Kwanini wanaCHADEMA wamekuwa hivi?

Kwanini wanaCHADEMA wamekuwa hivi?

Anayevunja katiba anapelekwa mahakamani na sio uhuni huu mnaoufanya.Kama maoni na criticism kila siku Lissu,Mbowe,Lowassa nk...wanaeleza,wanakosoa..nk....sasa sio kila hoja lazima iwe kweli, au sio lazima Raisi achukue mawazo yao...kuna mida utasikia wakisema ''Magufuli hasikii la mtu,hachukui ushauri wetu''...asikilize kutoka watu wangapi?...tubadilike...na hii tabia ya kuchukia hadi wananchi wengine wanaochagua viongozi tofauti na chadema,maana yake nini?
Bottom line tuambie hapa "Kwa nini Rais amepiga marufuku shughuli za kisiasa nchini"?
 
Kuna ka kozi nilikasoma enzi hizo kanaitwa Neo-colonialism and revolutionary.
Haka ka kozi kana symptoms of revolution na stages zake,na revolution si lazima mapigano wala umwagaji damu HAPANA.Isipokuwa hata kufanikiwa kubadili fikra za watu dhidi ya serikali yao ni revolution.
Kwa hatua iliyopo Tanzania ni wazi people they have a DESIRE of having changes,na wanataka kitu kipya,/chama ama watawala wanaotokana na chama kingine.Hakuna kingine ni hiki tu.Yani akili zao ndo zinataka hivo,na sababu za msingi hawana ila "WANATAKA TU"
Ndo ka kanuni ka maisha kalivo.
Huoni mtaani,mtu aweza kuwa na Mke mzuri balaa lakini anakuja kamatwa anamla beki 3,au. Limwanamke la hovyo kabisa.NDO KITU DESIRE KILIVO.
 
Bottom line tuambie hapa "Kwa nini Rais amepiga marufuku shughuli za kisiasa nchini"?
Kwa hiyo Lowassa Mbeya alienda kuimba kwaya?...kikao cha chadema kilichoibuka na ukuta ilikuwa ni ukuta?...huko bunda Esta Bulaya mikutano anayofanya ni ya wachawi?...panua akili yako dogo...wanafanya siasa kasha wanadanganya wajinga, wanamkosoa Raisi halafu wanalalamika Raisi hataki kukosolewa...ndio maana nikaandika pale juu....moja ya mambo yanayowasumbua CHADEMA ni pamoja na ujinga,mazingaombwe/ushirikina..nk..nk...soma tena upate chakula cha ubongo.
 
Kuna ka kozi nilikasoma enzi hizo kanaitwa Neo-colonialism and revolutionary.
Haka ka kozi kana symptoms of revolution na stages zake,na revolution si lazima mapigano wala umwagaji damu HAPANA.Isipokuwa hata kufanikiwa kubadili fikra za watu dhidi ya serikali yao ni revolution.
Kwa hatua iliyopo Tanzania ni wazi people they have a DESIRE of having changes,na wanataka kitu kipwa/chama ama watawala wanaotokana na chama kingine.Hakuna kingine ni hiki tu.Yani akili zao ndo zinataka hivo,na sababu za msingi hawana ila "WANATAKA TU"
Ndo ka kanuni ka maisha kalivo.
Huoni mtaani,mtu aweza kuwa na Mke mzuri balaa lakini anakuja kamatwa na naamka beki 3,au. Limwanamke la hovyo kabisa.NDO KITU DESIRE KILIVO.
Kwa hivyo hapa ndipo Mbowe alipowateka na falsafa ya ''bora kuchagua jiwe''....''bora kuchagua maiti''...sidhani hata hiyo ni ''desire''...mfano wako ni wahovyo sababu ni nani amesema kuwa beki3 sio wananawake...hapa suala ni maajabu ya mtu kuacha mwanamke na kwenda kufanya mapenzi na mbwa!...fungua akili..hapa ndio ile tabia ya mazingaombwe na ujinga ambayo mmefungwa nayo...pole!
 
Umemnyonyesha mwanao sio unakimbilia kunung'unika tu humu....
Kingine usilazimishe watu wawasikitikie hao wavaa kadeti wenu.
 
