Kwanini Shilingi ya Kenya ina thamani kuliko Shilingi ya Tanzania?

Ongeza hapo neno kusomea uchumi. Sisi wasomi wengine haya mambo yametupita kushoto.
Sio lazima usome kitu flani ili ujue area flani,kuna wachumi kibao wana pHD hawajui hata maana ya blockhain,Defi,smart contract......wakati milions usd of transactions zinapita huko per second...elimu ni zaidi ya kua na vyeti
 
Wakuu turejee.

Huwa najiuliza. Wanaohusika ku adjust (kupandisha na kushusha) thamani ya pesa kwenye mataifa ya kidunia ni nani (najua hii process haifanyei na mungu inafanywa na binadamu)

Pia nilikua najiuliza, Kenya mbona sometimes uchumi wake unayumba lakini thamani yake ya pesa inanaki palepale licha ya kwamba tanzania kuna mali za kutosha na nguvu kazi. Na sisi ndo tunalisha almost east africa nzima. Kama sisi ndo tunategemewa kwa nn sisi ndo pesa yetu isiwe na value kuliko pesa ya nchi yoyote inayo tuzunguka east afrika. Tunafeli wapi.

Pia tunajua nchi kama Kenya thamani yake ya pesa ni kubwa kuliko yetu inakua na advantage kubwa sana kutulalia. Kwa maana ya kwamba. Kwa kazi ile ile atakayofanya Mkenya na Mtanzania.

Mkenya ata gain more akitumia pesa yake. Kwa maana ya kwamba mkenya akija na pesa yaje Tanzania anaweza akanunua magunia ya chakula mengi zaidi kuliko wewe ukienda kenya na tsh. Kwa hiyo hii inampa mkenya advantage ya kutofanya kazi nyingi kama mtz.

Hii ni opinion yangu. Kama una i-challenge. Naomba uje kwenye mada.
halafu unajiita genius kweli?
 
Tshs inajishindanisha na fedha za kigeni, obviously kama wewe hufanyi exportation ya kutosha basi demand ya fedha ya kigeni nchini kwako itakuwa juu kwa sababu wafanyabiasha watahitaji Foreign currencies kuagiza mizigo yao hivyo Local currency yako inaporomoka thamani yake.

Kwa mfano leo tungeuza bidhaa zetu nje zaidi ya tunavyoagiza, by default Tshs yetu ingepanda....na ndiyo tunasema tujitahidi kuzalisha zaidi na zaidi ili tuuze nje !! Kenya kwa mfano wao wanauza bidhaa zao nje kuliko sisi.

Nimtoe tu wasiwasi mtoa hoja kwamba labda kuna taasisi duniani ambayo inapanga hizi thamani za fedha hapana - ni masuala ya kuuza na kununua nje ya nchi yako ndiyo yanashusha ama kupandisha thamani ya fedha yako.
 
Tshs inashindanishwa na fedha za kigeni, obviously kama wewe hufanyi exportation ya kutosha basi demand ya fedha ya kigeni nchini kwako itakuwa juu - na ikiwa juu Local currency yako inaporomoka thamani yake.

Kwa mfano leo tungeuza bidhaa zetu nje zaidi ya tunavyoagiza, by default Tshs yetu ingepanda....na ndiyo tunasema tujitahidi kuzalisha zaidi na zaidi ili tuuze nje !! Kenya kwa mfano wao wanauza bidhaa zao nje kuliko sisi.

Nimtoe tu wasiwasi mtoa hoja kwamba labda kuna taasisi duniani ambayo inapanga hizi thamani za fedha hapana - ni masuala ya kuuza na kununua nje ya nchi yako ndiyo yanashusha ama kupandisha thamani ya fedha yako.
nailed it
 
Kulingana na nadharia ya Purchasing Power Parity (PPP), fedha za nchi zina thamani inayolingana. Thamani ya pesa inapimwa kulingana na baskets of goods and services it can buy. Kama mbuzi mmoja kwa pesa ya Kenya anauzwa sh elf moja na mbuzi 'huyo huyo' kwa Tanzania akawa anauzwa kwa Tsh elfu ishirini then 1000 ya Kenya itakuwa sawa na Tsh 20,000 ya Tanzania.
Vingekua vinathamani sawa vingekua vinalingana digits. Kama ni 1000 kenya inatakiwa pia iwe 1000 tz. Ila kwa sababu thamani ni tofauti ndo maana unaona utofauti
 
Mkenya mwenye laki ni sawa na matanzani mwenye milioni mbili na laki tatu,zingatia hilo kwanza.

