Kwanini wana CCM wanamuogopa Lowassa?

Kwanini wana CCM wanamuogopa Lowassa?

It's true wanaomwogopa Lowassa ni watu wa CCM hasa viongozi wa juu kabisa kwa sababu wanajua walichomfanyia alivyojiuzulu. Alijitoa mhanga alijua atalindwa na washiriki wenzake aliowaacha nyuma.

Lakini kwa bahati mbaya alivyoondoka na wenzake ndiyo wakamtupia tope lote ili kujiokoa wao. Wanajua akirudi atawafanyia nini. Kwetu sisi ambao siyo CCM hii ni theatre moja yenye action kali sana. Vuta kiti.
 
Lowasa anaogopwa sana na wenye dhambi,lowasa ni mtakatifu na muadilifu,Lowassa ameandaliwa na Mungu kutukomboa watanzania
 
N

Kasi ya Lowassa kufuatilia malengo yaliyokubaliwa ndo inawasumbua,wanajua mziki wa Comrade akitangaza ziara sehemu yako ya kazi hupati usingizi hadi ukamilishe malengo hizo ndo figisufigisu za kumkataa Che wa tz Lowassa.wazalendo tumewajua hao na huu2015 mwisho wao!!Hastle Vista Siempre LOWASSA.
Kazi sana kubeba gunia la upu-pupu!
 
Kuna usemi kuwa, kwa jinsi binadamu anavyozidi kutenda dhambi, shetani naye kaanza kumhofia binadamu.Sasa,CCM ni mafisadi ila wanadai Edo kapitiliza.Anaweza uza hata nchi.Alafu Edo hayupo smart kichwani na ni mwingi wa jaziba, anaweza hata pinduliwa.
 
CCM wanamuogopa Lowassa kwa sababu yeye siyo kiongozi wa ndimi mbili!. Alisema jambo analiamini na kulisimamia mpaka mwisho.

Hata hivyo', walimuundia zengwe kumfyeka kisiasa lakini walishindwa, waliogopa kazi wakajiunga kundi, wakafanikiwa kumundoa nchi, hawakuweza tena kuzungumza MKUKUTA, Dira ya Maendeleo2025.

Hata alipoibukia Lowassa ni Mungu na mapenzi ya Watanzania kwake na siyo CCM. Baadhi ya viongozi ndani ya Chama chake wametumia nguvu nyingi Sana kumshughulikia huyu bwana lakini wameumia. Wengine Kama kina Mkama wao badala yake Kama wasisi kauli ambazo hazijakuwa na tija ndani ya Chama wakawa majeruhi Wa kwanza.

Tunapofanya jambo kwa hila lazima tuharibikiwe. Baada ya Watanzania kufuatilia sarakasi za Lowassa na Chama chake, wakagundua ukweli na sasa huruma zao zote ziko kwa huyu bwana.

Hata cha takriban miezi mitatu iliyopita ilipowatuma vijana karibu 30 kwenda mikoa yote kufanya utafiti, juu ya kiongozi gani anayekubalika na wananchi, matokeo yalibainisha ni Lowassa akifuatiwa kwa mbali na Dr. Magufuli.

Huu ndiyo ukweli CCM wanalifahamu na mbingu zinajuwa ukweli huu. Bora tu Watanzania wapewe chaguo Lao tutakuwa tumeepuka mtego tuliojiwekea wenyewe kwa maslahi ya wachache!
 
Sio kwamba wanamuogopa LOWASA bali miongoni mwao hakuna msafi kiasi cha kumnyooshea mwenzie kidole...kwa kuwa wote ni watu wa dili...
 
Ntachangia ukirekebisha Kichwa Cha habari sema ukoo wa Mtu flani sio wana CCM, huoni Mtiti wa wana CCM na Watanzania kote nchini wanavyo mkubali..!? Ni ukoo wa Mtu mmoja Na marafiki zake tu..!
 
Kiiza wacha kutwambia ujinga wako, mla rushwa awezi kupambana na rushwa. Stop it
 
Hawamwogopi hata chembe, nina uhakika wana ogopa wakimchagua kuwa mgombea Urais wao kuwakilisha chama chao basi ndio itakuwa mwisho wa CCM, Lowassa ni mchafu sana, upinzani watakuwa na kazi rahisi tu ya kuuelezea ufisadi wake, CCM oyeeeeeeeee
 
Wanao mpiga vijembe Lowassa ni waoga wanajua jinsi wanavyompakazia so akiwa rais wanadhan atalipa kisasi kumbe si kweli... Lowassa ni muungwana Sana
 
Ngoja wiki ijayo kila mmoja wao atataka jiunga na timu Lowasa
 
aisee ccm hawajiamini mpaka kukaribisha na kutoa form za urais mpaka kwa wakulima.ccm wameleta watu weng ilimrad kura zgawanyike ovyoovyo.
 
Back
Top Bottom