Kwanini Taksi Mtandao Zinakatazwa Kupaki Uwanja wa Ndege wa Dar?

Tareman

Member
Jun 3, 2019
53
33
Habari zenu wana JamiiForums?

Leo nimekuja na hili suala ambalo nimejaribu kulitafutia uvumbuzi ila sijafanikiwa.

Jumamosi ya tarehe 13/05/2023, nikiwa ndani ya uwanja wa JK T2 jijini Dar es Salaam nilishuhudia mambo ambayo sikutegemea kama yanaweza kutokea hususani kwenye maeneo kama yale yenye ugeni wa kila aina.

Kuna walinzi wenye kuvaa nguo za kiraia kazi yao ni kufunga tairi za gari kwa chuma lenye mnyororo hasa kwa magari yote madogo yanayo park mule ndani kwa madai ni gari zenye kujihusisha na biashara ya Uber na Bolt.

Kwa kweli nilitamani sana kusikia ni nini hasa lengo lao juu ya kile wanachokifanya dhidi ya hizo biashara ya tax mtandao, niliamua kumfuata mmoja wa wale wafungaji wa magari nilijaribu kumhoji ni kwanini wanafunga ila hakuwa na jibu alisema yeye kapewa tu kazi ya kuzifunga gari ndogo zote zitakazo park ndani ya uwanja kwa muda wa dk10 hadi 15.

Ghafla kulizuka mabishano ya wamiliki wa hizo gari zilizofungwa na kupelekea kuitwa kwa Meneja Finance ila hakuwa na muda wa kuja hivyo alikuja msaidizi wake.

Nikaamua kumfuata na yeye ili kumhoji juu ya hicho kilichotokea ila majibu yake hayakuniingia akilini maana alisema wameamua kukataza Tax mtandao kwa sababu za usalama wa wateja wao, akaniambia dereva uber na Bolt wanaruhusiwa kushusha tu abiria na sio kukaa humu ndani.

Pia nikamuuliza na kama kuna abiria wake anayetakiwa kumpokea na bado hajafika nalo limekaaje: akaniambia masuala ya kubeba abiria anatakiwa wasubiriane huko huko nje ya uwanja na sio humu.

Kwa majibu yake nilishangaa ila nilipata kufahamu kuwa Tax za uwanja wa ndege wamiliki wake ni viongozi wa mule ndani kutokana na majibu yake.

Kwenu wana JF kama kuna mwenye ufafanuzi zaidi katika hili naomba nayeye anitoe kibanzi nilicho nacho maana bado nawaza kila mmoja kwenye sekta yake akijiamulia kuweka sheria zake ni nani atakayekuwa salama?
 
Zamani kabisa ilikuwa ukiteremka airport ukachukua taxi halafu ikatokea umeacha mzigo wako kwenye tax ..basi ukienda airport lazima upate mzigo wako...usalama ulikuwa mkubwa Sana ... nafikiri wanajaribu kulinda hilo
 
"Tax za uwanja wa ndege, wamiliki wake ni viongozi wake wa mule ndani", hapo ndo kuna majibu yako yote.
Naomba kuwasilisha.

Ndo maana wamejitungia sheria zenye Zuio kwa Tax mtandao ndani ya uwanja pasipokuwa na sababu zenye kujenga hoja.

Iliwapasa pia kuondoa kodi ya tsh 2000 ya egesho la gari kwa tax mtandao kwa sababu hatakiwi kuegesha gari.

Kwani sheria kama hiyo inahitaji kutungwa na kutekelezwa na mamlaka ya uwanja pasipo kuipeleka sehemu husika ipitishwe.
 
Zamani kabisa ilikuwa ukiteremka airport ukachukua taxi halafu ikatokea umeacha mzigo wako kwenye tax ..basi ukienda airport lazima upate mzigo wako...usalama ulikuwa mkubwa Sana ... nafikiri wanajaribu kulinda hilo

Huu ni mtazamo mzuri mno ila kumbuka hata hizo tax mtandao zina security zake labda kama kuna wapuuzi wachache wenye kuleta ujinga katika ajira za watu
 
1. Wanajuaje kama hili gari ni taksi mtandao au la mtu binafsi tu kaja kumpokea au kumleta mgeni wake?

2. Kupaki zaidi ya dakika 15, ndiyo alama pekee ya kujua kwamba hii ni taksi mtandao?
 
Kwa sasa watu wanaita taxi afu wanasogea nje ya geti

Ila sio mtazamo mzuri hasa kwa upande wakibiashara ukizingatia eneo la biashara ni Airport
Wanakubali kukosa 2000 2000 za tozo ya egesho kwa ujinga tu
 
Hiyo ndio inapelekea kukimbiwa na wateja walitakiwa wabadilike waende sawa na usasa badala yake wanaipinga Technology
Wengi madereva Tax was uwanja was ndege wengi wameishi kwa kuwapiga wateja na bei kubwa, Sasa teknoloji itawaumbua tuuuu, ngoja tuone apa
 
Airport wanakosea Uber ni usafiri uko Dunia nzima wao mbona hawataki technology, hafu tax za mle ni expensive kuliko Uber. Mimi nikishuka natembea Hadi nje naita bolt au uber
 
Back
Top Bottom