo.

Aidha, wengi wa wanafunzi hao wanawapenda sana Ma-father (Mapadre) kuliko Masista.

Utasikia baadhi ya wanafunzi hususan wa kike wakisema "sina hamu na mtu anayeitwa Sister na wala sitamani kumuona kwa macho yangu kama siyo kukutana naye kwenye maisha yangu mazima, hata kwenye Misa nikienda sitamani kuwaona"

Mwanafunzi mmoja alimwambia mzazi wake kuwa "mimi siendi tena F5 shule ya Masista, ukilipa ada huko basi kasome mwenyewe, siyo mimi"

Humu jamvini kuna wadau waliosoma seminari na seminari ndogo za Kikatoliki tunaomba kupata maarifa kwenu yatayojibu maswali haya:
1. Mnadhani tatizo ni nini?

2. Kipi kibadike kwa Masista au hata kwenye mtaala wa kuwaandaa?

3. Je, Masista ni walezi wazuri au wabomoaji wazuri?

4. Kwanini Masista kama watumishi wa Mungu waonekane hawafai?

5. Ma-father wana kipi ambacho Masista hawana?

6. Kama Kanisa ni moja, shule moja kwanini mifumo ya malezi iwe tofauti kati ya Ma-father na Masista?

Tujadili kwa nia ya kupata maarifa yenye ufumbuzi na faida kwetu na kizazi kijacho.
Hakuna kitu kama hicho. Umelishwa matango pori.
 
Watoto wengi age ya secondary wanakuwa kwenye foolish age hawataki kupangiwa kitu
Kwahiyo masisiter inabidi wawe strict ili kupambana na foolish age..lazima wawaone wanoko
Ila masisiter ni walezi wazuri sana...wanafundisha skills nyingi sana kwa watoto wote wa kike na kiume nje ya masomo ya darasani...nidhamu,usafi,ustarabu,adabu,mipangilio ya vitu yaani mtoto anakuja likizo unaona kabisa amebadilika.


Suala la kutozaa halifanyi sister kuwa mnoko kwa sababu Kuna wazazi pia ni wakatili vilevile kwa watoto wao.
 
1. Mimi nimesoma seminari ya Maua.
2. Kuna mambo mengi tulikuwa haturuhusiwi kufanya ambayo katika shule nyingine yalikuwa ya kawaida. Mfano, sisi hatukuruhusiwa kulala wanafunzi wawili kitanda kimoja, lakini nilikuwa nasikia kuna baadhi ya shule wanafunzi walikuwa wanaruhusiwa.
3. Sisi hatukuruhusiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na wasichana, isipokuwa tuliruhusiwa kuwa marafiki wa kawaida wa kutembeleana na hata kusaidiana masomo. Shule nyingine mtu akiwa na girlfriend au boyfriend siyo issue.
4. Sisi tulikuwa na wastani fulani wa kufaulu na kama mwanafunzi alishindwa kufikisha huo wastani (generally siyo kwa bahati mbaya) alishauriwa atafute shule nyingine na mwalimu wetu mkuu alikuwa akiwatafutia wanafunzi wa aina hiyo nafasi katika shule nyingine ambapo surprisingly walioenda kusoma huko walifaulu vizuri pia.
5. Wasichana wengi wanataka kuwa 'handled softly' hata pale ambapo ni kwa faida yao. Masista wamefundishwa kuvumilia magumu na hata ku'suspend' baadhi ya mambo kwa sababu ya masomo na kufaulu vizuri darasani. They are for the good of girl students.
6. Vision ya wasichana walio wengi ni kusoma huku una boyfriend anayekuletea vitu na hata kiwezekana anayekupeleka sehemu weekend hata kulala huko na kurudi after one or two or three days. Masista hawawezi ku'entertain' jambo kama hilo kwa sababu kwanza itakuwa scandal kwao na pia siyo njia ya kumsaidia mtoto wa kike afanikiwe katika maisha yake. Kama anataka kufanya anayotaka asubiri akienda likizo (madudu yote anayotaka afanye huko na baada ya likizo ayaache hukohuko).
7. Katika mazingira haya ambayo wasichana wanatambiana nani ana 'vitu vikali' zaidi na wenzao katika shule ambazo mambo yanajiendeaendea tu, lazima wasichana waone kama wanabwa unfairly.
8. Lakini hata shule ambazo si za masista ambazo zina masharti magumu kwa wasichana ufaulu wao huwa ni mzuri sana na hata hizo shule wasichana wanaopenda mambo 'soft soft' hawazipendi pia.
9. Kusema masista kwa vile hawazai ni wakatili ni 'bullshit' kwa sababu wazazi wanazaa ni wakatili pia na baadhi yao hata wanaua watoto wao. Ukatili siyo attribute ya sista. Ndivyo binadamu tulivyo. Na haiwezekani hata kama kuna sista katili ikawa shule nzima masista wakawa wakatili na kwa vile wazazi hutafiti kwanza shule gani nzuri inayowafaa watoto wao hawawezi kumpeleka shule ambayo wanajua masista ni wakatili na hakuna shule kama hiyo. Hii is a 'mind invention' - taja shule ambayo masista ni wakatili na wazazi wamepeleka watoto wao huko kama ipo.
10. Utafiti wako ulioufanya pengine uliufanya kwa wale ambao wana negative attitude na masista kwa sababu kuna wasichana wengine na hata watu wazima ambao walisoma shule za masista wanaona kwamba walipata msingi mzuri wa elimu na maisha na wanashukuru kwamba walipata nafasi kusoma katika hizo shule.
Naungana na wewe mimi nilisoma katika shule hizo pia. Form 1 tulianza 39 form 4 tulimaliza 19. Form six tulimaliza 7. Kama mfanya utafiti alikutana na watu kati ya ishirini walioishia njiani basi utapata negative response.
 
Uchunguzi wangu umebaini kuwa asilimia kubwa sana ya wanafunzi waliosoma shule za Masista hawawapendi Watawa hao na wala hawapendi kurudi kusoma shule hizo.

Aidha, wengi wa wanafunzi hao wanawapenda sana Ma-father (Mapadre) kuliko Masista.

Utasikia baadhi ya wanafunzi hususan wa kike wakisema "sina hamu na mtu anayeitwa Sister na wala sitamani kumuona kwa macho yangu kama siyo kukutana naye kwenye maisha yangu mazima, hata kwenye Misa nikienda sitamani kuwaona"

Mwanafunzi mmoja alimwambia mzazi wake kuwa "mimi siendi tena F5 shule ya Masista, ukilipa ada huko basi kasome mwenyewe, siyo mimi"

Humu jamvini kuna wadau waliosoma seminari na seminari ndogo za Kikatoliki tunaomba kupata maarifa kwenu yatayojibu maswali haya:
1. Mnadhani tatizo ni nini?

2. Kipi kibadike kwa Masista au hata kwenye mtaala wa kuwaandaa?

3. Je, Masista ni walezi wazuri au wabomoaji wazuri?

4. Kwanini Masista kama watumishi wa Mungu waonekane hawafai?

5. Ma-father wana kipi ambacho Masista hawana?

6. Kama Kanisa ni moja, shule moja kwanini mifumo ya malezi iwe tofauti kati ya Ma-father na Masista?

Tujadili kwa nia ya kupata maarifa yenye ufumbuzi na faida kwetu na kizazi kijacho.
Hii mbona iko wazi tu kama ya mbuzi,.Tangu lini wanawake wakapendana?
 
Back
Top Bottom