Blessed Tajiri
JF-Expert Member
- Dec 16, 2023
- 221
- 659
Wakuu,
Nimejikuta tu najiuliza maswali, kwanini sisi wengi maeneo yetu njia za mtaani ni songombingo hasa kipindi cha mvua, yaani ukitaka kutoka nje mpaka uite mizimu kwanza ukisaidie kupata ujasiri wa kupita😂😂
Sisi wa maeneo mengine kama Sinza, Manzese, Mbezi Beach, Tegeta, Bunju, Kimara, Kigamboni, nk, tofauti na Mikocheni, Upanga, Masaki, na Temeke (kiasi chake wamejitahidi kule) hatustahili kuwa njia nzuri za lami au zege mitaani? Hatuna hiyo hadhi? Au wenzetu ndio wananchi sana sisi wengine tuko vipande jina la wananchi halitutoshi hivyo hatustahili kupata huduma nzuri?
Kuna njia ukipita kama hujapita inabidi usimame kama dk 5 hivi ili upige hesabu za kupita usije ukateleza, ukaanguka ukavunjika utulie nyumbani kujiuguza, mtu mwenyewe ni ansesta wa miaka 30 na kuendelea ukivunjika mfupa unachukua miaka kuungua😂😂😂
Utani pembeni Wakuu, kwanini sisi wengine tunatengwa kupatiwa barabara nzuri?
Na sasa hivi hata danganyatoto za kuchongewa barabara hakuna, yaani tumetelekezwa, tuko kama wahamiaji haramu ambao tumeachwa tu tukae bila usumbufu!🥲
=======
Nimejikuta tu najiuliza maswali, kwanini sisi wengi maeneo yetu njia za mtaani ni songombingo hasa kipindi cha mvua, yaani ukitaka kutoka nje mpaka uite mizimu kwanza ukisaidie kupata ujasiri wa kupita😂😂
Sisi wa maeneo mengine kama Sinza, Manzese, Mbezi Beach, Tegeta, Bunju, Kimara, Kigamboni, nk, tofauti na Mikocheni, Upanga, Masaki, na Temeke (kiasi chake wamejitahidi kule) hatustahili kuwa njia nzuri za lami au zege mitaani? Hatuna hiyo hadhi? Au wenzetu ndio wananchi sana sisi wengine tuko vipande jina la wananchi halitutoshi hivyo hatustahili kupata huduma nzuri?
Kuna njia ukipita kama hujapita inabidi usimame kama dk 5 hivi ili upige hesabu za kupita usije ukateleza, ukaanguka ukavunjika utulie nyumbani kujiuguza, mtu mwenyewe ni ansesta wa miaka 30 na kuendelea ukivunjika mfupa unachukua miaka kuungua😂😂😂
Utani pembeni Wakuu, kwanini sisi wengine tunatengwa kupatiwa barabara nzuri?
Na sasa hivi hata danganyatoto za kuchongewa barabara hakuna, yaani tumetelekezwa, tuko kama wahamiaji haramu ambao tumeachwa tu tukae bila usumbufu!🥲
=======
Umesahau sehemu kubwa wilaya ya Temeke kama Yombo, Buza karibia yote .. Hawa jamaa waliulaga sana. Barabara zina lami/nzege na mifereji mikubwa na taa za barabarani.. hata hizo za upanga zikasome.
Kama upo ubungo sijui kinondoni sijui kibamba kazi ipo