Kwanini sitaki kujua kipato cha mke wangu?

Kwanini sitaki kujua kipato cha mke wangu?

Ninachojua mkishaoana mnakuwa mwili mmoja hakuna kitu changu wala chake bali ni chetu km huo utaratibu hakuna basi hapo hakuna ndoa bali watu wawili mtu mke na mtu mme waishio pamoja.... Mfn hutaki kujua mshahara wa mkeo vp siku ukagundua amejenga nyumba nzuri kwao wkt nyje mnakaa ktk nyumba ya kupanga
 
Wanandoa ambao ni mwili mmoja.....hawawezi kufichana mambo yoyote yanayowahusu....kuanza kufichana au kutojishughulisha na mambo yanayomhusu mwenzio ni dalili mbaya ya ndoa inayoelekea kuvunjika....wanaume
tumeagizwa kuwaongoza wanawake katika njia iliyonyooka kwa kuwa sisi ndio viongozi wao na hili ni jukumu letu wanaume....
Na kumuongoza mwanamke si kwa mabavu wala kwa mangumi bali kwa majadiliano na maafikiano ynayolenga kuleta amani ndani ya nyumba na sio mifarakano.....na hapo ndio inapotimia dhana ya mwanaume kuwa kiongozi...
Umenigusa mkuu, Mara ooh simu Yangu usiguse Na Mimi nisiguse yako, wewe kama si mdhambi kwann mumeo au mkeo asiguse simu yako.Narudi kwenye mada, siwezi vumilia hiyo hali ni lazima nijue kipato chake halisi ili niweze kuwa aman moyoni mwangu Na kwa nn anifiche kama kweli ni mtu mwema ???
 
Umenigusa mkuu, Mara ooh simu Yangu usiguse Na Mimi nisiguse yako, wewe kama si mdhambi kwann mumeo au mkeo asiguse simu yako.Narudi kwenye mada, siwezi vumilia hiyo hali ni lazima nijue kipato chake halisi ili niweze kuwa aman moyoni mwangu Na kwa nn anifiche kama kweli ni mtu mwema ???
Sasa kama hujui pato la mkeo mnapangaje mipango ya kimaendeleo ya kifamilia.....??? Mtapangiliaje bajeti ya miradi yenu yenu ya kifamilia bila kuwa na uhakika na kufahamu mapato yenu..????..Kutokufuatilia mapato ya mkeo ambapo wewe ndio kiongozi wake kuna uwezekano mkubwa kwa mkeo kujiingiza katika pesa haramu.....wanandoa lazima wajuane na kufahamiana ili kukamilisha ile dhana ya kuwa wao ni mwili mmoja....
 
Hizi ndoa ili kuepusha vita inabidi mambo mengine ukae kimya tu, ukiulizia sana utakuta kila siku ni ugomvi tu na mwisho mtaanza kutalikiana
 
Ninachojua mkishaoana mnakuwa mwili mmoja hakuna kitu changu wala chake bali ni chetu km huo utaratibu hakuna basi hapo hakuna ndoa bali watu wawili mtu mke na mtu mme waishio pamoja.... Mfn hutaki kujua mshahara wa mkeo vp siku ukagundua amejenga nyumba nzuri kwao wkt nyje mnakaa ktk nyumba ya kupanga

haya mambo ya kutaka kujua kila kitu ndo yanayovunja ndoa nying wakati mwingine ni kuuchuna tu
 
Ninachojua mkishaoana mnakuwa mwili mmoja hakuna kitu changu wala chake bali ni chetu km huo utaratibu hakuna basi hapo hakuna ndoa bali watu wawili mtu mke na mtu mme waishio pamoja.... Mfn hutaki kujua mshahara wa mkeo vp siku ukagundua amejenga nyumba nzuri kwao wkt nyje mnakaa ktk nyumba ya kupanga

Ukijua tabia ya mtu haikusumbui,baada ya kufahamu aina ya mke nilienae ndipo nilianza kujipanga kwa aina yoyote ya matokeo hasi yatakayojitokeza kwenye ndoa,unajua huwezi kuchukua maamuzi kama hayo ghafla tu,kuna udhaifu niliouona ambao utavuruga ndoa yangu na nikachukua hatua,na sijutii.
 
Sasa kama hujui pato la mkeo mnapangaje mipango ya kimaendeleo ya kifamilia.....??? Mtapangiliaje bajeti ya miradi yenu yenu ya kifamilia bila kuwa na uhakika na kufahamu mapato yenu..????..Kutokufuatilia mapato ya mkeo ambapo wewe ndio kiongozi wake kuna uwezekano mkubwa kwa mkeo kujiingiza katika pesa haramu.....wanandoa lazima wajuane na kufahamiana ili kukamilisha ile dhana ya kuwa wao ni mwili mmoja....

Nadhani hapa kuna kitu hakieleweki vizuri na naamini tatizo litakuwa ni "umagharibi" tunaouiga kila iitwapo leo, hivyo vitabu mnavyonukuu juu ya nadharia ya mwili mmoja havijasema mke akija kwako ajihusishe na miradi ya maendeleo, havijasema jasho la mwanamke liliwe na mwanaume, hivyo kama mwanamke alipata nafasi ya kuwa na chanzo cha mapato kabla hajaja kwako hivyo ni vyake achana navyo,

ndio kuna wakati mke huweza kuleta mabadiriko chanya kwenye familia kutokana na PESA yake, lakini hii haikupi haki ya we kuhoji au kuona kwamba alistahili kufanya hivyo, kama kichwa cha familia huwezi kuwa na tabia za aina hii, na kwa wale ambao huweka salary zao mezani ili kupanga matumizi ya pamoja basi na wawape hao wake zao sifa za "ukichwa wa familia" yaani 50/50.

Pasipo kukwepesha maneno jambo la kujifanya unafuatilia mambo ya PESA ya mkeo limekuwa chanzo cha migogoro mingi ya ndoa za kileo/kisasa, kwani tunawabebesha majukumu wake zetu wakati huo akili zao zikiwa zimefundishwa kwa mme we "ua/pambo" nenda katunzwe..
 
Afadhali usikijue tu, kama anatimiza majukumu yake vyema yanini uanze kutaka salary slip kwani wewe bank kwamba anaomba mkopo. mwache mdada awe huru na chake kama anasimamia vema majukumu ya nyumbani.

Kuna wanaume povu linawatoka loh!! sijui ndio wale wa ikifika mwisho wa mwezi tunaulizana "mshahara wako ushaingia???"" loh!!!!!!!!!

Sasa unataka iwe siri ili ukahonge au ili iweje
 
siku ya mke kukuletea gari la 40ml wakati kipato chake 300000 ndipo utaona umuhimu wa kujua kipato cha mkeo, au siku ya majembe act kuja kuzoa mkeo kutokana na lundo la madeni ndio utaona umuhim wa kujua chanzo na kipato cha mkeo, umeanza kwa mkeo itakuja na kwa watoto utasema hutaki kujua mambo ya watoto siku utamkuta binti yako na simu ya gharama zaidi yako
 
Inashangaza sana, unaacha watoto kwa masaa 8 hadi 12, afu mume hajui hata unapata nini?

Hiyo ndoa ni mfu.

Inashangaza sana, hivi kweli natoka nyumbani kwangu giza narudi giza in the name of looking for money inakuwaje wale ninaowapenda kuliko chochote wasijue ninapata nini huko ninakotumia muda wangu na wao mwingi hivi. Je kama anaweza kunisaidia nikapata mahali bora kuliko hapa nilipo sasa. Ninachopata ni kwa ajili yao hao wengine ni ziada tu.

Na hata kama akiniachia majukumu nitafanya pale ninapoweza lakini isiwe kwa makusudi.
 
Hizi ndoa za kipagani ni shida sana, yaani rukhusa kukojoleana, kulala kitanda kimoja etc.lakini sio kushikiana simu wala kuulizana mishahara AJABU.
Mnapofunga ndoa mnakuwa mwili mmoja lakini ndoa nyungi ni miili miwili.Poleni halafu mnavyojikutaga mna busara sasa mpaka mnatia huzuni.Sasa kama hamuaminiani hivyo kwa nini bado mnaishi pamoja? zero brain
 
Ndoa zinatofautiana kwa kiasi kikubwa sana! ningependa niwepa experience yangu! Mimi tulipofunga ndoa na mke wangu, mke wangu alikuwa anapokea mshahara (tahe home mara nne zaidi yangu) na house+other allowances ndiyo zilikuwa zinafanana na mshahara wangu.Before marriage, sikuwa na mpango kabisa na sikuwahi kuulizia kiasi anachopata kazini kwake ingawa mara nyingi alikuwa akiniambia nisijali kuhusu pesa zake za matumizi,

kwani alikuwa anaweza kujimudu. Baada ya kufunga ndoa tu aliniweka wazi kila kitu kuhusu mapato yake...na akaniambia kwa sababu nimemuoa anaomba mshahara wake woote tujumuisha na wa kwangu kwa ajili ya matumizi ya nyumbani....nikamkubalia kwa sababu ndivyo alivyokuwa anataka...miezi kumi baada ya hayo maongezi..

.nikipata kazi nyingine (international NGO) amabayo napata mshahara mara tatu ya mshahara wa mke wangu na bado tuna share mishahara. Kwetu sisi hakuna hela yangu hela yake...lakini sitaki kuamini kwamba hata ndoa zingine zipo hivi.....hivyo tuwe makini sana tunavyojadili mambo ya ndoa za watu...
 
