Kwanini waarabu weupe wanawabagua waarabu weusi?

Status
Not open for further replies.

Saint Ivuga

JF-Expert Member
Aug 21, 2008
54,363
58,386
Waarabu weusi wanabaguliwa sana na waarabu weupe achilia mbali wewe muafrika, wewe muafrika ni issue nyingine kabisa, nchi za kiarabu sijui kwa nini zina ubaguzi sana kwa watu weusi .
Ukienda europe utabaguliwa sana lakini ubaguzi wake sio kama wa waarabu.
The safe place for african ni Afrika.
Tulilinde bara letu..... Kila sehemu muafrika anabaguliwa akienda except Africa tu
 
Mkuu huu ubaguzi siyo wa rangi tu, kuna baadhi ya makabila ndani ya Tanzania yanabaguwana.Mfano ukienda kwenye jamii ya wakurya,utakuta na wao wamegawanyika kuna wakira,watimbaru,wanyabhasi nk.Nilichoshangaa pamoja na uafrika wao lakini utakuta mkira anambagua mnyabhasi licha ya kuwa wote ni watanzania na wote ni weusi.Suala la ubaguzi naona lina mzizi wa "huyu hatutoki sehemu moja"
 
Hata sisi watanzania tunao huo ubaguzi jiulize kwanini serikali na mashirika mengi yanakemea juu ya kuwanyanyapaa albino,wagonjwa wa ukimwi,tena kuna baadhi ya makabila hayaruhusu hata kuoleana na kabila jingine,wazo langu tujiangalie kwanza sisi kisha tuwaangalie hao waarabu, mada hii ukiisoma na kui pigia picha ya jinsi itakavyoishia inaonyesha huko mbele italeta u-dini ,furugu ambazo zilikuwepo jana huko dar,na mwisho inaweza kuwa kwakuwa waarabu wanachukiana wao kwa wao sembuse hawa waislam ambao wapo tanzania ambao ndo weusi na nywele ngumu zaidi ya hao warabu wanaoishi nao huko,
 
Waarabu wanabaguana hata kwa koo na kipato. Ni viumbe dhaifu kuliko wote linapokuja suala la ubaguzi. Inapokuwa kwa waswahili watokao Afariq kama wao wanavyopenda kuita ndiyo usiseme. Hata hivyo waswahili wakati mwingine ni wa kujilaumu. Je una habari kuwa wamakonde wa Sudan kwa mfano wanajiita waarabu na kubagua wenzao wa kusinin? Uzuri ni kwamba wakivuka mpaka kwenda Misri au Saudia huitwa Khaali au ibn muthnak. wanaharamu au watumwa. Wamisri hutumia abdi yaani mtumwa. Ni tatizo letu wenyewe. Hata ukienda nchi kama nyingi za kiarabu ukajitambulisha kwa majina ya kiarabu wanashagaa kama kwenu hakuna majina. Si hilo tu, hata ukienda misikitini wengi wanakuchukulia kama mwizi wa viatu. Yaliwahi kumtokea rafiki yangu toka Darfur aitwaye Ali akiwa nchini Misri alikwenda kusali na kutimliwa kwa madai kuwa mswahili alikuwa akitafuta nini kama siyo kuiba viatu.
 
waaarabu wabaguzi sana huko nchini mwao mashariki ya kati. wewe ona tuu mgogoro wa somalia Syria. Utaona arab legue wametikisana na UNO kuhusu syria lakini kwa somali, wao wanwaangalia kama vile vilikuwa vita vya ngombe. Halafu kule libya na uarabuni kote kuna Black arabs, huwaoni hata siku moja bungeni wala katika baraza la mawaziri nchini mwao. wewe utawaona tuu katika timu za soka lakini siasan hawatambuliki. Halafu somalia na sudan bado eti zinajiita members wa Arab League!!!!!!!!!!!!!!
 
Waarabu weusi wanabaguliwa sana na waarabu weupe achilia mbali wewe muafrika, wewe muafrika ni issue nyingine kabisa, nchi za kiarabu sijui kwa nini zina ubaguzi sana kwa watu weusi .
Ukienda europe utabaguliwa sana lakini ubaguzi wake sio kama wa waarabu.
The safe place for african ni Afrika.
Tulilinde bara letu..... Kila sehemu muafrika anabaguliwa akienda except Africa tu

Bro, at least get your shi.t right first.

Kwani Waingereza Weupe hawawabagui Waingereza Weusi?

Au Wamarekani Weupe hawawabagaui Wamarekani Weusi?

Hata Waswidi Weupe na Wafaransa Weupe wanawabagua wale kati yao walio weusi.

Kwa hiyo what's the big deal about Waarabu Weupe kuwabagua Waarabu Weusi?
 
Hata kama mtajaribu kupindisha thread ukweli uko wazi tu. Ubaguzi katika nchi za kiarabu unatisha mno. Kule hata mfumo wa sheria unawabagua weusi tofauti na ulaya na marekani. Mtoa mada amesema kweli tupu kwamba sehemu salama kwetu sisi wamakonde ni Afrika. Hayo mengine ya ukimwi n.k. si ubaguzi, ni unyanyapaa.
 
waaarabu wabaguzi sana huko nchini mwao mashariki ya kati. wewe ona tuu mgogoro wa somalia Syria. Utaona arab legue wametikisana na UNO kuhusu syria lakini kwa somali, wao wanwaangalia kama vile vilikuwa vita vya ngombe. Halafu kule libya na uarabuni kote kuna Black arabs, huwaoni hata siku moja bungeni wala katika baraza la mawaziri nchini mwao. wewe utawaona tuu katika timu za soka lakini siasan hawatambuliki. Halafu somalia na sudan bado eti zinajiita members wa Arab League!!!!!!!!!!!!!!

Acha uongo.....Somalia sio member wa Arab League

Google uone kama unabisha
 
Kwanza hakuna waarabu weusi
Waarabu wote weuope ama wekundu
WAle weusi ni waafrika wanao ongea kiarabu
Pili tukubali afrika ndio watu wake wapo nyuma katika kila nyanja ikiwemo ustaraabu ndo maana mpaka leo kwetu kuna mijizi mijambazi wabakaji nk
Tuko nuuma kielimu hata nchi tajiri kama tanzania lakin nchi inabaki maskin
Katika jamii zote afrika pekee ndo iliitwa dark continent la washenzi hivyo wazungu wakagawana kuja kustaarabisha lakini miaka mia 300 baadae hali ni ile ile
Hivyo usilaumu waraabu ni jamii yenyewe ya kiafrika weusi. In general hawaaminiki ndo. Tunadharauliwa ndo maana tunabaguliwa. Na kudharauliwa sio arabunu tu bali ulaya amerika na asia huu ndo ukweli tubadili tabia
Kule Oman kuna mjii unaitwa Salalah huu 60% ya wakaaz wake ni weusi lakini wanaheshimiwa na hawa ndio mabosi pale lakini wao hawana tabia hizi za kwetu wamestaaranika
Ama wapo wamarekani wafrica weusi huko marekani wana shughuli zao lakin ubaguzi upo sana maneo kama. Kule ilipotokea Katrina ni eneo la weusi maskini waliotupwa dhalili kuiliko afrika
Lakini ubaguzi ni hulka ya ya wazungu ndani damu hivyo upo mpaka leo
Ama ulaya waafrika wengi ni wabeba maboksi hawana nafasi muhimu akiwemo ni kwenye boxing ama mpira na ulaya ubaguzi sio kwa wafrika tu bali hata wao kwa wao kama unatoka eastern europe pia wanakudharau
Kwa hio ubaguzi wa rangi upo kila mahali na sana dhidi ya wafrika na inachangiwa zaidi na tabia zetu
Mungu aliumba adam na hawa sijui walikua rangi gani na sijui ilikuwaje baadae kukawa na wachina wajapan weusi wazungu wahindi.
Waraabu nk
Hii. Biology ya kubadilika kutoka watu wawili kabila moja labda mpaka watoto wakawa makabila tofauti niimejaribu kusoma Quraan na Biblia kujua imekuwaje tuwe makabila tofauti ilhali asili yetu watu wawili ??pia utaona kuna lugha zaidi ya 10000 duniani
Ingawa katika Quraan Mungu anatwanbia ametumba makabila tofauti ili tupate kujuana hayo mengine kutaka mjadal mpana kuhusu makabila


Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Waarabu wanabaguana hata kwa koo na kipato. Ni viumbe dhaifu kuliko wote linapokuja suala la ubaguzi. Inapokuwa kwa waswahili watokao Afariq kama wao wanavyopenda kuita ndiyo usiseme. Hata hivyo waswahili wakati mwingine ni wa kujilaumu. Je una habari kuwa wamakonde wa Sudan kwa mfano wanajiita waarabu na kubagua wenzao wa kusinin? Uzuri ni kwamba wakivuka mpaka kwenda Misri au Saudia huitwa Khaali au ibn muthnak. wanaharamu au watumwa. Wamisri hutumia abdi yaani mtumwa. Ni tatizo letu wenyewe. Hata ukienda nchi kama nyingi za kiarabu ukajitambulisha kwa majina ya kiarabu wanashagaa kama kwenu hakuna majina. Si hilo tu, hata ukienda misikitini wengi wanakuchukulia kama mwizi wa viatu. Yaliwahi kumtokea rafiki yangu toka Darfur aitwaye Ali akiwa nchini Misri alikwenda kusali na kutimliwa kwa madai kuwa mswahili alikuwa akitafuta nini kama siyo kuiba viatu.

Nakulewa mkuu, jamaa wana roho mbaya sana wakiwa kwao huwezi kuamini hadi uishi nao. The best place for african to live is africa. Tuilinde africa yetu
 
Saint Ivuga nimekuelewa. Tatizo ni kwamba waswahili wakiona hawa waarabu koko ambao nao wanatubagua wanadhani ni waarabu wote. hebu nenda Tabora Tanga Lindi Mtwara hata Zenj mabaki ya waarabu yanaozeshana yenyewe kwa yenyewe huku yakijishindia mabinti zetu wazuri. Hawa ni waja laana si uongo.
 
Waarabu weusi wanabaguliwa sana na waarabu weupe achilia mbali wewe muafrika, wewe muafrika ni issue nyingine kabisa, nchi za kiarabu sijui kwa nini zina ubaguzi sana kwa watu weusi .
Ukienda europe utabaguliwa sana lakini ubaguzi wake sio kama wa waarabu.
The safe place for african ni Afrika.
Tulilinde bara letu..... Kila sehemu muafrika anabaguliwa akienda except Africa tu


Saint Ivunga umeongea point, ila nakuomba kama una ink kwenye printer yako tafadhali toa kopi hata milioni uwapelekee waislam wote misikitini hapa Tanzania ili wajue hali halisi. Yaani waislam bwana utakuta mtu mweusi kama mkaa ila anajiita mwarabu au la atajifananisha tu na mwarabu kujifanya hajuwi kiswahili kizuri kila neno alitamkalo lina lafudhi ya kiarabu. We ahiia mbali tu huko Uarabuni, Sudan tu hapo waafrika wanadgarauliwa na waarabu wa huko Sudan.
 
Waarabu weusi wanabaguliwa sana na waarabu weupe achilia mbali wewe muafrika, wewe muafrika ni issue nyingine kabisa, nchi za kiarabu sijui kwa nini zina ubaguzi sana kwa watu weusi .
Ukienda europe utabaguliwa sana lakini ubaguzi wake sio kama wa waarabu.
The safe place for african ni Afrika.
Tulilinde bara letu..... Kila sehemu muafrika anabaguliwa akienda except Africa tu
Hao waarabu achana nao.Ubaguzi wao huwa si mkubwa sana kwani mara nyingi huwa unatokea kwa wale waarabu ambao si waislamu wenye elimu.Ukiangalia unaweza ukaona kinyume chake kwa wale waarabu walioanza kufika mwambao wa Afrika Mashariki.Unaweza ukasema kwanini waarabu wanawapenda sana waafrika.Wengi wao waliwach wake zao arabuni na kuwaowa wanawake wa kimanyema na kinyamwezi.Wale waliokuja na wake zao basi walipenda waongeze wake wengine wa kiafrika mpaka wanne.
Wasichana wa kiarabu nao wengine walikosana na wazazi wao kwa kulazimisha kuolewa na wanaume wa kiafrika waliowapenda.Hata hayati Karume alipendwa na mwarabu na yeye akapenda zaidi kwa kujiolea wengine bila ridhaa ya wazazi wao.
Ubaguzi ambao una athari na ambao hata mimi siupendi ni ule wa muafrika mkristo kumbagua muafrika mwenzake kisa ni muislamu tu.Akitaka ajira ananyimwa na elimu hapewi nafasi ya kupanda juu kulingana na kipaji chake.Unaweza ukakuta mwanasiasa muislamu ana sifa zote za kugombea na kuwa raisi lakini waafrika wenzake wakristo wakamfanyia kampeni chafu mpaka waislamu wenzake wakamtilia shaka.
Saint huenda umenielewa au kama una swali...
 
Saint Ivunga umeongea point, ila nakuomba kama una ink kwenye printer yako tafadhali toa kopi hata milioni uwapelekee waislam wote misikitini hapa Tanzania ili wajue hali halisi. Yaani waislam bwana utakuta mtu mweusi kama mkaa ila anajiita mwarabu au la atajifananisha tu na mwarabu kujifanya hajuwi kiswahili kizuri kila neno alitamkalo lina lafudhi ya kiarabu. We ahiia mbali tu huko Uarabuni, Sudan tu hapo waafrika wanadgarauliwa na waarabu wa huko Sudan.

Hebu jaribu pia kutembelea na israel ujue ubaguzi umefikia kiwango gani pale,halafu pima ubaguzi wa warabu na wazungu upi zaidi?
 
Nakulewa mkuu, jamaa wana roho mbaya sana wakiwa kwao huwezi kuamini hadi uishi nao. The best place for african to live is africa. Tuilinde africa yetu
Nenda zako kakojoe ukalale.Huna hoja Saint.Kumbe masaint ndivyo mlivyo.Waongo na hamfikiri kabla kusema.
Umeambiwa Salala nchini Oman utadhani uko Mtwara na wao ndio mabosi wa kila kitu kule.Hata mfalme wao anatoka huko.Sasa tena unaanza kurusha mawe eti Ooh! jamaa wana roho mbaya.
 
Ubaguzi umeenea kila kona ya dunia,ubaguzi wa ndani ya chadema hamuoni? Ubaguzi wa nafasi za ubunge ndani ya vyama vya siasa hamuoni kuwa watu wanapeana kwa kujuana?au huo sio ubaguzi? Ubaguzi ndani ya ccm chama chote wamejaa vigogo na family zao au huo sio ubaguzi?

Oman wana sheria kali sana kuhusu ubaguzi na adhabu ya chini kabisa ni kifungo cha miezi 6,oman hata mfanyakazi wa ndani ukimfokea au kumtukana bado wao wana sheria kali sana utamlipa au utafungwa,oman pia wana sheria za kulinda wafanyakazi wote wanaotoka nje ya nchi yao kutokana na ubaguzi wa aina yeyote,
Sasa hapo kwetu tz tumechukua hatua gani juu ya ubaguzi au ndio tunauendeleza?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom