*Sex is designed to happen between married people. It is an emotional and spiritual glue designed by God to bind wife and husband together for life. Making love celebrates the intimacy and commitment of marriage.
*Sex is about "becoming one" in body, but also one in soul. Sex is more than skin on skin, it's heart joining another heart. When you sleep with someone, you give part of yourself to them and take part of them into you.
*Sex is meant to be free - shame. If it needs people to keep secrets, then it's less than God's best. Sex should bring joy and peace, not fear, shame, loneliness and regrets
Ndiyo maana linaitwa "tendo la ndoa, na sio tendo la urafiki wala uchumba. Kama ngono haiwafanyi watu wawili kuwa mwili mmoja, na tena kama ngono inaondoa utakatifu wa miili yenu basi hiyo ni dhambi. "Miili yenu ni hekalu takatifu la kumpendeza Mungu".
I wakorintho 7:2, 8-9.
"Lakini kwa sababu ya zinaa, Kila mwanaume na awe na mke wake mwenyewe, na Kila mwanamke awe na mume wake mwenyewe.
8. Lakini nawaambia wale wasiooa bado na wajane. Ni heri wakae kama mimi nilivyo.
9. Lakini ikiwa hawawezi kujizuia na waoe: maana ni afadhali kuoa
Kuliko kuwaka tamaa
1 wakorintho 6:18.. Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake, Ila yeye afanyaye zinaa, hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe.
Waebrania 13:4 Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu". Kwa hiyo tukizini au kufanya uasherati tutaadhibiwa vizuri tu
Mithali 6:32 " Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa. Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake.". Kwa hiyo ngono inapanda maangamizi na uharibifu kwenu. Mifano tunayo kabisa, Sodoma na Gomora ilivyoangamia kwa sababu ya uzinzi. Nuhu na gharika, kuhani Eli na watoto wake Hofni na Finehasi wote walifariki. Wana wa Israel kupigwa na adui zao Wafilisti hadi sanduku la Agano la Mungu kutekwa; yote ni sababu ya uzinzi.
Na pia zinaa huondoa ufahamu (Hosea 4:11) "uzinzi na divai na divai mpya huondoa fahamu za binadamu"
Na maandiko yanasema "basi mpingeni shetani naye Atawakimbia". Yakobo 4:7
Lakini maandiko hayasemi ipingeni zinaa; bali yanasema "Ikimbieni zinaa". Kama ambavyo Yusufu alikimbia akaacha nguo zake ili asizini na mke wa bwana wake.
2. Kwa nini ngono isiwe dhambi kwa wanyama ila kwa binadamu. Mungu ametupa "conscious" binadamu tofauti na viumbe vingine. Tuna uwezo wa kutambua mema na mabaya. Ndo maana hata kwenye uzinzi mbona hufanyi na dada/kaka zako unaenda kutafuta watu ambao si ndugu zako?
3. Kwa nini kumtamani mwanamke ni sawa na kuwa umeshazini naye. Kutamani mwanamke asiye mkeo ni kuuwashia tamaa mwili wako. Unakaribisha uzinzi. "Roho I radhi lakini mwili ni dhaifu". Roho inataka tu iishie kwenye kutamani lakini mwili utakupelekea kwenye uzinzi
Zaburi 119: 37 " Uyageuze macho yangu, nisitazame visivyofaa".
Eva aliishia kutenda dhambi kwa sababu ya macho yake. Yule nyoka mwerevu alimdanganya Eva " mwanamke alipoona ule mti wafaa kwa chakula, WAPENDEZA KWA MACHO, nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa...... (mwanzo 2:6)
Mwanzo 6:2 " wana wa Mungu WALIWAONA hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri
; wakajitwalia wake wowote waliojichagulia". Mwisho wake ni gharika ya Nuhu
Kwa hiyo macho yako yana nguvu kubwa sana ya kuchochea tamaa ndani yako. Yazuiye macho yako yasione wala kufurahia yale maovu
Credit: sister Judith, Mwl Mwakasege et al