Kwanini nilimfukuza Kikwete????

Mvaa Tai

JF-Expert Member
Aug 11, 2009
6,159
4,443
Mara nyingi wakati wa uchaguzi mtu humpigia kura mtu amtakaye awe kiongozi wake akiwa ana sababu mbalimbali, Pia huwa na mtu ambaye asingependa kabisa awe kiongozi wake kiasi kwamba hata angelishindanishwa na kivuri angechagua kivuli(rejea miaka ya nyuma enzi za chama kimoja)

Kura ya mtu ni siri lakini kwasababu hapa Jamvini watu tunajifunza mengi sana kutoka kwa wachangiaji mbalimbali hivyo nafurahi leo hii kutoa siri yangu kwamba nilimpigia kura Dr Slaa na kuwaambia wenzangu kwamba sikumpigia kura Kikwete kwasababu nyingi tuu na nilitegemea hatoshinda lakini ikawa tofauti, zifuatazo ni baadhi ya sababu zilizonifanya nisimchague Kikwete.

1. Namuona kama hana uchungu na nchi yake, naamini anawakingia kifua Wezi wa rasilimali za nchi hata wanapobainika wazi. Mfano wezi wa pesa za EPA pamoja na kwamba wanafahamika aliamuru warudishe pesa walizoiba kisha waendelee kuwa huru japo mpaka wakati wa kampeni hakusema ni nani karudisha na nani bado na amechukuliwa hatua gani mpaka sasa. Kutokana na hili niliamua kumfukuza kazi.

2. Ninamuona kama ni mbabaishaji na mbahatishaji, kitendo chake cha kuunda baraza la mawaziri na baada ya mda fulani kutumia mda mwingi kuhamisha mawaziri toka wizara moja hadi nyingine, inaonyesha kwamba hafahamu uwezo wao hivyo ana bahatisha. Mfano Dr Shukuru Jumanne Kawamb’waalimteua kama Waziri wa Mawasiliano, sayansi na teknolojia baadaye akagundua amekosea, akamuhamisha kwenda Wizara ya maendeleo ya miundombinu, hivi sasa huyu mtu ni waziri wa elimu naamini ipo siku atapata mahala sahihi pa kumuweka. Uzaifu huu ulinifanya nimfukuze kazi kikwete.

3. Nina muona kama hana Confidence, Katika kipindi chake kilichopita amekuwa anapenda sana kukaa na kuongea masuala nyeti ya nchi na wazee wa Dar es salaam ambao mimi naamini angewaacha wapumzike maana wamelitumikia Taifa kwa mda mrefu sana sasa na matunda yao tunayaona pia, hivyo angeyageukia makundi mengine kama vile Wawakilishi wa vyuo vikuu na taasisi mbalimbali nchini, Vijana wa Dar es Salaam nakadhalika, pia kitendo cha kukataa mijadala wakati wa kampeni nilihisi hana Confidence ya kushindanisha hoja zake na wenzake, hii pia ilipelekea nimfukuze kazi kikwete.

4. Namuona kama ni mtu asiyejali. Anadaiwa kutamka kwamba wanafunzi kupata uja uzito mashuleni wanajitakia wenyewe, haya si maneno mazuri kutoka kwa mzazi na Rais wa nchi. Hili nalo lilipelekea nimfukuze kazi kikwete.

5. Namuona kama ni muongo, katika kampeni zake za awamu yake ya kwanza aliniambia kwamba atahakikisha maisha bora kwa kila Mtanzania, japo nilistuka kidogo, lakini nikamuamini tu nikampa kura yangu, kumbe alikuwa ananidanganya. Kwasababu binafsi sipendi mtumishi muongo, hili pia lilipelekea awamu hii nimfukuze kazi.



6. Na hivi karibuni nimegundua kwamba hayupo Serious, hii ni baada ya kutamka hadharani kwamba hamfahamu muwekezaji wa DOWANS, kama Rais wa nchi hamfahamu muwekezaji mkubwa kama huyo sisi wananchi itakuwaje? Hivyo nina shaka ipo siku nchi itauzwa yeye akiwa hana habari.


Hizi ni sababu zangu zilizo nipelekea nisimchague Kikwete naweza kuwa nilimuonea au nilimtendea haki nakaribisha maoni maana yatanisaidia kimsimamo hapo mwaka 2015
 
Sababu zote ulizotoa za kutompigia kura Kikwete nakubaliana nalo

Je kwa nini sasa ulimpa kura Slaa? mwaga ma-point
 
7. Anatoa ahadi hovyo hovyo na nyingi ambazo utekelezaji wake ni mgumu hasa kwa uchumi wa nchi yetu.

8. Hana uthubutu wa kufanya maamuzi magumu, mfano kuwafikisha watu wote ambao imebainika kuwa waliliibia taifa, instead anawapa muda waungame, tht's bul***t

Summation of all th reasons above made me too not only to vote for him, also to see him as "JOKE" to be a head of state.
 
Sababu zote ulizotoa za kutompigia kura Kikwete nakubaliana nalo

Je kwa nini sasa ulimpa kura Slaa? mwaga ma-point

Bado naziorodhesha maana zipo nyingi sana nashindwa kuzisamaraizi
 
Mi nilimpigia jk,hakuna raisi kama yeye na hatapata kuwepo kama yeye tena
 
Nadhani next time utataja mazuri yake japo kwa uchache maana binaadamu huwa na mazuri yake pia

Nimsaidie kidogo:
-Kavunja Baraza la Mawaziri mwaka 2008 na kumtosa EL.
-Kavunja Kamati Kuu ya CCM na kumtosa RA, AC, YM, among others.
-Nchi ya Zanzibar imezaliwa upya.
-Hakuna mgombea wa wazi wa CCM 2015.
 
Mi nilimpigia jk,hakuna raisi kama yeye na hatapata kuwepo kama yeye tena

Nakubaliana na wewe kuwa hakuna rais kama yeye na hatakuwepo kwa sababu zifuatazo (kwa uchache tu):
  1. Ni rais pekee asiyejuwa kwa nini watu wake ni masikini
  2. Ni rais pekee ambaye anasema hakujua kutakuwa na shida ya walimu walipoanzisha sekondari kata.
  3. Ni rais pekee asiyemjua mmiliki wa kampuni ambayo serikali yake iliingia nayo makataba wa kufua umeme
  4. Ni rais pekee anayejua matatizo ya wasichana kupata mimba kuwa ni kiherehere chao
  5. Ni rais peke aliyetoa ahadi kibao wakati wa kampeni halafu baada ya siku 100 akasema hawezi kuondoa matatizo ya wananchi wake kwa kuwa hata waliomtangulia walishindwa
  6. Ni rais pekee anayeweza kutoa mfano wa kujivua gamba bila kufikiria mantiki yake halisi: Kuwa ni nyoka tu anayeweza kujivua magamba na kisha akaendelea kutema sumu yake kama mwanzo. [Hivyo ccm ni nyoka yule yule]
  7. nk, nk. ... (the list is long)
Kwa sababu hizo; naunga mkono hoja yako!
 
Nakubaliana na wewe kuwa hakuna rais kama yeye na hatakuwepo kwa sababu zifuatazo (kwa uchache tu):

  1. Ni rais pekee asiyejuwa kwa nini watu wake ni masikini
  2. Ni rais pekee ambaye anasema hakujua kutakuwa na shida ya walimu walipoanzisha sekondari kata.
  3. Ni rais pekee asiyemjua mmiliki wa kampuni ambayo serikali yake iliingia nayo makataba wa kufua umeme
  4. Ni rais pekee anayejua matatizo ya wasichana kupata mimba kuwa ni kiherehere chao
  5. Ni rais peke aliyetoa ahadi kibao wakati wa kampeni halafu baada ya siku 100 akasema hawezi kuondoa matatizo ya wananchi wake kwa kuwa hata waliomtangulia walishindwa
  6. Ni rais pekee anayeweza kutoa mfano wa kujivua gamba bila kufikiria mantiki yake halisi: Kuwa ni nyoka tu anayeweza kujivua magamba na kisha akaendelea kutema sumu yake kama mwanzo. [Hivyo ccm ni nyoka yule yule]
  7. nk, nk. ... (the list is long)
Kwa sababu hizo; naunga mkono hoja yako!

Ni katika utawala wake pia umeweza kuyazungumza hayo uyazungumzayo maana ingekuwa Rais mwingine ungeenda jera
 
Ni katika utawala wake pia umeweza kuyazungumza hayo uyazungumzayo maana ingekuwa Rais mwingine ungeenda jera

Jera au jela? Anyway nimekuelewa! Hii ni shida ya kizazi cha zidumu fikra. Kwamba kufikiri nje ya mwenyekiti ni kuvunja sheria! Sioni lolote ambalo lingenipeleka jela hapo.
 
Mi nilimpigia jk,hakuna raisi kama yeye na hatapata kuwepo kama yeye tena
NATAMANI HIYO SEHEMU YA PILI YA SENTENSI YAKO IWE HIVYO MILELE! Maana ikitokea kumpata tena rais wa hivi, itakuwa sawa na sunami la Japan kuikumba Zanzibar!!
 
Jera au jela? Anyway nimekuelewa! Hii ni shida ya kizazi cha zidumu fikra. Kwamba kufikiri nje ya mwenyekiti ni kuvunja sheria! Sioni lolote ambalo lingenipeleka jela hapo.

Sidhani kama umenielewa nilichotaka kumaanisha, mimi namaanisha katika utawala wake kuna uhuru wa kujieleza kwani hujawahi kuona nchi ambayo ni vigumu sana kumsema Rais wa nchi kama tufanyavyo hapa kwetu?
 
Nilishaseeeema sana kuhusu attirbutes za JK.

Simtofautishi na Laurent Gbagbo!!! Na nihisi yatamkuta yaliyo mkuta mwenzake Ivory Coast.
 
Back
Top Bottom