Kwanini Pasco haipendi serikali ya Magufuli?

Kwanini Pasco haipendi serikali ya Magufuli?

Kimla

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2008
Posts
3,954
Reaction score
7,006
Wanabodi,

Mie nashangaa sana kwanini huyu anayejiita Pasco hapendi chochote kinachofanywa na serikali ya Magufuli. Mbona sijahawi kuona akikosoa matendo mabaya ya watendaji serikalini na wafanyabiashara waliokuwa wanakwepa kodi?

Mbona hata hajawahi kusema chochote juu ya Richmond? Mie nadhani hata kama tuna mahaba na serikali iliyopita na machafu yake, basi tutoe sapport kwa serikali iliyopo ili ifanye kazi yake kama amabavyo wananchi tunataka..
 
Last edited by a moderator:
Bado anaamini lowassa alishinda uchaguzi ila kaibiwa kura.

Maguful kashasema uchaguz umeisha,mda wa kujenga nchi ila wakina Pasco bado wanakinyongo
 
Kama lowasa alishinda kwanini tumeomba hapa watubandikie matokeo ya form za jimbo ili tulinganishe na zile za nec kwanini hawafanyi.mimi anyaway ni chadema lakini naangalia ukweli wa mambo na haki
 
Pasco yuko kwenye payroll ya Wadokozi Ltd...ila kushtukia ni ngumu kwasababu pale Ufipa jamaa hupokea mishahara dirishani kwenye bahasha..No Income tax (PAYE), No NSSF!
 
Last edited by a moderator:
Hatuwezi wote kuwa na mawazo sawa. Ukiona Taifa lenye watu wanaofikiri saresare ujue ni Taifa la mazuzu.

Bty huwa kila baada ya miaka flani anakumbushia nyuzi zake zilizopita na mnamwambia alikuwa mtabiri mzuri!!
 
Wanabodi,
Mie nashangaa sana kwanini huyu anayejiita Pasco hapendi chochote kinachofanywa na serikali ya Magufuli. Mbona sijahawi kuona akikosoa matendo mabaya ya watendaji serikalini na wafanyabiashara waliokuwa wanakwepa kodi?
Mbona hata hajawahi kusema chochote juu ya Richmond? Mie nadhani hata kama tuna mahaba na serikali iliyopita na machafu yake, basi tutoe sapport kwa serikali iliyopo ili ifanye kazi yake kama amabavyo wananchi tunataka..
Mkuu Kiimla, hizi ni tuhuma mzito! , kwa kuanzia, naomba kukanushwa kuwa sio kweli kuwa Pasco wa JF hampendi Magufuli na serikali yake, bali Pasco wa JF ni mkweli daima, ambaye siku zote anasema ukweli halisi kwa kutanguliza mbele maslahi ya taifa bila woga ambapo penye mazuri anasifu, penye mabaya anakosoa tena kwa ukosoaji wa nia njema!, yaani constructive criticism with a good faith!.

Hapa chini nimekuwekea japo threads 10 ambazo zote ni za kusifu utendaji wa Magufuli, kuuthibitisha hizi tuhuma zako humu sio za kweli! .

Kuhusu ukosoaji, na usifiaji, unaweza kukuta sisi ambao tunamkosoa Magufuli ndio tunaomsaidia kuliko hao wanaomsifia! .
Karibu mitaa hii and please take time kufungua bandiko moja moja ushuhudie jinsi watu wanavyomkubali Magufuli!.
Magufuli Kama Nyerere:Ni Mtu wa Watu, Hapapasi, Hamung'unyi, Ni ...
Rais Magufuli ni Simple, Genuine & Down To Earth-He is Simply A ...
Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata ...
Magufuli amecapture attention ya Watanzania, Watu wako makini na ...
Ushauri wa Bure Kwa Lowassa: Kwa Vile ni Magufuli, Kubali Matokeo ...
Je, Kasi ya Magufuli itaua Upinzani Uchwara na Kuimarisha Upinzani ...
Kama Magufuli Anaangalia Clouds TV na Kuipongeza, Kunatuma Ujumbe ...
Kwa Kasi hii ya Magufuli, kuna haja Kufanya Uchaguzi wa Rais 2020 ...
Baraza Jipya: Pongezi kwa JamiiForums, WanaJF watatu(VERIFIED ...

Pasco
 
Pasco kasikia ushauri wa Augustine Lyatonga Mrema! Alikuwa, lakini sasa kakata shauri. Msimuharibie tafadhali.
 
Kama lowasa alishinda kwanini tumeomba hapa watubandikie matokeo ya form za jimbo ili tulinganishe na zile za nec kwanini hawafanyi.mimi anyaway ni chadema lakini naangalia ukweli wa mambo na haki
naaaaaamu na ikithibitika kashinda
what next.
 
Wanabodi,

Mie nashangaa sana kwanini huyu anayejiita Pasco hapendi chochote kinachofanywa na serikali ya Magufuli. Mbona sijahawi kuona akikosoa matendo mabaya ya watendaji serikalini na wafanyabiashara waliokuwa wanakwepa kodi?

Mbona hata hajawahi kusema chochote juu ya Richmond? Mie nadhani hata kama tuna mahaba na serikali iliyopita na machafu yake, basi tutoe sapport kwa serikali iliyopo ili ifanye kazi yake kama amabavyo wananchi tunataka..





Nilifikiri uwenyeji wako hapa jukwaani kwa takribani miaka 8 ungetosha kukufanya uwe na hoja zenye kuakisi ukongwe wako,kinyume chake umekuwa na michango ya hovyo kabisa.Hivi hadi Pasco ambebe huyo mtakatifu wako mgongoni ndiyo uone anamuunga mkono au la??Unataka mtu afanyeje ili aonekane anamuunga mkono huyo mtu wako?

Kutofautiana katika baadhi ya mambo na kukubaliana katika mambo ya msingi ni kanuni ya kimaumbile,ukiona mtu anakubaliana na kila jambo lifanywalo na mwanadamu mwenzake,hizo ni dalili za mtu huyo kutokuwa na matumizi sahihi ya kichwa chake.Badala ya kukitumia kichwa chake kufikiri,ameamua kukitumia kuoneshea mitindo ya nywele.

Yawezekana watu tukatofautiana katika mambo fulani,lakini tofauti zetu zisichukuliwe kuwa ni chuki juu ya yule uliyeamua wewe kumpenda katika kila jambo alifanyalo.Zipo hoja nyingi tu zilizoletwa hapa jukwaani na Pasco,zinazoonesha kuuunga mkono utendaji wa Mh.JPM,lakini kuna hoja pia alizozileta zinazokosoa utendaji wa JPM,sasa ulitaka misimamo ya watu juu ya JPM isibadilike?Kama wewe umeamua kuwa na ufuasi na ushabiki wa kikondoo hata katika mambo ya msingi ambayo sote tunaona hayapo sawa,huo ubaki kuwa msimamo wako,usiwalazimishe watu wapende kila kitu kifanywacho na serikali mithiri ya jeshi la policcm linalowalazimisha watu walisifie hata katika mambo ambayo yanaonekana dhahiri kuwa yanafanywa kwa mlengo wa kukibeba chama tawala.

Jamii iliyoacha wajibu wake wa kufikiri na kupanga kwa mustakabali wa ustawi wake,badala yake ikaamua kuwa mshangiliaji wa ghiriba za kisiasa,ni jamii mfu na isiyo na maono.Tusipoziruhusu fikra zetu kufikiri sawa sawa na kuyaruhusu macho yetu na ubongo wetu kuunda taswira sahihi ya yale tuyaonayo,kamwe hatutaweza kutambua jema na baya,tutabaki kuwa washangiliaji wa mambo ya kipuuzi na yasiyo na majibu ya changamoto zinazotukabili kama Taifa.Ukondoo wa namna hiyo unapatikana kwa makada wa aina yako tu,makada waliokunywa maji ya bendera kiasi cha kuvigeuza vyama vyao kama dini ya Mwenyezi Mungu,huo ni upumbav zaidi ya upumbav wenyewe.Badirika.
 
Back
Top Bottom