Yaani nguvu na thamani ya kuitafuta hiyo pesa inakwenda kwa ratio hiyo.
Usiseme mkenya akiwa na laki na mtanzania akiwa na laki.
Nini maana ya pesa ya mkenya kua na power kuliko ya tanzania kama unabisha kwenye tofauti ya thamani. Yani kama digits doesnt matter. Power ya kenya shilling inaonekana wapi sasa. Na impact ya kenyan shilling iko vipi
 
Kuhusu nani anaudjust sijui.
kuhusu pesa fulani kua kubwa kuliko nyingine,...hio haireflect uchumi wa sehemu ama nchi husika....kinachoangaliwa ni PPP=Purchasing Power Parity,...uwezo wa hio pesa kufanya manunuzi katika sehemu husika,usd 2,ni sawa sawa na Iran rial 80,000 lakini usd 2 Iran unapata kikombe cha kahawa,marekani hupati....hapo means kwa value ile ile purchasing power ya rial ipo juu Kuliko US dollar.......ukubwa wa pesa haupimwi kwa wingi wa masifuri bali hupimwa kwa wingi wa uwezo wa manunuzi
Umejibu vizuri. Dollar ni kubwa kuliko ksh na ina manunuzi makubwa kuliko ksh. Vivyo hivyo ksh ni kubwa kuliko tsh na ksh ina purchasing power kubwa kuliko tsh.
Hapa umenisupport bila kujua umekubaliana na mm
 
Mimi huwa naona ni digits tu ndio huwa tunatofautiana,ila sio Uchumi kukua.kwa mfano,
Shilingi 10000 ya Tanzania ni Sawa na Ksh 450 lakini hapo haimaanishi hiyo 450 ni rahisi kupatikana ukiwa kenya.ni kwamba malipo yaleyale ya tsh 10000 kwa tanzania na kwa kenya ni 450.yani mzazi fukara wa kenya hawezi kumpa mwanae 450 akatumie shuleni ni hela kubwa pia kwao.
Umeeleza vema sana, umeeleweka.
 
Hio 4,444ksh ni pesa ya mshahara mkubwa tu wa mtu Kenya,na huwezi kumiliki hata kipande cha ardhi kulima.
Ila laki 1 Tanzania ni mshahara wa kibarua tu,na hio laki moja unaweza kodi/kununua ardhi mwaka mzima na kulima.....hapo utaona pesa ipi ina thamani Kati ya Ksh ama Tsh?
Ndo utuambie ili uingie kwenye argument. Hatuelewi uko upande gani
 
2005/15 nchi iliongozwa na mchumi. Na dhanani ya fedha yetu alioanda kulikoni. 2015/20 tumeona kupanda na kushuka kwa Tsh. (Mkemia na hesabu)
 
Umejibu vizuri. Dollar ni kubwa kuliko ksh na ina manunuzi makubwa kuliko ksh. Vivyo hivyo ksh ni kubwa kuliko tsh na ksh ina purchasing power kubwa kuliko tsh.
Hapa umenisupport bila kujua umekubaliana na mm
Purchasing power ya Ksh ni ndogo mno kuliko ya Tsh.....laki moja ya Tz,unapata heka moja ya ardhi kijijini mali yako kabisa,ila 4500 ya Kenya ambayo ni laki moja ya Tz hupati uwanja Kenya,.......kumbuka thamani ya pesa hulingaishwa na uhalali wa eneo uliopo,raia wa Kenya haruhusiwi kununua ardhi Tz anakodi tu kwa muda
 
Vingekua vinathamani sawa vingekua vinalingana digits. Kama ni 1000 kenya inatakiwa pia iwe 1000 tz. Ila kwa sababu thamani ni tofauti ndo maana unaona utofauti
Ha haa. Hizo digits zisikuchanganye. Mfano kwa Tz ungeambiwa ulipie mkate kwa kutumia karata ya mavi ya mbuzi kisha Kenya ukaambiwa ulipie kwa karata ya jembe, je kungekuwa na tofauti gani?
 
1. Central Govt fixes the rates to encourage exports. Cases of Chinese Yuan and Vietnemese Dong.

2. Demand and Supply of the currency. Cases of USD, Euro.

3. WB & IMF influence on devaluation.

4. Too much borrowings create stress on local currency.

Case ya Kes na Tzs ni historical.

Kabla ya vita vya Uganda Tzs ilikuwa na nguvu sana almost equal to USD.

