Ikiwa lengo la mwanamke kufanya kazi ili kusaidiana katika kuihudumia familia, haiwezi kuwa ni jambo la ajabu kwa wenza kujuana vipato vyao....kwa kuwa wao lengo lao ni moja ambalo ni kuboresha familia.....kwa wanandoa wanawajibika katika kuijenga familia yao...sidhani kama kitendo cha kupanga bajeti za miradi yenu ya kifamilia huku ukimuhusisha mkeo kwa kuwa na yeye pia ana kipato si kumuingilia matumizi yake.....kwa sababu jambo linalofanywa hapo lina manufaa kwenu wote.....ubinafsi ni sumu mbaya kwenye NDOA.....
.wasema " lengo la mwanamke kufanya KAZI ni kusaidiana katika kuihudumia familia" hivyo basi walirudia jambo ulilolikataa hapo juu nambari 58 , kuihudumia familia ni kutumia PESA ya mwanamke, labda nijaribu kukumbusha jambo moja Tarime One alisema kwanza alimsoma mkewe hivyo basi yeye kufanya vile ilikuwa ni ushindi na amani kwenye ndoa yake, ila asijue kwamba anachokifanya ni kufuata kanuni za asili ambazo zinauendesha huu ulimwengu.
Kunaweza kuwako na aina kadhaa/mitindo ambapo ndoa zinajengwa
1: Wote wawili me na ke mnaanza katika hali duni na kupanda taratibu hadi kilele cha mafanikio, NAHISI WE UMELITAZAMA SANA HILI JAMBO KATIKA NDOA HII, nirekebishe kama nimekosea.
2: Me na Ke wote tayari wamejijenga kiuchumi na wanatoka familia zenye PESA, hapa pia tutazungumza tofauti.
3: Ke ana kipato zaidi ya Me, na pia familia yake ni bora zaidi ya Me, hapa tusiseme chochote manake bila Ustaarabu au hekima za Ke sijui!!!!
4: Me ana kipato zaidi ya Ke, wakati huo huo familia ya Me ni zaidi ya Ke.
Na aina nyingine na nyingine yategemea na namna tu utavyoweza kucheza na hali, sasa ukilitazama jambo hili kwa mapana yake mwisho wa siku litaibua mambo mengi zaidi, lakini jambo la msingi katika kumfanya mme abaki na Ukichwa wa nyumba na asifanye vile utakavyo wewe...