Odhiambo cairo
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 15,989
- 22,057
Ulichojivunia ni viongozi na vyombo vya dola na vya maamuzi au kazi nzuri ya Jpm ?!. Kama ni vyombo vya dola hata kina Amin walivitumia !!. Lakini kama ni hiyo inayoitwa kazi nzuri. Aachie wananchi waamueKwa usawa huu ni ndoto sana upinzani kushinda serikali za mitaa na hata tu uchaguzi wa udiwani , ubunge , Urais ! Ni kama tu hawatashinda tena. Washukuru awamu zilizopita za kudekezana mpaka watu wanaitwa Ikulu kunywa juice baridiii...
Ni DED / DC /DAS / R C /RAS / RPC gani ndani ya nchi hii atakubali kuwa na chembe ya mpinzani eneo lake ? Ni nani atakubali mpinzani atangazwe na aapishwe ?
Ni ngumu sana mpinzani kushinda kwa Tanzania hii ya JPM kwa haya makubwa anayofanya :-
1. Reli ya SGR
2.Elimu bure
3. Mradi wa Stigler's George
4. Ununuzi wa ndege ATC
5. Uwajibikaji na adabu kwa watumishi wa umma
6. Mahakama ya mafisadi
7. Miradi ya umeme , maji , barabara , mazingira
8. Serikali kuhamia Dodoma
9. Ufufuaji wa viwanda nchini
10. Kupunguza safari za nje zisizo na tija
11. Kuzuia siasa ili watu wafanye kazi kwa nguvu
12. Viwanja vya ndege
13. Kufufua shirika la reli TRC
Kama unataka maendeleo unataka nini zaidi ?
Wapinzani watatoboaje kwenye game hili ?
Kwanini wasitumie mtaji walioupata ili kufanya kazi zingine ?
Kuna ulazima sana wao kuendelea kufanya siasa ?
Watafute miradi ya kufanya.
JPM atosha.