Kwanini UKAWA wasishitakiwe?

Kwanini UKAWA wasishitakiwe?

Barbarosa

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2015
Posts
22,584
Reaction score
27,837
Kila mara nimekuwa nikimsikia Lowassa, Mbowe, Mbatia &Co. wakisema kwamba wameibiwa kura kwenye uchaguzi uliopita lakini bila kutoa ushahidi wowote ule, sasa nauliza ni kwa nini wasishitakiwe kwa uzushi ambao wanajaribu kuwaaminisha baadhi ya watu mambo ya Uongo?

Hivi sasa kuna baadhi ya wananchi wamepoteza Imani na Serikali na vyombo vyake kwa sababu ya tuhuma za ukawa kwamba serikali yetu iliiba kura wakati mpaka leo hii ukawa hawajaonyesha ushahidi wowote ule. Sasa hamna sheria ya kuwashitaki?
 
Peleka wewe hili suala mahakamani. Maana limekuathiri
 
Kila mara nimekuwa nikimsikia Lowassa, Mbowe, Mbatia &Co. wakisema kwamba wameibiwa kura kwenye uchaguzi uliopita lakini bila kutoa ushahidi wowote ule, sasa nauliza ni kwa nini wasishitakiwe kwa uzushi ambao wanajaribu kuwaaminisha baadhi ya watu mambo ya Uongo?

Hivi sasa kuna baadhi ya wananchi wamepoteza Imani na Serikali na vyombo vyake kwa sababu ya tuhuma za ukawa kwamba serikali yetu iliiba kura wakati mpaka leo hii ukawa hawajaonyesha ushahidi wowote ule. Sasa hamna sheria ya kuwashitaki?
Anza wewe tuone
 
Sidhani kama kuna mtu mwenye akili timamu anaamini UKAWA kuwa wameibiwa kura. Hivyo serikali imeamua kukaa kimya ikiwa ni jibu bora kabisa kwa mtu mpumbavu. Mtu mpumbavu dawa yake sio kumjibu....ni kukaa kimya tu.
 
Kama JPM angekuwa anajiamini hivyo si angemruhusu Lowasa ataapike nyongo yake hadharani pale Jangwani?? Mbona mnamzuia? Huo ushahidi auweke wapi kama sio hadharani tuujue tujinyamazie?? Nenda sasa weye mahakamani
 
Sidhani kama kuna mtu mwenye akili timamu anaamini UKAWA kuwa wameibiwa kura. Hivyo serikali imeamua kukaa kimya ikiwa ni jibu bora kabisa kwa mtu mpumbavu. Mtu mpumbavu dawa yake sio kumjibu....ni kukaa kimya tu.

Well said!!
 
Kila mara nimekuwa nikimsikia Lowassa, Mbowe, Mbatia &Co. wakisema kwamba wameibiwa kura kwenye uchaguzi uliopita lakini bila kutoa ushahidi wowote ule, sasa nauliza ni kwa nini wasishitakiwe kwa uzushi ambao wanajaribu kuwaaminisha baadhi ya watu mambo ya Uongo?

Hivi sasa kuna baadhi ya wananchi wamepoteza Imani na Serikali na vyombo vyake kwa sababu ya tuhuma za ukawa kwamba serikali yetu iliiba kura wakati mpaka leo hii ukawa hawajaonyesha ushahidi wowote ule. Sasa hamna sheria ya kuwashitaki?

Katika nchi za kiafrika hii imezoeleka, kuwa ni mbinu ya kisiasa kushinikiza ushindi, ikibidi kumjenga hofu mshindi halali ili kutoa nafasi ya kuingia madarakani kwa upenyo wa maridhiano. Ndiyo maana utasikia lugha kama 'ushahidi tunao ila tutautoa muda muafaka ukifika'
 
Kila mara nimekuwa nikimsikia Lowassa, Mbowe, Mbatia &Co. wakisema kwamba wameibiwa kura kwenye uchaguzi uliopita lakini bila kutoa ushahidi wowote ule, sasa nauliza ni kwa nini wasishitakiwe kwa uzushi ambao wanajaribu kuwaaminisha baadhi ya watu mambo ya Uongo?

