Kwanini nchi za Magharibi hupenda kukopesha zaidi nchi Maskini kwenye miradi ya huduma za jamiii badala ya Uzalishaji?

Japan, Ujerumani na Korea Kaskazini.

Ahsante mkuu, ukiongelea hizo nchi za wenzetu walishatuacha kitambo sana.

Mleta uzi amejikita zaidi kwenye hizi nchi masikini nyingi zikiwa bara la Africa.

US mwenyewe sio kwamba hakopi, anakopa ila anaamua akope kwa ajili ya nini na atatumiaje mkopo wake.

Shida hapa sie nchi masikini, unapewa mkopo na kupangiwa namna ya kuutumia huo mkopo.

Mara zote hua nashauri serikali zetu zingetumia muda mwingi kupembua vipaumbele vyao kama nchi kisha waamue wanataka wakope kwa miradi ipi itakayoleta tija.

Uliona wapi tumepigwa kwenye deal la radar na ikaamuliwa kwamba tulipigwa, mnaambiwa mnarudishiwa pesa yenu lakini iende kwenye madawati au kununua vitabu, seriously? Utasema kweli huyo mtu ana nia njema na maendeleo ya nchi yenu?

Kwanini wasiwarudishie tu pesa mkaamua wapi muielekeze kulingana na vipaumbele vyenu?
 
Hivi ni kwanini nchi za Magharibi hupenda kukopesha zaidi nchi Maskini kwenye miradi ya huduma za jamiii badala ya Uzalishaji?

Mikopo italipika vipi wakati pesa nyingi wanatukopesha kwa ajili ya huduma za jamiii?

Na kwanini tunapenda kupokea? Kwanini tusiwaambie watukopeshe zisaidie kwenye Uzalishaji zaidi?
sasa kwenye uzalishaji wanamkopesha nani maana serikali haizalishi
 
Asante kwako elimu muhimu kwenye sekta zote zikiwemo za siasa

Nikuulize swali Kama Elimu muhimu kwa Nini Chadema mwenyekiti wake wa Taifa elimu yake Ni form six Division zero ya Ihungo secondary wakati Chadema Kuna wasomi Kama akina Dokta Lwaitama wenye PhD?


Kwa Nini mliweka form six Division zero kuwa mwenyekiti wa Chadema Taifa?
Kwanza mimi sihusiki na kumweka kwenye uongozi mtu yeyote wa CHADEMA.

Lakini uzingatie sana hoja yangu ya quality education. Nina mfano mmoja sitaki kuweka hapa maana itakuwa risala. Lakini kwenye mradi mmoja mdogo wa umeme wa maji ilidhihirika wazi kuwa technician mjerumani aliyekuwa amesomea Ujerumani alikuwa na uwezo mkubwa kiutendaji kiasi cha kuanzisha na kuhakikisha mradi wa umeme unakamilika, wakati mhandisi mtanzania wa TANESCO aliyesomea UDSM na mwenye miaka mingi kazini kuliko huyo kijana alishindwa.

Quality education haimaanishi kuwa na makaratasi na vyeti vingi au kukaa darasani miaka mingi au kupata A na B+ na first class degree, it is about knowledge. Wasomi tunao wengi lakini hawana knowledge. Nini kinawafanya wasiwe na knowledge? Ni poor quality ya elimu yetu.

Ndiyo maana, ukiingalia mijadala yetu hata hapa JF, hata mahali pengine popote kwenye ushindani, watu wanaweza zaidi mipasho, na siyo hoja.
 
Hivi ni kwanini nchi za Magharibi hupenda kukopesha zaidi nchi Maskini kwenye miradi ya huduma za jamiii badala ya Uzalishaji?

Mikopo italipika vipi wakati pesa nyingi wanatukopesha kwa ajili ya huduma za jamiii?

Na kwanini tunapenda kupokea? Kwanini tusiwaambie watukopeshe zisaidie kwenye Uzalishaji zaidi?
Sababu matatizo mengi ktk nchi maskini ni huduma za kijamii.

Haiwezi kulipika sababu matatizo nayo huongezeka kutokana na kuongezeka kwa idadi ya watu ambao wengi wao ni maskini.

Inatubidi tukope ili walau tupunguze hali ya umaskini,huku tukijitahidi kuweka mazingira wezeshi ya kuondoa umaskini na kukaribisha wawekezaji wenye mitaji mikubwa kuwekeza katika uzalishaji ili walau watu wetu wapate uzoefu na mitaji.
 
Rekebisha. Ni Korea Kusini, siyo Kaskazini.

Ongeza pia mataifa kama Australia,Mexico na Brazil.
Yote hayo watu weupe watupu Hakuna nchi ya kiafrika hata moja na hawajawahi kopa kwa ajili ya huduma za jamii
 
Kasome Marshall Plan wewe kilaza,
Tatizo elimu yetu imekuwa dhaifu sana hata mambo madogo kama haya unakuta jitu zima lililomaliza chuo kikuu halijui.
Uongo mikopo Ni asilimia ndogo mno ya bajeti zao Halafu hawajawahi kopa kwa ajili ya huduma za jamii ni kwa ajili ya uzalishaji
 
Israel
Lengo la hao wakopeshaji halijawahi kulenga kutukomboa kiuchumi.

Kama kuna mtu ana maoni tofauti atuambie ni nchi gani hawa jamaa waliikopesha na kuisaidia sasa hivi imesimama kama yenyewe haihitaji misaada wala mikopo tena, ataje moja tu.
 
Ndiege, mwendokasi, reli UCHWARA ya SGR, bawa la Nyerere, mibarabara UCHWARA ni huduma za jamii?
Tuelimishe Taratibu zote hizo mikopo? Kama Mikopo basi Magufuli alifanya mageuzi makubwa kuwa tukope miradi ya uzalishaji lakini ujenzi wa madarasa na elimu bure na hospitali tutumie pesa za ndani sio Mikopo

Kukopa kwa akiki ya kugharimia pure huruma za Jamii Ni nchi kujitia umaskini
 
Lengo la hao wakopeshaji halijawahi kulenga kutukomboa kiuchumi.

Kama kuna mtu ana maoni tofauti atuambie ni nchi gani hawa jamaa waliikopesha na kuisaidia sasa hivi imesimama kama yenyewe haihitaji misaada wala mikopo tena, ataje moja tu.
Hakuna nchi Duniani iliyosimama na ahihitaji mikopo.. MAREKANI ni miongoni mwa nchi yenye mikopo zaidi kutoka Bank ya Dunia na wahisani mbalimbali...
 
Itendee haki akili yako jikite kwenye hoja
KWA HELA ALIYOIBA YEYE NA GENGE LAKE WALIOKOPA ZINGETUMIKA INGESHAKAMILISHA SASA HIVI IYO SGR KUTOKA DAR HADI MWANZA. KAFA KAONDOKA KAZI ACHA NA AMEMUACHA BRAZA LISSU AKIDUNDA.
 
Viwanda vya kuchakata korosho, mbolea kuchkata matunda, na bidhaa zote zitokanazo na kilimo,
Miundo mbinu kama reli na barabara kisha mengune hayo ya kijamii tutajitrngenezea wenyewe
Hata siku moja developing country haina uwezo wa kufanya biashara, nchi nyingi za Africa ziligubikwa na privatization miaka ya 90 kwasabab yakukosa uwezo wa kusimama biashara at the same time itafute mapato pia ifanye maendeleo ikawa serikali zinajikuta zinaanza kutafuta pesa kwa ajili ya kuinua viwanda vinavyopata hasara au kuvisaidia Kulipa mikopo ya MA Bank.. Mfumo ili bidi ubadirike serikali iwe Ina regulate mifumo ya biashara zote na baadae kukusanya mapato.....serikali inapokopa inainua huduma za jamii ambayo huchoche uzalishaji na biashara wakikusanya mapato pesa zinaenda BOT.. BOT wanakopesha commercial banks kama( NMB, CRDB) wao ndio hukopesha watu binafsi na makampuni mbalimbali ili yenyewe ibaki na mzigo tu wa kufanya maendeleo ndani ya nchi na sio kufanya biashara moja kwa moja
 