Hakuna anayeshangilia. Hakuna afurahishwaye na kifo chake yeye afaye, ila ni angalizo tu kwa polisi. Uimara wao unatakiwa uonekane katika matukio ya kihalifu, na si vinginevyo. Nina hakika unaelewa ninachomaanisha.
Wacha kuficha furaha yako...mbona hata huko majuu polisi wanauwawa....nafikiri hao wahalifu unaowasifu ni waoga kwani walipaswa walitaarifu jeshi la polisi ili wapambane...kwa kushitukiza kila mtu huzidiwa nguvu hata kama una silaha nzuri vipi...hongerene kwa ujumbe mliotaka ufike..sherehe njema!
 
Umemnyonyesha mwanao sio unakimbilia kunung'unika tu humu....
Kingine usilazimishe watu wawasikitikie hao wavaa kadeti wenu.
Hongereni chadema kwa mauaji haya!...kwani mnafurahia mafanikio yenu waziwazi.
 
Kwa hiyo Lowassa Mbeya alienda kuimba kwaya?...kikao cha chadema kilichoibuka na ukuta ilikuwa ni ukuta?...huko bunda Esta Bulaya mikutano anayofanya ni ya wachawi?...panua akili yako dogo...wanafanya siasa kasha wanadanganya wajinga, wanamkosoa Raisi halafu wanalalamika Raisi hataki kukosolewa...ndio maana nikaandika pale juu....moja ya mambo yanayowasumbua CHADEMA ni pamoja na ujinga,mazingaombwe/ushirikina..nk..nk...soma tena upate chakula cha ubongo.
Sina lengo la kubishana na mtu mwenye upeo mdogo. Ukichorewa msitari huwezi hata kuangalia pembeni ya msitari. Nitakuwa napoteza wakati wangu bure. Wewe ni kama chumba kitupu au milima inayoakisi maneno ya wakubwa zako tu.
 
Hongereni chadema kwa mauaji haya!...kwani mnafurahia mafanikio yenu waziwazi.
Ungeanza kuwapongeza kwanza polisi. kwanza nina mashaka na hayo mauaji, yanaweza yasiwe ya kijambazi. intelijensia ina mbinu nyingi.
 
Anayevunja katiba anapelekwa mahakamani na sio uhuni huu mnaoufanya.

Kwa bahati mbaya, Rais akivunja kipengele cha katiba, kama ilivyo hivi sasa, hawezi kushitakiwa mahakamani. huwezi kumshitaki Rais aliye madarakani na hata akitoka madarakani. hiyo ni kwa mujibu wa katiba yetu ya sasa. kuna njia nyingi za kukabiliana na changamoto, au kutatua tatizo. kuna njia za kisheria, kuna njia za kisiasa, kuna njia za mabavu - nguvu za dola. Tatizo kubwa ni kwamba hapa Tanzania inaonekana njia za kutumia mabavu ndio zinapendwa zaidi. matatizo mengine yanahitaji "political solution" tu.

Kama maoni na criticism kila siku Lissu,Mbowe,Lowassa nk...wanaeleza,wanakosoa..nk....
Kwa mujibu wa Katiba yetu, na Sheria ya Vyama vya Siasa, Viongozi wa vyama vya siasa wanawajibika kueleza sera zao kwa wananchi, kutoa mawazo mbadala, na kukosoa mwenendo wa serikali iliyoko madarakani. Katiba inaruhusu hayo kufanyika kupitia vyombo vya habari, au kuongea na vikundi au katika mikutano ya hadhara. kwa hakika, wananchi wote wana uhuru wa kupokea na kutoa habari, kwa mujibu wa katiba. hao uliowataja wanalazimika kuongea kupitia vyombo vya habari, kwa sababu mikutano imepigwa marufuku. Rais hana mamlaka ya kupiga marufuku mikutano ya vyama vya siasa wala maandamano yao. sheria inamruhusu OCD kuzuia mkutano, na kuupangia siku nyingine. hiyo ni kwa ajili ya kulinda usalama tu. unataka tuamini kwamba Tanzania si salama mpaka 2020? Lakini Rais hana mamlaka ya kisheria. na kwa kupiga marufuku shughuli za vyama vya siasa, anavunja katiba na sheria. kumshitaki mahakamani haiwezekani. kinachowezekana ni kusisitiza kwamba ni haki ya kikatiba na kisheria kufanya mikutano ya siasa. ndio lengo la UKUTA

kuna mida utasikia wakisema ''Magufuli hasikii la mtu,hachukui ushauri wetu''.
nadhani ni kweli hasikulizi ushauri wa washauri wake. kama angefanya hivyo, asingekuwa anafanya baadhi ya mambo, au kutoa baadhi ya kauli: Polisi kuiba matairi ya magari yaliyokamatwa, ili wafanye biashara ya matairi; Polisi kupokea hongo ya elfu tano; kufyatua watoto ili wasome bure, nk. pia hatua alizochukua kwenye ishu ya sukari, wananchi wakapata usumbufu mkubwa; kukataa kuondoa VAT kwenye utalii, nk. Lakini wapinzani awaache waongee kwenye mikutano, atasikia vizuri zaidi. na aache bunge lioneshwe live, atapewa na kupata majina zaidi ya kutumbua, na sifa itakwenda kwake. tatizo liko wapi?
 
Wacha kuficha furaha yako...mbona hata huko majuu polisi wanauwawa....nafikiri hao wahalifu unaowasifu ni waoga kwani walipaswa walitaarifu jeshi la polisi ili wapambane...kwa kushitukiza kila mtu huzidiwa nguvu hata kama una silaha nzuri vipi...hongerene kwa ujumbe mliotaka ufike..sherehe njema!
Duh! Polisi wanaomba wahalifu wawataarifu kuwa wanakuja kufanya uhalifu? maajabu haya! Intelijensia inafanya nini? Au inatumika kwa shughuli maalum tu?
 
Kwa bahati mbaya, Rais akivunja kipengele cha katiba, kama ilivyo hivi sasa, hawezi kushitakiwa mahakamani. huwezi kumshitaki Rais aliye madarakani na hata akitoka madarakani. hiyo ni kwa mujibu wa katiba yetu ya sasa. kuna njia nyingi za kukabiliana na changamoto, au kutatua tatizo. kuna njia za kisheria, kuna njia za kisiasa, kuna njia za mabavu - nguvu za dola. Tatizo kubwa ni kwamba hapa Tanzania inaonekana njia za kutumia mabavu ndio zinapendwa zaidi. matatizo mengine yanahitaji "political solution" tu.


Kwa mujibu wa Katiba yetu, na Sheria ya Vyama vya Siasa, Viongozi wa vyama vya siasa wanawajibika kueleza sera zao kwa wananchi, kutoa mawazo mbadala, na kukosoa mwenendo wa serikali iliyoko madarakani. Katiba inaruhusu hayo kufanyika kupitia vyombo vya habari, au kuongea na vikundi au katika mikutano ya hadhara. kwa hakika, wananchi wote wana uhuru wa kupokea na kutoa habari, kwa mujibu wa katiba. hao uliowataja wanalazimika kuongea kupitia vyombo vya habari, kwa sababu mikutano imepigwa marufuku. Rais hana mamlaka ya kupiga marufuku mikutano ya vyama vya siasa wala maandamano yao. sheria inamruhusu OCD kuzuia mkutano, na kuupangia siku nyingine. hiyo ni kwa ajili ya kulinda usalama tu. unataka tuamini kwamba Tanzania si salama mpaka 2020? Lakini Rais hana mamlaka ya kisheria. na kwa kupiga marufuku shughuli za vyama vya siasa, anavunja katiba na sheria. kumshitaki mahakamani haiwezekani. kinachowezekana ni kusisitiza kwamba ni haki ya kikatiba na kisheria kufanya mikutano ya siasa. ndio lengo la UKUTA


nadhani ni kweli hasikulizi ushauri wa washauri wake. kama angefanya hivyo, asingekuwa anafanya baadhi ya mambo, au kutoa baadhi ya kauli: Polisi kuiba matairi ya magari yaliyokamatwa, ili wafanye biashara ya matairi; Polisi kupokea hongo ya elfu tano; kufyatua watoto ili wasome bure, nk. pia hatua alizochukua kwenye ishu ya sukari, wananchi wakapata usumbufu mkubwa; kukataa kuondoa VAT kwenye utalii, nk. Lakini wapinzani awaache waongee kwenye mikutano, atasikia vizuri zaidi. na aache bunge lioneshwe live, atapewa na kupata majina zaidi ya kutumbua, na sifa itakwenda kwake. tatizo liko wapi?
Huna hoja kwa sababu chadema wameenda mahakamani kupinga zuio la maandamano dhidi ya jeshi la polisi na wameshindwa...kwa mcha demokrasia moja ya jambo muhimu ni kutii taasisi za kidemokrasia..la sivyo unaongea maneno mengi kama unatafuna kiazi cha moto mdomoni...!
 
Sina lengo la kubishana na mtu mwenye upeo mdogo. Ukichorewa msitari huwezi hata kuangalia pembeni ya msitari. Nitakuwa napoteza wakati wangu bure. Wewe ni kama chumba kitupu au milima inayoakisi maneno ya wakubwa zako tu.

Hata mimi nimeliona hilo. Jamaa anajiita "wakudadavua" lakini hakuna lolote, ni mshirikina fulani hivi. hana hoja na hata ukimpa hoja hazijibu, anajificha kwenye udaku na kejeli rejareja. ama kweli asiyejua maana usimwambie maana!
 
45773a022e8351ec66b338542c860be7.jpg
Akili kumkichwa.
 
Zwazwa katika ubora wako.
pinga kwa hoja na sio kulia lia...Mbowe aliokolewa na maafisa usalama,Wasira alimpa mbowe sare za CCM wakampandisha gari la usalama akatoroshewa Mwanza baada ya ndugu na wananchi wa Tarime kumtuhumu kumuua marehemu Chacha Wange.Huo ndio ukweli!
 
Hata mimi nimeliona hilo. Jamaa anajiita "wakudadavua" lakini hakuna lolote, ni mshirikina fulani hivi. hana hoja na hata ukimpa hoja hazijibu, anajificha kwenye udaku na kejeli rejareja. ama kweli asiyejua maana usimwambie maana!
Naona mmeanza kubembelezana wenyewe kwa wenyewe.....jibu hoja pale juu...la nyamaza na uendelee kufurahia mauaji ya polisi kama ambavyo mmedhihirika mkifurahia.
 
Huna hoja kwa sababu chadema wameenda mahakamani kupinga zuio la maandamano dhidi ya jeshi la polisi na wameshindwa...kwa mcha demokrasia moja ya jambo muhimu ni kutii taasisi za kidemokrasia..la sivyo unaongea maneno mengi kama unatafuna kiazi cha moto mdomoni...!

Hilo la kesi usianze kucheka sasa hivi, maana bado kuna kesi zinaendelea kuunguruma, na bado zingine zitafunguliwa. kutupiliwa mbali lalamiko la kisheria haina maana kwamba halina mantiki, inawezekana tu kuna taratibu za kisheria hazikuzingatiwa. kumbuka pia kuna kukata rufaa. lakini pia kumbuka sheria mama ambayo ni katiba, inaruhusu watu kukutana na kuandamana. kwa hiyo ni suala la muda tu.
 
Hilo la kesi usianze kucheka sasa hivi, maana bado kuna kesi zinaendelea kuunguruma, na bado zingine zitafunguliwa. kutupiliwa mbali lalamiko la kisheria haina maana kwamba halina mantiki, inawezekana tu kuna taratibu za kisheria hazikuzingatiwa. kumbuka pia kuna kukata rufaa. lakini pia kumbuka sheria mama ambayo ni katiba, inaruhusu watu kukutana na kuandamana. kwa hiyo ni suala la muda tu.
Mimi sijacheka...kama kuna kesi zinaendelea uhuni wa kusema maandamano unatokea wapi?...au mnatumia ujinga wa wanachadema ili wajue Mbowe/Lissu/Lowassa wananyanyaswa pale watakapovunja sharia?.....Katika inatoa haki na wajibu...na maandamano lazima yalindwe na polisi...sasa ni jukumu la polisi kuwa na hakika kuwa waandamanaji watakuwa salama.....Hivi mbona kipindi Mbowe na Zitto hawaelewani....Mbowe aliomba jeshio la polisi kuwadhibiti wafuasi wa chadema amabo walikuwa bega kwa bega na Zitto...kama demokrasia ni kuacha kila mtu afanye atakalo?..Mbona juzi Maalim Seif na Mtatiro wameondoshwa ukumbini na polisi...!...tusipende kutetea kila upuuzi.Nawapongeza kwa uamizi wa kwenda mahakamani...na sio kufanya mambo yote kwa wakati mmoja.
 
Back
Top Bottom