Hivi sasa kuna baadhi ya wananchi wamepoteza Imani na Serikali na vyombo vyake kwa sababu ya tuhuma za ukawa kwamba serikali yetu iliiba kura wakati mpaka leo hii ukawa hawajaonyesha ushahidi wowote ule. Sasa hamna sheria ya kuwashitaki?
Ushahidi unatolewa wapi?
Polisi au mahakamani?

Nimesikia kuna wagombea wamefungua kesi za uchaguzi, je hawatakuwa na vielelezo na ushahidi wa kuuwasilisha huko mahakamani?

Lakini CCM wanahitaji ushahidi?

Maalim Seif ana ushahidi na vielelezo vyote kuwa ameshinda uchaguzi, ameviweka hadharani, imesaidia nini?

Kama hujaviona tafuta uzi mmoja wa dada Faiza, kuna mJF mmoja ameweka ushahidi huko.
 
Ushahidi unatolewa wapi?
Polisi au mahakamani?

Nimesikia kuna wagombea wamefungua kesi za uchaguzi, je hawatakuwa na vielelezo na ushahidi wa kuuwasilisha huko mahakamani?

Lakini CCM wanahitaji ushahidi?

Maalim Seif ana ushahidi na vielelezo vyote kuwa ameshinda uchaguzi, ameviweka hadharani, imesaidia nini?
Kama hujaviona tafuta uzi mmoja wa dada Faiza, kuna mJF mmoja ameweka ushahidi huko
.



Kwa nini unakimbilia Zanzibar? Kama ningetaka kujadili kuhusu Zanzibar ningefanya hivyo! Kama unavyosema ni kweli kwamba Seif ameweka ushahidi hadharani ni kwa nini basi ukawa nao wasifanye hivyo huku wakisubiri kwenda Mahakamani?
 
Kwa akili yako ndogo iv kuna kidume wa kumshtaki LOWASSA au SEIF
 
Kwa nini unakimbilia Zanzibar? Kama ningetaka kujadili kuhusu Zanzibar ningefanya hivyo! Kama unavyosema ni kweli kwamba Seif ameweka ushahidi hadharani ni kwa nini basi ukawa nao wasifanye hivyo huku wakisubiri kwenda Mahakamani?

Zanzibar ndo mfano uliopewa,pamoja na kuweka ushahidi mezani imesaidia nini?!!ebu jibu swali bro
 
Kwa nini unakimbilia Zanzibar? Kama ningetaka kujadili kuhusu Zanzibar ningefanya hivyo! Kama unavyosema ni kweli kwamba Seif ameweka ushahidi hadharani ni kwa nini basi ukawa nao wasifanye hivyo huku wakisubiri kwenda Mahakamani?
Umekimbia swali.

Nimeuliza kwa CCM ushahidi unasaidia nini? Kutenda haki?

Goli la mkono maana yake nini?

Kwa nini NEC ilikimbilia kutangaza matokeo bila kusikiliza malalamiko ya Lowassa?
 
Kama JPM angekuwa anajiamini hivyo si angemruhusu Lowasa ataapike nyongo yake hadharani pale Jangwani?? Mbona mnamzuia? Huo ushahidi auweke wapi kama sio hadharani tuujue tujinyamazie?? Nenda sasa weye mahakamani

UKAWA ni wa ajabu sana. Baada ya kukosa ushindi kwenye sanduku la kura, wanatafuta ushindi barabarani na kwanye vijiwe vya kahawa.
 
Hawanaga ushahidi hao, ni mboyoyo tu. Tumewazoea. Mabomu ya Soweto Arusha walisema wanao ushahidi, wakaambiwa watoe, wakaingia mitini. Wanaowaamini inabidi wapimwe akili. Serikali haina haja ya kusema lolote.
 
UKAWA ni wa ajabu sana. Baada ya kukosa ushindi kwenye sanduku la kura, wanatafuta ushindi barabarani na kwanye vijiwe vya kahawa.

kakosa ushindi au kaporwa ushindi? Ccm wajue hakuna marefu yasiyo na ncha!
 
Umekimbia swali.

Nimeuliza kwa CCM ushahidi unasaidia nini? Kutenda haki?

Goli la mkono maana yake nini?

Kwa nini NEC ilikimbilia kutangaza matokeo bila kusikiliza malalamiko ya Lowassa?

Itasaidia kwa wananchi kujua kilichotokea na hili litawasaidia ukawa pia sana kwani hata wale walioipigia kura CCM wataona jinsi kura zilivyoibiwa na hivyo kuongeza nguvu ya ukawa kwa Wananchi!
Hii italeta uhalali wa kushinikiza wananchi kwa Umoja wao waungane kudai haki yao, lkn kama hakuna ushahidi wowote ule unaoonyeshwa isipokuwa maneno ambayo kila mtu anaweza kuyasema ni Mwananchi gani atakubali kupigania kitu asichokuwa na uhakika nacho?

Hivyo ni kazi rahisi sana kwa ukawa kufanya waite wana Habari watuonyeshe jinsi walivyoibiwa jambo litakalopelekea NEC nayo kujibu mapigo kutoka kwao halafu ukweli utajulikana!

Halafu isitoshe Jumuiya za Kimataifa chini ya wasimamizi wake waliofika hapa nchini wote wanajua kwamba isipokuwa Zanzibar uchaguzi ulikwenda vizuri na bila malalamiko yoyote yale makubwa ktk pande zote mbili, sasa kama ukawa wana vithibitisho na hawatuamini Watz kwa nini basi hata wasivionyesha kwa wasimamaizi wa Umoja wa Mataifa, SADC, Umoja wa Ulaya, Marekani n.k kabla ya tamko la mwisho la wasimamizi hao kutolewa?

Leo hii kila mtu anajua kwamba Raisi wa JMTZ ni Dr.Pombe Magufuli, ameshapongezwa na nchi nyingi Duniani ikiwemo Marekani, Umoja wa Ulaya hata Ban Ki Moon Mkuu wa Umoja wa Mataifa, majirani zetu wote akiongozwa na Mkuu wa AU walifika kwenye sherehe ya kumuapisha Raisi wetu sasa huko kutokumtambua Raisi Magufuli kunakoendelezwa na ukawa kutasaidia nini kama Dunia nzima imesharidhia kwamba Uchaguzi ulikuwa huru na wa haki?
 
Watu mnashangaza sana kama ninyi si waafrika. Mnataka ushahidi upi. Nchi nyingi za Afrika ziko hivyo. Hata leo Ukawa wakiingia madarakani wataakikisha hawaondoki na watatafuta njia yoyote ile waweze kubakia madarakani hata kuiba kura. Mbona ushahidi upo tu aliosema Mheshimiwa Mbatia na hata baada ya kukabidhi polisi hakuna kilichoendelea. Tatizo unaleta hoja hapa ukiwa mpenzi wa ccm lakini jaribu kuwa huna chama na uangalie mazingira yote ya uchaguzi utapata jibu.
 
Kila mara nimekuwa nikimsikia Lowassa, Mbowe, Mbatia &Co. wakisema kwamba wameibiwa kura kwenye uchaguzi uliopita lakini bila kutoa ushahidi wowote ule, sasa nauliza ni kwa nini wasishitakiwe kwa uzushi ambao wanajaribu kuwaaminisha baadhi ya watu mambo ya Uongo?

Hivi sasa kuna baadhi ya wananchi wamepoteza Imani na Serikali na vyombo vyake kwa sababu ya tuhuma za ukawa kwamba serikali yetu iliiba kura wakati mpaka leo hii ukawa hawajaonyesha ushahidi wowote ule. Sasa hamna sheria ya kuwashitaki?

Data zote zipo, ivi unaweza kuiba alaf ukaenda kumshtaki ulomwibia wakati uthibitisho anao? Ivyo vitakuwa vituko vya kwanza vya dunia.
 
Back
Top Bottom