KWA HELA ALIYOIBA YEYE NA GENGE LAKE WALIOKOPA ZINGETUMIKA INGESHAKAMILISHA SASA HIVI IYO SGR KUTOKA DAR HADI MWANZA. KAFA KAONDOKA KAZI ACHA NA AMEMUACHA BRAZA LISSU AKIDUNDA.
Nikuambie uwezo wako wa kujenga hoja humu Jamii Uko chini mno ushauri wa bure penda ku comment vitu vinavyoendana na uwezo wako mdogo wa akili sio lazima u comment kila kitu .Una akili ndogo mno tafuta post za mambo madogo madogo ka comment huko
 
Hakuna nchi Duniani iliyosimama na ahihitaji mikopo.. MAREKANI ni miongoni mwa nchi yenye mikopo zaidi kutoka Bank ya Dunia na wahisani mbalimbali...
Uko sahihi China Ni mmoja wa wakooeshaji wakubwa wa Marekani wakiwemo Brazil, ujerumani, Japan,uingereza, Taiwan,nk lakini pesa wanazokopa marekani hawapeleki kwenye huduma za jamii hata siku moja zinaenda kwenye uzalishaji .Huduma za jamiii Wana fund kwa hela zao za ndani
 
Uko sahihi China Ni mmoja wa wakooeshaji wakubwa wa Marekani wakiwemo Brazil, ujerumani, Japan,uingereza, Taiwan,nk lakini pesa wanazokopa marekani hawapeleki kwenye huduma za jamii hata siku moja zinaenda kwenye uzalishaji .Huduma za jamiii Wana fund kwa hela zao za ndani
Nchi za Dunia ya Tatu hazijafikia wastani wa juu wa maendeleo mpaka zifanye biashara.. kwa sas ni lazima tuboreshe vichocheo vya maendeleo kwanza viwe stable... Miaka ya 80 nchi zote za Africa zilishindwa kuendeleza viwanda vilivyokua Chini ya serikali kwa sababu hio... Ndipo tulipolazimishwa kama utataka mikopo ni lazima ukubaliane na privatization yani uzalishaji ziachiwe sector binafsi na serikali izipe mikopo sector binafsi zenye zichukue mapato then serikali zitumie mikopo kufund projects muhimu kwanza
 
Hoja gani? Aliiba matrillion mikono yake ilijaa damu. KAONDOKA AMETUACHIA mzigo mkubwa wa maden. Tunalipa haya madeni kwa wizi wake. Halaf ujenge hoja, hoja gani hizo UCHWARA?
Nikikuambia akili Huna sitanii hakuna Benki iwe ya ndani au nje Mkopo mkubwa isiofuatilia Kama ulichokopa ndicho unafanya unafikiri Ni sawa na kukopa mtaani kuwa unakopa kujenga SGR au Bwawa la Nyerere halafu hella wanakupa kwenye mabegi you are stupid .Mikopo tu ta elimu ya juu havipewi vyuo au wizara waziri au Raisi analipwa mhusika moja kwa moja na mkopeshaji sembuse mikopo ya Kununua Ndege,SGR na Bwawa ka Mwalimu Nyerere? Wewe akili Huna katafute mada za kiwango chako Cha akili ndogo

Sitachangia mada zako Tena mjinga wewe
 
Ahsante mkuu, ukiongelea hizo nchi za wenzetu walishatuacha kitambo sana.

Mleta uzi amejikita zaidi kwenye hizi nchi masikini nyingi zikiwa bara la Africa.

US mwenyewe sio kwamba hakopi, anakopa ila anaamua akope kwa ajili ya nini na atatumiaje mkopo wake.

Shida hapa sie nchi masikini, unapewa mkopo na kupangiwa namna ya kuutumia huo mkopo.

Mara zote hua nashauri serikali zetu zingetumia muda mwingi kupembua vipaumbele vyao kama nchi kisha waamue wanataka wakope kwa miradi ipi itakayoleta tija.

Uliona wapi tumepigwa kwenye deal la radar na ikaamuliwa kwamba tulipigwa, mnaambiwa mnarudishiwa pesa yenu lakini iende kwenye madawati au kununua vitabu, seriously? Utasema kweli huyo mtu ana nia njema na maendeleo ya nchi yenu?

Kwanini wasiwarudishie tu pesa mkaamua wapi muielekeze kulingana na vipaumbele vyenu?
Viongozi wizara ya fedha hili jibu Kama hamuluelewi kuitendea haki nchi mjiuzulu
 
Back
Top Bottom