Baada ya vita vya Kagera, foreign reserve pale BOT ilikuwa empty.

Ukienda WB na IMF wakaja na SAP ambayo moja ya condition ni currency devaluation.

Tzs ikaanza kushuka thamani, viwanda havikuwa vinazalisha, no exports, more imports. Tzs ikawa inazidi kuanguka.

Kenya ilikuwa tayari industrialized, fedha yake ikawa stable. Tz tukawa tunaenda zaidi kenya kuchukua mzigo.

Mpaka sasa Kes ina nguvu kuliko Tzs.

Uchumi wa nchi haina uhusiano wowote na thamani ya fedha.
 
Lets say mtanzania una laki moja na mkenya ana laki moja. Mkenya pesa yake ina power kuliko yako. Kwa maana ya kwamba wote mki exchange na dollar mkenya anakua ana dollar nyingi kuliko ww. So kama ana dollar nyingi inamaana anaweza akanunua vitu vingi kutoka kwako kuliko ww utakavonunua kutoka kwake. Kwa maana hiyo. Atakufanya ww ulazimike kufanya kazi nyingi kuliko yeye ili ku cover kiasi alicholuzidi kwenye biashara.

Au put it this way. Imagine dunia ingekua na pesa moja. Ingekua rahidi kunielewa. Kwa sababu kungekua hakuna haja ya kutumia nguvu kukuelewesha maana mkenya sasa angetakiwa kuja na laki moja ya tanzania kununua magunia 2 ya mahindi na sisi tungeweza kwenda kenya na laki moja kununua magunia mawili ya mahindi.

Lakini kwa sababu thamani ni tofauti. Ndo maana mkemya anaweza kuja na laki moja akanunua magunia 10 ya mahindi wakati wewe ukienda na laki moja kenya unanunua gunia moja.( mfano)
Mpaka mkenya aipate hiyo 100K lazima afanya kazi kuliko kawaida.

Hiyo 100k haipatikani kirahisi hivyo.
 
Kwa sababu fedha ni bidhaa kama bidhaa nyingine(Rejea Bureau di Change,Banks nk) ndio maana huwa tunasema kupanda na kushuka kwa shilingi,lakini ukitaka kujua uhalisia wa thamani ya pesa nenda mipakani ndio utajua kuwa utofauti uko kwenye namba tu.kwa mfano
Huwezi kukuta bidhaa ambayo sio ya magendo mpakani inauzwa bei tofauti na nchi jirani.na ndio maana hata nauli ya kutoka Kenya kuja Tanzania kwa basi moja huwa haipandi kutokana na mipaka ya nchi bali inabadilika namba tu.
 
Tshs inajishindanisha na fedha za kigeni, obviously kama wewe hufanyi exportation ya kutosha basi demand ya fedha ya kigeni nchini kwako itakuwa juu kwa sababu wafanyabiasha watahitaji Foreign currencies kuagiza mizigo yao hivyo Local currency yako inaporomoka thamani yake.

Kwa mfano leo tungeuza bidhaa zetu nje zaidi ya tunavyoagiza, by default Tshs yetu ingepanda....na ndiyo tunasema tujitahidi kuzalisha zaidi na zaidi ili tuuze nje !! Kenya kwa mfano wao wanauza bidhaa zao nje kuliko sisi.

Nimtoe tu wasiwasi mtoa hoja kwamba labda kuna taasisi duniani ambayo inapanga hizi thamani za fedha hapana - ni masuala ya kuuza na kununua nje ya nchi yako ndiyo yanashusha ama kupandisha thamani ya fedha yako.
OK sasa inazidi kuchanganya. Na labda ni nje ya mada lakini Inakuwaje wanaouza zaidi nje kwa maana kuwa pesa ya Dollar wanayo nyingi hawapo uchumi wa kati na sisi ambao hatuuzi sana nje tupo uchumi wa kati.
 
Jibu la swali hili ni simple basic economy.

DEMAND AND SUPPLY.

Nchi ambao inauhaba wa ku export maranyingi inakuwa na shida / Demand ya pesa za kigeni. Matokeo yako pesa yake inashuka thamani.


Na nchi ikisafirisha sana bidhaa nje ya nchi demand ya pesa za kigeni ni ndogo, hivyo pesa ya nchi hiyo huwa na thamani zaidi kuliko nchi inayoagizia vitu vya nje kwasana.

Ila China ni story tafauti.

USA Wanawalazimisha wapandishe thamani ya oesa zao lkn wachina hawataki..
hii nitsielezea baada kama utanitaka
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom