Kwanini Toyota premio inauzwa bei juu?

Kwanini Toyota premio inauzwa bei juu?

Benjamin Nyamseri

Senior Member
Joined
Oct 13, 2020
Posts
149
Reaction score
299
Ni matumaini yangu kuwa mnaendelea vema huko mlipo. Nilikuwa napita pita kwenye mtandao wa beforward kuangalia bei za magari. Nimeshangazwa na bei za Toyota premio. Yaani unakuta gari ya 2004 CIF inasoma $5000 huko, ambayo ni milioni 12 na kitu. Ukiweka kodi za TRA na bandari inafika 24 M. Miaka minne hapo nyuma hizi premio zilikuwa kwenye milioni 15 hivi. Lakini cha kushangaza Toyota wish unakuta CIF $4000 hapo. Naomba kwa waojua kwanini Toyota premio iendane bei sawa na SUVs kama subaru.
 
Hiyo gari inafit Sana Kwa soko la Africa, Kwa kuzingatia

- Hali ya barabara zetu Africa,
-Elimu ya mafundi Wetu wA kiAfrica,
-Upatikanaji WA vipuli vyake,
-uingilianaji WA vipuli na gari brand nyingine

Ni gari sahii Sana kwa wabangaizaji WA kiafrika.
 
Ni kama ilivyo TOYOTA HILUX,
Almaarufu kama Gari ya dunia.
Haijawai kushuka Bei Wala kushuka thamani.
Wanainunua kuanzia wazungu, waarabu , wakorea hadi alshabab
 
Ngoma ngumu nyingine ni carina hii gari haijawahi kushuka bei
20250508_110849.jpg
20250508_110900.png
 
Hata IST miaka minne nyuma ilikuwa 13M,leo ni 18-19M.

Mtu aliyetunza gari yake vizuri,anauza leo kwa bei aliyoagizia 2021 au pungufu ya 1M.

Dualis vipi?
 
Ni kama ilivyo TOYOTA HILUX,
Almaarufu kama Gari ya dunia.
Haijawai kushuka Bei Wala kushuka thamani.
Wanainunua kuanzia wazungu, waarabu , wakorea hadi alshabab
Kwanini gari za Japani ni nzuri kuanzia kwe muenekano tofauti na za India, mfano ndogo Bus za Tata pamoja na ukibwa wake lakini ukiiweka na Coaster Tata inaoneka haina maandhari nzuri ndani ya kuvutia ukiangali viti madirisha na ata muonekano wa eneo la Dashboard halivutii, hii ni kwa gari zote za India ata Double kibin Za Toyota hilux ni nzuri kuliko za Tata.
 
Hivi wakuu kati ya Crown athlete na brevis ipi nzuri kwa maana ya kwamba haina usumbufu sana wa kila mara garage
 
Back
Top Bottom