Kwanini Serikali isilipe fidia simu feki?

Kwanini Serikali isilipe fidia simu feki?

Mimi nishakaa tayari laboratory na team yangu ya ma engineer, tunajipanga VP tutaweza kutumia simu fake baada ya june.
 
wazo lako zuri ila tuambie hili jipu ni nani atumbuliwe?maana kosa ni kwa wanaoingiza wananchi uelewa mdogo tuwasamehe........nani apewe lawama hizi
 
Tatizo la humu Jf watu wanawaza vyama, hata hoja yenye mantiki watu wanafikiria vyama. Hatutaendelea kwa mtindo huu. Kipindi cha nyuma Jf ilikuwa sehemu Makini ya kupata taarifa zenye uhakika na mijadala yenye tija. Siku hizi ni mipasho tu humu.
Kuna mtu anachangia au kuanzisha Mada mpaka unatamani kuulizia umri wake, japo uhuru tunao ila tuutumie vizuri.
Kuhusu mada, tcra walitakiwa kuwaelimisha wananchi jinsi ya kubaini simu halisi na bandia kwani chombo hicho hakijaundwa leo. Pili wadhibiti bidhaa zinazoingizwa nchini walikuwa wanafanya nini wakati kazi ya udhibiti wa bidhaa ni yao. Viongozi tafadhali kabla mwananchi hajaathirika muanze na wale waliopewa dhamana za kusimamia hayo.
 
Pelekeni kwenye nchi ambazo bado hawajazuia hiyo mi-simu yenu feki kama walivyofanya wakenya kutuletea sisi kipindi kile walivyozizuia kwao.
 
Majibu ya kitoto haya. Bidhaa zote kutoka nje zinapoingia vipo vyombo vya serikali vyenye utaalam kuchunguza ubora wake na kuhakikisha kodi inalipwa. Jee ina maana serikali kumbe inakusanya kodi hata kwa bidhaa fake ili kupata mapato bila kuangalia madhara kwa mlaji? Hao wanaonunua simu fake wanajikuta wanazinunua kutoka katika maduka yanayotambuliwa na bidhaa hizo wanaamini zimekaguliwa ubora wake.
Mbona kwenye madawa, vipodozi na vyakula wako makini?au ni kwa vile kuna kuooteza maisha?
Siku nyingine usijibu kama unetoka usingizini
Endelea kuishi kwa hisia....
 
Pelekeni kwenye nchi ambazo bado hawajazuia hiyo mi-simu yenu feki kama walivyofanya wakenya kutuletea sisi kipindi kile walivyozizuia kwao.
Mmoja wa wale 46. Sishangai comment hii.
 
jamani mabondeni mmejenga wenyewe fidia mnataka,barabarani mmejenga wenyewe fidia mnataka na simu feki mmenunua wenyewe fidia mnataka mmeona serikali sasa ni shamba la bibi.Acheni ujinga hakuna cha fidia
Mmoja Wa wale 46 ukiendelea kutetea kubarua kwa nguvu zote.
 
Tatizo nalo liona hapa .nikwamba hizi simu zimeimgia kupitia Yale makontena kumi na moja elfu.kwahiyo serikali ataa wao hawajalipwa ushuru.so kudai fidia sio haki.cha msingi wazihalalishe .na inawezekana Kenya walifanya hivyo.ingawaje ilikuwa kwa malipo kidogo.
 
Kufuatia kutangazwa kwa kuzimwa kwa simu feki,na hasara moja kwa moja kumkuta mwananchi,

Je serikali kwa nini isiwajibike kurudishia gharama wote watakao athirika na zoezi hilo. Sababu
1. Serikali ndio ilikuwa na jukumu la kudhibiti bidhaa hizo, lakini ilishindwa hivyo wananchi wake tayari wameathirika kiafya.

2. Wameshakusanya kodi ya hizo simu.
MKUU, ULIPASWA KUJIULIZA HIVI KABLA YA KUNUNUA KITU CHOCHOTE, JE GHARAMA NI RAHISI?! AU RAHISI NI GHARAMA?!!!
 
Kufuatia kutangazwa kwa kuzimwa kwa simu feki,na hasara moja kwa moja kumkuta mwananchi,

Je serikali kwa nini isiwajibike kurudishia gharama wote watakao athirika na zoezi hilo. Sababu
1. Serikali ndio ilikuwa na jukumu la kudhibiti bidhaa hizo, lakini ilishindwa hivyo wananchi wake tayari wameathirika kiafya.

2. Wameshakusanya kodi ya hizo simu.
Yaani ununue simu feki kwa akilizako alafu serikali ikufidie!?
 
KWENYE UNUNUZI WA SIMU FEKI HAPO TRUMP AKICHAGULIWA MTACHAPWA TUUUUU......MAANA HAKUNA NAMNA NYINGINE...........
 
TFDA wanapita na kukagua bidhaa feki na kuziharibu ili zisifike kwa mlaji na kula sumu kwani ni wajibu wao.
Sasa inakuwaje TBS wanakiri kuwa kuna simu fake na hawachukui hatua wakatizimezagaa
TBS bado haijapewa capacity ya kuwepo kwenye kila upenyo ndani ya nchi hiii..Tanzania inamipaka rasmi isiyozidi 32 na siyoyote inawakaguzi wa TBS lakini vilevile kunamipaka isiyokuwa rasmi mingi sana ambapo pengine bidhaa nyingi feki ndipo inapopitia....kutokana na hlo naona siyo haki kuwatupia jiwe hao TBS kwani pengine kutokuwezeshwa ndipo kuliposababisha wao kutoku-exit kwenye kila border...by tha way unataka serikali ndo iwajibike vipi kuhusu ile simu yako ya techno aliyokuletea mjomba nayo serikali ikulipe fidia? it wont be possible..? wacha wazime tuanze upya...na tutajua watu walikua na visimu feki mara baada ya watu kuacha kupatikana kwenye mitandao...
 
Sheria ya serikali ya 'Sale of goods act Cap 215' inatoa angalizo, 'Buyer be ware'...
Buyer be aware, ni pamoja na kufanya manunuzi katika sehemu sahihi na bidhaa hiyo ikawa na risit ambayo serikali imekusanya kodi. kwa hiyo serikali yenyewe inatoza kodi bidhaa feki.
 
MKUU, ULIPASWA KUJIULIZA HIVI KABLA YA KUNUNUA KITU CHOCHOTE, JE GHARAMA NI RAHISI?! AU RAHISI NI GHARAMA?!!!

unataka kukaririsha watu bidhaa kuwa aghali ndio bora? tazama factors nyingine za pricing.
 
umeniwahi mkuu! nami nilitaka kumpa the same jibu! hilo hilo
Mkuu bidhaa halali zote ni pamoja na kuwa na risiti halali maana hapo serikali imekusanya kodi.
sio mbaya irudishe hizo chenji za wananchi ktk kodi waliyokusanya. Utavunaje usipo panda?
 
Buyer be aware, ni pamoja na kufanya manunuzi katika sehemu sahihi na bidhaa hiyo ikawa na risit ambayo serikali imekusanya kodi. kwa hiyo serikali yenyewe inatoza kodi bidhaa feki.
Hata ukinunua chuma lenye kutu/ tetenasi n.k serikali itakata kodi yake. Serikali haiangaliii ubora wa kitu. Kazi yake ni kuangalia kuwa kodi imekusanywa? Ubora wa bidhaa wewe mwenyewe kama mnunuzi ndio unatakiwa uridhike nao. Yani wewe hushangai hii simu inauzwa laki mbili na hii nyingine inafanana nayo lakini inauzwa elfu thelasini alafu unailamu serikali. Kwa nini usitumie ubongo wako? We ubongo umepewa wa nini?
 
Back
Top Bottom