Kwanini paliitwa 'Kariakoo'?

Kwanini paliitwa 'Kariakoo'?

Mala nyingi majina ya miji au mitaa uitwa majina ya watu mashuhuri wa kitaifa au kimataifa, ua kutokana na matukio yliyokuwa yanatokea sehemu husika. Naomba mwenye kujua jina Kariakoo lilitokana na nini anijulishe tafadhali.

Carrier Corpses: Watumwa waliokamatwa toka bara kituo kikubwa kilikua pale Kariakoo baadae walipelekwa Kilwa na kupandishwa ktk majahazi makubwa na kupelekwa Arabuni na kwingineko kwa ajili ya kuongeza nguvu kazi ktk viwanda.
Watumwa walitembea kwa miguu umbali mrefu sana wakiwa na mizigo ya pembe za ndovu hadi Kariakoo; Wengi wao hadi kufika Kariakoo, walikuwa wamedhoofu sana na kuitwa: Carrier Corpses - mizoga iliyobeba mizigo.

Hatimaye Waswahili wakaita sehemu hiyo Kariakoo, kwani hawakuweza kutamka vema maneno :CARRIER CORPSE.
 
Baada ya vita kuu ya dunia ya 2 Askari wa ki afrika waliorudi kutoka vitani waligawia Hilo eneo na pakaitwa carrier cops. Waswahili wakawa wanatamka kariakoo.

mmmh???
 
yah kuna hiyo ya carrier cops-ikawa kariakoo
what kind of rock-- ikawa kindoroko
long journey -- ikawa longijave
check line ---- chekereni
zipo nyingi sana yaani unaweza cheka ukawa huna mbavu

"Cow way", Kawe, "Njia ya ng'ombe", Chang'ombe. "Idodomya",Dodoma!
 
Carrier Cops maana yake ni Askari wasafirisha mizigo vitani(kwasasa watu wa mfano wao huitwa wabeba box)


...Mkuu ilikuwa ni Corps kwa maana ya 'A special Army Unit' katika hili la Kariakoo ikiwa na maana ya Askari maalumu wa Kubeba Mzigo yaani Carrier Corps... na sio ile Cops yenye maana ya 'Police Officer'!
 
Carrier Corpses: Watumwa waliokamatwa toka bara kituo kikubwa kilikua pale Kariakoo baadae walipelekwa Kilwa na kupandishwa ktk majahazi makubwa na kupelekwa Arabuni na kwingineko kwa ajili ya kuongeza nguvu kazi ktk viwanda.
Watumwa walitembea kwa miguu umbali mrefu sana wakiwa na mizigo ya pembe za ndovu hadi Kariakoo; Wengi wao hadi kufika Kariakoo, walikuwa wamedhoofu sana na kuitwa: Carrier Corpses - mizoga iliyobeba mizigo.

Hatimaye Waswahili wakaita sehemu hiyo Kariakoo, kwani hawakuweza kutamka vema maneno :CARRIER CORPSE.

...mmm, Mkuu Adoe, Nijuavyo, hapo Kariakoo palikuwa Kituo cha Wapagazi wa Kibantu kwa ajili ya Kubeba vifaa vya Vita kwa ajili ya Jeshi la Mkoloni na waliojulikana kwa jina la CARRIER CORPS - jeshi la Wapagazi - lililokuwa likipigana Burma, India na kwingineko. Hii maana yako uliyotoa hii....mmmmmmm, Haya Bana!!!:confused2::smiling::becky:
 
Hayo majina ya uko Zanzibar hata kuyatamka huwa napata ukakasi kinywani, lakini hata huku Tanganyika kuna Kunduchi.
Endelea kulinganisha ,zanzibar kuna makunduchi ,mtu haliwa (haliwi), mzuri hendi(haendi),mgeni haji,kiinua miguu,mfereji maringo,mwembe mimba!
 
Na Bagamoyo ilitokana na watumwa kukata tamaa ya kurudi makwao walipofika bandarini tayari kwenda kuuzwa,kwa hiyo wakawa wana bwaga moyo.na Msasani inatokana na jina la Musa Hassan,sasa wakazi wengi wa maendeo hayo enzi hizo walikuwa ndugu zetu Wamakonde ambao badala ya kusema naenda kwa Musa Hassan ,waliishia kutamuka naenda kwa Msasani
 
Back
Top Bottom