DolphinT
JF-Expert Member
- Mar 9, 2016
- 2,366
- 3,457
Mahakama ya Rufaa ya Tanzania leo imeagiza Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufuta vifungu vinne vya sheria vilivyokuwa vikiweka vikwazo mashauri ya kikatiba yenye maslahi ya umma.
Mwaka 2020 bunge lilifanya merekebisho ya sheria mbalimbali pamoja na zile utekelezaji wa Haki za msingi na wajibu (sura ya 3) kwa kuongeza vifungu vya 4(2), 4(3), 4(4), na 4(5). Vifungu hivyo ni mwiba kwa mashauri yenye maslahi ya umma ambayo vilikuwa vilazimisha muambajio awe na muathirika wa moja kwa moja na jambo liliomfanya afungue shauri pia mashauri yote yanayowahusu viongozi wakuu kama vile Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mku, Spika, Naibu Spika wa Bunge na Jaji Mkuu, yafunguliwe dhidi ya Mwanasheria Mkuu na sio kuwahusisha viongozi hao.
Uamuzi huo umesomwa jana tarehe 13 Juni 2025, na Joseph Fovo, Naibu Msajili wa mahakama hiyo ambaye aliusoma kwa njia ya mtandao.
Uamuzi huo uliobatilisha vifungo vyote vinne vilivyolalamikiwa aliyefungua shauri hilo Wakili Onesmo Olengurumwa, mwanaharakati wa haki za binadamu dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Rufaa hiyo Na. 134 ya Mwaka 2022 iliyosikiliza mbele ya jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa: Jaji Rehema Levira, Jaji Wilfred Rumanyika na Jaji Gerald Ngwembe. Wakili Olengurumwa aliwakilishwa na jopo la mawakili maarufu likiongozwa na Prof. Issa Shivji pamoja na Dk. Rugemeleza Nshala, Mpale Mpoki na Wakili John Seka.
Uamuzi huo ulisema kuwa:- Kifungu cha 4(2) kinavunja dhana ya mashauri ya maslahi kwa umma kwa kuhitaji waathirika binafsi pekee, hali inayokinzana na Ibara ya 26(2) ya Katiba.
Kifungu cha 4(3) ni batili kwa kuwa kinachanganya masharti ya Ibara ya 30(3) (maslahi binafsi) na haki za maslahi kwa umma zinazolindwa chini ya Ibara ya 26(2).
Kifungu cha 4(4) ni batili kwa kuwa Mwanasheria Mkuu hana mamlaka ya kikatiba kuwakilisha mihimili mingine, hasa Mahakama au viongozi wa kisiasa walio huru kikatiba kama Jaji Mkuu.
Kifungu cha 4(5) pia ni batili kwa kuwa hakuna sheria nyingine zinazotoa nafuu ya moja kwa moja kwa mashauri ya maslahi ya umma.
Mwaka 2020 bunge lilifanya merekebisho ya sheria mbalimbali pamoja na zile utekelezaji wa Haki za msingi na wajibu (sura ya 3) kwa kuongeza vifungu vya 4(2), 4(3), 4(4), na 4(5). Vifungu hivyo ni mwiba kwa mashauri yenye maslahi ya umma ambayo vilikuwa vilazimisha muambajio awe na muathirika wa moja kwa moja na jambo liliomfanya afungue shauri pia mashauri yote yanayowahusu viongozi wakuu kama vile Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mku, Spika, Naibu Spika wa Bunge na Jaji Mkuu, yafunguliwe dhidi ya Mwanasheria Mkuu na sio kuwahusisha viongozi hao.
Uamuzi huo umesomwa jana tarehe 13 Juni 2025, na Joseph Fovo, Naibu Msajili wa mahakama hiyo ambaye aliusoma kwa njia ya mtandao.
Uamuzi huo uliobatilisha vifungo vyote vinne vilivyolalamikiwa aliyefungua shauri hilo Wakili Onesmo Olengurumwa, mwanaharakati wa haki za binadamu dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Rufaa hiyo Na. 134 ya Mwaka 2022 iliyosikiliza mbele ya jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa: Jaji Rehema Levira, Jaji Wilfred Rumanyika na Jaji Gerald Ngwembe. Wakili Olengurumwa aliwakilishwa na jopo la mawakili maarufu likiongozwa na Prof. Issa Shivji pamoja na Dk. Rugemeleza Nshala, Mpale Mpoki na Wakili John Seka.
Uamuzi huo ulisema kuwa:- Kifungu cha 4(2) kinavunja dhana ya mashauri ya maslahi kwa umma kwa kuhitaji waathirika binafsi pekee, hali inayokinzana na Ibara ya 26(2) ya Katiba.
Kifungu cha 4(3) ni batili kwa kuwa kinachanganya masharti ya Ibara ya 30(3) (maslahi binafsi) na haki za maslahi kwa umma zinazolindwa chini ya Ibara ya 26(2).
Kifungu cha 4(4) ni batili kwa kuwa Mwanasheria Mkuu hana mamlaka ya kikatiba kuwakilisha mihimili mingine, hasa Mahakama au viongozi wa kisiasa walio huru kikatiba kama Jaji Mkuu.
Kifungu cha 4(5) pia ni batili kwa kuwa hakuna sheria nyingine zinazotoa nafuu ya moja kwa moja kwa mashauri ya maslahi ya umma.