Kwanini wana CCM wanamuogopa Lowassa?

Kwanini wana CCM wanamuogopa Lowassa?

KakaKiiza

Platinum Member
Joined
Feb 16, 2010
Posts
11,943
Reaction score
9,457
WanaJamvi, nina swali hapa Nimekuwa nikifuatilia watia nia hakuna aliyetangaza nia bila kumiga kijembe Lowassa!Ajabu na kweli nikuwa kuna watu ndani ya CCM wanamuogopa Lowassa endapo atachukua hii nchi na kuwa Rais!

Kuna vitu tujiulize kwanini wanamuogopa!

(a)Atakwiba mali za nchi hii??
(b)Atawawajibisha wala rushwa na kuwatia adabu wavivu ndani ya serikali?
(c)Kwakuwa anapendwa na watu wanajua hawawezi kupambana naye ndo maana wanaanza fitna mapema?
Au basi ni siasa za maji taka?

Naomba maelezo yenu!
 
Wakina mama wa kitanzania kama kaweida yao ya kushangilia hata kama hawajaelewa mfano leo kwa pinda.ht pale alipoulizwa swali gum la kutoka kwa nyanje.
 
hawampend ila ni wasala.tonge ebu siku moja aseme ameishiwa hatoi hela muone watakavyo mkimbia wote.
 
Ccm wako makini hawawezi kukubali nchi iharibiwe na wachache afu ionekane chama ndo kimevurunda. Kila mtu atabeba mzigowake mwenyewe
 
(b) is the correct answer.

Wanaogopa uadilifu wake utawaumbua....
 
lohasa akiteuliwa na ccm. ujue tanzania ufisadi utakuwa umeshinda rasmi.....
 
Ccm wako makini hawawezi kukubali nchi iharibiwe na wachache afu ionekane chama ndo kimevurunda. Kila mtu atabeba mzigowake mwenyewe

ccm sio ile uijuayo wewe.Hii imetekwa na vibaka by makongoro.Lowasa ni kibaka kubwa lao ndio linatuangaisha watanganyika wote
 
Hawamwogopi Lowassa ila ccm wanaogopa genge lake, genge lililonyuma yake ni hatari sana, Chenge, Rostam Aziz, Karamagi, Tibaijuka na Ngereja ogopa sana watu hao
 
KakaKiiza

Wanaccm hawataki mafisadi yeye ni fisadi kwahiyo hafai kabisa kuwa miongoni mwa wanaccm wasafi na wachukia Rushwa.
 
Last edited by a moderator:
Lowasa ni jipu, ukitumbua vibaya utachafuka wewe, linahitaji timing sana.
Huwezi kumtenganisha fisadi lowasa na rushwa.
 
Kwa sababu wamezoea kufanya kazi kwa mazoea hawataki kiongozi mfuatiliaji wa mambo kifupi wanapenda business as usual.....
 
Lowasa ni jipu, ukitumbua vibaya utachafuka wewe, linahitaji timing sana.
Huwezi kumtenganisha fisadi lowasa na rushwa.
Kwa lipi wewe unalolijua kuhusu rushwa

Wanaccm hawataki mafisadi yeye ni fisadi kwahiyo hafai kabisa kuwa miongoni mwa wanaccm wasafi na wachukia Rushwa.
Tupe facts kuhusu rushwa yake

lohasa akiteuliwa na ccm. ujue tanzania ufisadi utakuwa umeshinda rasmi.....
Kwa maana ipi mkuu maana ujaonyesha njia

Kwa sababu wamezoea kufanya kazi kwa mazoea hawataki kiongozi mfuatiliaji wa mambo kifupi wanapenda business as usual.....
Kwa hiyo siyo Ufisadi??
 
Si Lowasa peke yake anayesemwa. Wapo wengine pia wanasemwa katika fora mbalimbali. Na Hakuna anayemwogopa Lowasa. Huyu wanamchukia na kumwona kama donda ndugu liliovunda lakini kwa sababu za kuoneana haya hakuna anayeweza kupendekeza afukuzwe chamani kwa kukidhalilisha Chama.
 
Wanaogopa kuliangamiza Taifa kumpa mtu Mwizi ambaye atawaibia hadi walichoficha uvunguni mwao
 
KakaKiiza


Kasi ya Lowassa kufuatilia malengo yaliyokubaliwa ndo inawasumbua,wanajua mziki wa Comrade akitangaza ziara sehemu yako ya kazi hupati usingizi hadi ukamilishe malengo hizo ndo figisufigisu za kumkataa Che wa tz Lowassa.wazalendo tumewajua hao na huu2015 mwisho wao!!Hastle Vista Siempre LOWASSA.
 
Last edited by a moderator:
Kwa lipi wewe unalolijua kuhusu rushwa

Tupe facts kuhusu rushwa yake

Kwa maana ipi mkuu maana ujaonyesha njia

Kwa hiyo siyo Ufisadi??

Jambazi sugu na fisadi papa lowasa kamwe hawezi kuwa rais wa taifa hili. Uwezo wake ni kuongoza ng'ombe sio watu!!!
 
UKAWA ndiyo wanamuogopa Lowassa, huo ndiyo ukweli.
 
Back
Top Bottom