Kwanini ung'atwe ovyo!!

Kwanini ung'atwe ovyo!!

Mmh hii yako mwenzangu inaitwa za mwenzio changanya na zako ila nikwambie sio kila kung'atwa ni lazima uchape lapa kung'atwa kwingine sababu ni kutokutaka kuzungumza na yule mng'ataji au sisi wanawake kushindwa kutambua sababu za huko kung'atwa hivo kusababisha kuwa jambo endelevu.

Hivyo naona kabla ya yote hayo kufanyika kama kubaki au kuondoka mazungumzo muhimu sababu tukisema kila tuking'atwa tunasepa huo ndio utakuwa mwanzo wa kujichakaza.
Fact
 
Habarini wadau wa jf natumai mko fiti mnapambana na hali zenu za kusaka tonge la maisha leo nimewakumbuka sana na kuonelea kuwa letea mada isemayo: Kwanini ung'atwe ovyo

Ilihali una miguu ya kusepa chanja mbuga achana nae kwani ni huyo tu uliyeandikiwa nae kufa na kuzikana shosti usikalie kuti kavu ilihali una mwelekeo wa kusepa achana nae songa kivyako maisha popote mtu anakusumbua wewe bado eti kisa mapenzi kwani ulizaliwa nae.

Achana nae Mungu atakupa mwingine wa kufanana nae wanaume wa sikuhizi hawaeleweki kabisa shosti wewe ukiona anakuletea zogo wewe ondoka utapata mwingine ambaye atakulea na ku handle maisha ni furaha sio karaha jifunze kuondoka kwani yeye ataona baadaye umuhimu wako

Najua mmeshapata somo hapa nawatakia kila kheri

kwaherini
209573.jpg
 
Mleta Mada kama huna Bahati ya kupendwa na wanaume
Waache wenzio wavinjari
Siku zoote mnaambiwa msiombe Uzuri ombeni bahati
 
Huo ni uoga wa kukimbia changamoto.

Ni sawa na mangi afunge duka kisa kapata loss
 
Ukiona hyo ujue hujampenda, mapenzi ni uvumilivu na kuchukuliana mapungufu, ukikosewa ongea mrekebishe na sio kukimbia.

Ukijua kwamba binaadam hatujakamilika basi utakuwa mvumilivu kwa mwenzio na utakuwa unajitahidi kujenga zaidi ya kubomoa. Mtoa uzi kwa hili umekurupuka aisee
 
Ukisoma hiipost between lines mtoa mada ametoka kuvurugwa hata hajafanya tathmini amekuja hapa bado kajaa upepo.

Maamumuzi mazuri huwezipata mtandaoni kaa chini waza kwa nini mnapitia hayo mnayoyapitia jiulize chanzo ni nini?

Lakini pia mnatakiwa kujua wanaume na wanawake wote ni binadamu, na kwa asili yao kukengeuka na kukosea ni jadi yao.... Hata adamu na hawa walimkosea Mungu pamoja na ukaribu wote waliokua nao kwa Mungu.

Utasepa kwa mr X ukienda kwa Y ndio mbaya Aidi utaondoma utaenda kwa Z utagundua bora yule wa kwanza ukitaka kurudi nafasi imejaa.


Pia kumbukeni kinadada mpo wengi kwa sasahivi wanaume hawapati shida kama zamani maneno mawili tayari. Hivyo hii inafanya wanaume wasione hatari au kuondoka kwa mmoja haina shida maana mwingine atachukua nafasi faster.


Ndoa au mahusiano ya m/mume na m/mke yanahitaji kuvumiliana kujitoa na kusahihishana. Kuachana iwe tu pale inapobidi, sio kwa kujAna upepo
 
Ndo mnavyo danganyanaga sio?

Sikatai kuna wanaume hawafai hasa manake kutwa utalia.

Lakini kuna wanaume ambao wanarekebishika, na kubadilika kabisa and they turn out to be awesome husbands and Dads.

I wish ungewapa limits wenzio na kuwapa moyo wawe wavumilivu kwa sababu hamna mwanamme aliekamilika na sisi pia hatujakamilika.

Tufundishane, tuelekezane na tuvumiliane. Sio kosa dogo tu unasepa na hapo ushatumika. Ndo utasikia mwingine anaibuka na kusema oooh sitaki mwanaume bora mwanamke mwenzangu, mara oooh naweka dildo yangu chumbani.

Wanaanzaga hivi hivi.
Halafu we bibie nakutafuta ujue
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom