Kwanini Tanzania ina Jeshi la Polisi la ajabu?

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,529
41,045
Nina hakika, kukifanyika sensa ya kupima ni taasisi gani ya serikali iliyo ya hovyo kuliko zote, Jeshi la Polisi litashika nafasi ya kwanza.

Siku za nyuma kulipokuwa kukitolewa mwenendo wa rushwa nchi, taasisi ambayo kila mwaka ilikuwa inaongoza kwa rushwa ni Jeshi la Polisi likifuatiwa na mahakama.

Jeshi letu la Polisi limejaa maharamia , badala ya kuwa kioo cha utiifu wa sheriana maadili, ndiyo linaongoza kwa kutenda mambo yaliyo kinyume cha sheria.

Badala ya kulinda raia, jeshi la polisi likilinganishwa majeshi yetu mengine yote, ndilo linaloongoza kwa kuua raia.

Watu waliopo ndani ya Jeshi la Polisi, wengi wao ni watu wa ajabu ajabu. Wengine wanafahamika jinsi waliyokuwa watu wema, waungwana, wenye maadili, lakini wakijiunga tu na Jeshi la Polisi, utashangaa.

Hawajui hata kuhoji, mara nyingi ni watu wa kufokafoka.

Hivi chuo cha Polisi huwa kinatoa mafunzo ya namna gani? Kwa nini watu wakienda hicho chuo, wakitoka wawe watu wa ajabu katika jamii?

Ili kuifanya Tanzania kuwa nchi inayoendana na ustaarabu wa Dunia, ni vema Jeshi la Polisi likaundwa upya, hatua ya kwanza ni kuangalia mitaala ya chuo cha Polisi maana ukiangalia matendo ya Polisi wakitoka hicho chuo, ni kama wanaenda kufundishwa ugaidi wa kidola badala ya kuwawadimamizi wa sheria.

Lakini pia kufanyowe tathmini kuona kama ni halali watu wenye akili kidogo, walioshindwa kwenye masomo, ndio wanaostahili kuwa Polisi.

Kuna baadhi ya mambo wanayoyafanya, tunaweza kuwalaumu, kumbe yanachamgiwa na uwezo mdogo wa akili.

Sifa za mtu kuwa askari Polisi ziangaliwe upya. Tusiwe na hao polisi ambao hawajui hata mwongozo wao wa kazi (Police General Order - PGO).

Rais Samia anataka kuijenga Tanzania inayoendana na ustaarabu wa Dunia, lakini tatizo moja kubwa lipo kwa Jeshi la Polisi, ambalo kimsingi ni primitive,ni jeshi lisiloelewa hata thamani ya utu.
 
Shida ya kwanza watanzania wengi hawajui haki zao hivyo polisi hutumia huo mwanya kuwadhulumu haki zao ikiwemo kuwabambikizia kesi.

Mienendo mingi ama taratibu nyingi za kisheria haziko wazi. Mfano dhamana jambo dogo hilo lilikua linafanywa kificho hadi Kangi Lugola alipolipigia kelele.

Polisi wengi pia ni fukara wa kutupwa ukiunganisha na nafasi ya mamlaka waliyopewa basi wanayatumia vibaya kujinufaisha.

Tukiweka taratibu nyingi wazi na watu wakazijua polisi hawatakua na nafasi kubwa kudhulumu watu haki zao.
 
Jeshi la Polisi ni la ajabu kwa sababu lina kiburi cha kuiweka CCM madarakani kwenye kila chaguzi.
 
Polisi linatokana watu hawa hawa sisi sote anatokea mmoja wetu anakuwa polisi, hivyo ni malezi yetu na makuzi yetu sote.
 
Polisi linatokana watu hawa hawa sisi sote anatokea mmoja wetu anakuwa polisi, hivyo ni malezi yetu na makuzi yetu sote.
 
Nina hakika, kukifanyika sensa ya kupima ni taasisi gani ya serikali iliyo ya hovyo kuliko zote, Jeshi la Polisi litashika nafasi ya kwanza.

Siku za nyuma kulipokuwa kukitolewa mwenendo wa rushwa nchi, taasisi ambayo kila mwaka ilikuwa inaongoza kwa rushwa ni Jeshi la Polisi likifuatiwa na mahakama.

Jeshi letu la Polisi limejaa maharamia , badala ya kuwa kioo cha utiifu wa sheriana maadili, ndiyo linaongoza kwa kutenda mambo yaliyo kinyume cha sheria.

Badala ya kulinda raia, jeshi la polisi likilinganishwa majeshi yetu mengine yote, ndilo linaloongoza kwa kuua raia.

Watu waliopo ndani ya Jeshi la Polisi, wengi wao ni watu wa ajabu ajabu. Wengine wanafahamika jinsi waliyokuwa watu wema, waungwana, wenye maadili, lakini wakijiunga tu na Jeshi la Polisi, utashangaa.

Hawajui hata kuhoji, mara nyingi ni watu wa kufokafoka.

Hivi chuo cha Polisi huwa kinatoa mafunzo ya namna gani? Kwa nini watu wakienda hicho chuo, wakitoka wawe watu wa ajabu katika jamii?

Ili kuifanya Tanzania kuwa nchi inayoendana na ustaarabu wa Dunia, ni vema Jeshi la Polisi likaundwa upya, hatua ya kwanza ni kuangalia mitaala ya chuo cha Polisi maana ukiangalia matendo ya Polisi wakitoka hicho chuo, ni kama wanaenda kufundishwa ugaidi wa kidola badala ya kuwawadimamizi wa sheria.

Lakini pia kufanyowe tathmini kuona kama ni halali watu wenye akili kidogo, walioshindwa kwenye masomo, ndio wanaostahili kuwa Polisi.

Kuna baadhi ya mambo wanayoyafanya, tunaweza kuwalaumu, kumbe yanachamgiwa na uwezo mdogo wa akili.

Sifa za mtu kuwa askari Polisi ziangaliwe upya. Tusiwe na hao polisi ambao hawajui hata mwongozo wao wa kazi (Police General Order - PGO).

Rais Samia anataka kuijenga Tanzania inayoendana na ustaarabu wa Dunia, lakini tatizo moja kubwa lipo kwa Jeshi la Polisi, ambalo kimsingi ni primitive,ni jeshi lisiloelewa hata thamani ya utu.
Kwa sababu halifuati sheria,kanuni na taratibu ziilizotumika kufanya kazi zao. Ni tawi la mbogamboga
 
Polisi ni watoto wetu, Baba zetu, Kaka zetu, majirani zetu na marafiki zetu sidhani kama ni wabaya sana kiasi hicho ambacho sasa tunataka kutengeneza sumu mbaya mnooo na kupandikiza mbegu ya chuki dhidi yao. Tutiii sheria bila shuruti ili tupunguze kuingia kwenye 18 zao, hakika wapo askari waelewa sana.
Lkn wewe endelea tu kukejeli polisi ukiwa nyuma ya Keyboard. Siku yamekukuta umemgonga boda boda halafu wenzake 30 wakuunganishie huko nyuma kukukimbiza upewe kisago ndio utajua wanaitwa polisi au POLISI.
Anyway mabadiliko ni muhimu pia

10307361_807166232634618_1686232840898764867_n.jpg
 
Serikali ndio inapaswa kulaumiwa kuhusu polisi , imeshindwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya kazi , vitendea kazi, nyumba , mishahara midogo.
 
Shida ya kwanza watanzania wengi hawajui haki zao hivyo polisi hutumia huo mwanya kuwadhulumu haki zao ikiwemo kuwabambikizia kesi.

Mienendo mingi ama taratibu nyingi za kisheria haziko wazi. Mfano dhamana jambo dogo hilo lilikua linafanywa kificho hadi Kangi Lugola alipolipigia kelele.

Polisi wengi pia ni fukara wa kutupwa ukiunganisha na nafasi ya mamlaka waliyopewa basi wanayatumia vibaya kujinufaisha.

Tukiweka taratibu nyingi wazi na watu wakazijua polisi hawatakua na nafasi kubwa kudhulumu watu haki zao.
Polisi wa Tanzania ukiwaelewesha kuhusu sheria na haki zako wanaanza unajifanya unajua sana eh.
Basi wanakupa kesi ya ziada.
Kwanza polisi watanzania ukiwaelewesha wanapanic
 
Kila unapoona akili yako inakulazimisha uamini kwamba zaidi ya watu 60 elfu ni wajinga kwenye taasisi moja Tafadhali pitia upya fikra zako.

Unapoamini kwamba watu kumi au 20 hawajui kuhusu maandiko yaliyomo kwenye vitabu vyao vitakatifu vya MUNGU basi wanawakilisha waumini wote basi rudi nyumbani jitafakari zaidi inawezekana kunatatizo kichwani mwako.

Kuhusu Polisi kufanya mambo ambayo ni chukizo Kwa WANANCHI wengi hilo linahitaji mikakati ya pamoja ili kuweka SHERIA na miongozo inayokubaliwa na WANANCHI wengi.

Mmomonyoko wa maadili ni mojawapo wa sababu za watumishi wengi kufanya mambo KINYUME na sheria zinavyotaka katika sehemu zao za kazi.

Mimi huwa sijawahi kwenda Polisi ndiyo maana ninasikia tu Kutoka Kwa marafiki na jamaa kuhusu Kero za hawa waheshimiwa lakini nimekuwa mteja mzuri Sana Hosptalini,Bank,Halimashauri,Tanesco nk. huduma zao ni zaidi ya Kero Polisi napata uchungu namna Baba yangu alivyopoteza MAISHA kwenye hosptali kubwa kabisa jinsi madaktari walivyotunyanyapaa matukio kama hayo yakajitokeza Kwa Mama yangu miaka 20 baadaye na wiki iliyopita nilifika hosptali moja Ile huduma ilinitisha nikakimbilis hosptali binafsi mako Daktari ananiambia amechoka ANAKWENDA kupumzika nikiangalia wagonjwa tunaosubiri kumuona kunawngine wanatia huruma.

Wengi akili yetu tumeihamishia Polisi pekee naamini wakati tunaweka vizuri Polisi ili itufae wote basi tusisahau na taasisi nyingine kama watafiti watatusaidia kujua MCHAWI nadhani tuanze kumuua MCHAWI Kwanza.
 
Back
Top Bottom