Wanaume wa JF walivyokuja juu na hili suala utafikiri kweli wake zao wanajua vipato vyao....Kama ni kweli na Mungu aendelee kuwatetea kwa hilo.

Ila kwenye misiba tunaona matokeo mengi sana kuwa wajane hawana be wala te wa kilichoachwa na wenza wao....
 
Tarime one

mkuu mwanzo kidogo nikupinge, lakini nilipofikia hitimisho lako nikakubaliana na wewe kwa asilimia 80, nadhani kujua ni vizuri zaidi ili hata unapompa majukumu ujue ana uwezo kiasi gani, ila ni kumwachia uhuru wa kipato chake ni jambo jema sana,

kama ana akiri naye hatatumia huo mwanya vibaya, ila usipokuwa na udhibiti na hicho kipato kwa upande mwingine hicho kipato kinaweza kukugeuka vibaya sana maana anaweza kukitumia vibaya au kuanzisha miradi kwa siri ambayo itamfanya asiwajibike kikamilifu nyumbani.
 
Last edited by a moderator:
Nadhani hapa kuna kitu hakieleweki vizuri na naamini tatizo litakuwa ni "umagharibi" tunaouiga kila iitwapo leo, hivyo vitabu mnavyonukuu juu ya nadharia ya mwili mmoja havijasema mke akija kwako ajihusishe na miradi ya maendeleo, havijasema jasho la mwanamke liliwe na mwanaume, hivyo kama mwanamke alipata nafasi ya kuwa na chanzo cha mapato kabla hajaja kwako hivyo ni vyake achana navyo,

ndio kuna wakati mke huweza kuleta mabadiriko chanya kwenye familia kutokana na PESA yake, lakini hii haikupi haki ya we kuhoji au kuona kwamba alistahili kufanya hivyo, kama kichwa cha familia huwezi kuwa na tabia za aina hii, na kwa wale ambao huweka salary zao mezani ili kupanga matumizi ya pamoja basi na wawape hao wake zao sifa za "ukichwa wa familia" yaani 50/50.

Pasipo kukwepesha maneno jambo la kujifanya unafuatilia mambo ya PESA ya mkeo limekuwa chanzo cha migogoro mingi ya ndoa za kileo/kisasa, kwani tunawabebesha majukumu wake zetu wakati huo akili zao zikiwa zimefundishwa kwa mme we "ua/pambo" nenda katunzwe..
Mkuu tunaongelea uhalali wa wewe kujua pato la mkeo na sio kumfuatilia au kumpangia matumizi ya pato lake.....jikite zaidi hapo kwenye mzizi wa mada....
 
haya mambo ya kutaka kujua kila kitu ndo yanayovunja ndoa nying wakati mwingine ni kuuchuna tu

Kma mlioana kwa kuwa umri umeenda na mnataka watoto, au mmelazimishwa kuoana kwa sababu wazazi wanataka wajukuu ndoa ni makubaliano tangu mwanzo lkn km juna ubinafsi basi yaache yawe hivyo ili msivunje hiyo ndoa kila mtu awe na chake ndoa ikishafika mahakamani mke akitaka talaka ujue mnagawana kile mlichochuma km yeye amejenga kimya kimya na ana asset za kutisha nje ya familia ujue hizo hazigushwi anakuwa amefanikiwa alichopata maana ulimuhudumia vizuri yeye anahudumia miradiyake na ndivyo ilivyo maana wanaendaga mahakamani kudai talaka ni hao hao ambao mnaishi nao kwa kutoingiliana
 
Mkuu tunaongelea uhalali wa wewe kujua pato la mkeo na sio kumfuatilia au kumpangia matumizi ya pato lake.....jikite zaidi hapo kwenye mzizi wa mada....

.labda unijuze wewe mkuu pale ulipouliza nakunukuu
1: Mtapangiliaje mipango ya maendeleo ya familia.
2: Mtapangiliaje bajeti ya miradi yenu....bila kujua kipacho CHENU.
Je hujaona hapo kwamba tayari umeingilia matumizi ya kipato cha mwanamke?..na kwa kufanya hivyo ni kujaribu kuleta usawa kati ya mwanamke na mwanaume jambo ambalo ni hatari kwa uhai wa ndoa..na pia katika ile post niliyokukoti uliongeza kwamba bila kujua mapato ya mkeo anaweza kujiingiza kwenye biashara haramu, YES inaweza kutokea, lakini si LAZIMA kwani wakati wote ndege wafananao huruka PAMOJA, hivyo basi haramu yake ni yako kabla au hata baada ya ndoa.
Mwisho kabisa ya mwanamke yafanywe na mwanamke na ya kwetu wanaume tuwajibike kwayo!!!
 
Back
Top Bottom