Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 360,417
- 829,763
Tumeshajadili kwa mapana sana habari za makafara athari zake na ubaya wake na kwamba ukishaanza hii habari huwezi kuacha utaanza na kafara dogo mpaka kubwa kabisa na mwishowe kila kitu huwa hadharani. Mwisho wa ubaya ni aibu kubwa
Unapotafuta mafanikio kwa maana ya mali nyingi fanya kazi kwa bidii ujuzi na maarifa huku ukiomba kudra za mwenyezi Mungu, usitafute njia za mkato za kuumiza na kuteketeza roho zisizo na hatia kwa manufaa binafsi huu ni uchoyo na kujiona bora kuliko wengine....kama unataka njia ya mkato ya mafanikio isiyo na maneno kubali kutoa damu yako au kiungo chako...kuna wengi wanaishi na madonda makubwa mwilini na wanapeta
Kafara la utajiri ni baya...licha ya laana ya kuteketeza roho zisizo na hatia lakini kila kafara lina kikomo cha matumizi (expire date)
Iko hivi kila kiumbe kina umri wake wa kuishi hapa duniani, na muda ukifika kiumbe hivyo hufa, kwahiyo unapotumia kiumbe chochote kwa kafara unakikatisha maisha yake kabla ya muda wake....kwahiyo kibinadamu kitakufa lakini katika ulimwengu wa roho kitakuwa hai mpaka muda wake ufike ndio kife rasmi.
Hapa ndio huona kila baada ya miaka kadhaa watu hutoa kafara ili kuboost zile nguvu...ubaya wa hili ni kwamba jinsi utajiri unavyoongezeka ndivyo pia aina ya kafara hubadilika yaani kuku, mbuzi, ng'ombe na hatimaye binadamu.
Makafara yanatesa makafara ni mabaya ndio maana ni kawaida kuwaona baadhi ya watu kila wiki au kila mwaka kutoa makafara ya kuchinja wanyama ili kuuhami utajiri wao.
Kafara ni maagano ya kuzimu kama unafikiri kuzimu kunashiba damu umeula wa chuya...kama hujawahi kufanya tafadhali usifanye...kama mambo yanaenda Kombo usiogope wala kukata tamaa siku hazigandi na Mungu yupo utasimama tena.
Usiingie kwenye vifungo na mateso ya milele yenye laana ya damu uliyomwaga iso hatia
Unapotafuta mafanikio kwa maana ya mali nyingi fanya kazi kwa bidii ujuzi na maarifa huku ukiomba kudra za mwenyezi Mungu, usitafute njia za mkato za kuumiza na kuteketeza roho zisizo na hatia kwa manufaa binafsi huu ni uchoyo na kujiona bora kuliko wengine....kama unataka njia ya mkato ya mafanikio isiyo na maneno kubali kutoa damu yako au kiungo chako...kuna wengi wanaishi na madonda makubwa mwilini na wanapeta
Kafara la utajiri ni baya...licha ya laana ya kuteketeza roho zisizo na hatia lakini kila kafara lina kikomo cha matumizi (expire date)
Iko hivi kila kiumbe kina umri wake wa kuishi hapa duniani, na muda ukifika kiumbe hivyo hufa, kwahiyo unapotumia kiumbe chochote kwa kafara unakikatisha maisha yake kabla ya muda wake....kwahiyo kibinadamu kitakufa lakini katika ulimwengu wa roho kitakuwa hai mpaka muda wake ufike ndio kife rasmi.
Hapa ndio huona kila baada ya miaka kadhaa watu hutoa kafara ili kuboost zile nguvu...ubaya wa hili ni kwamba jinsi utajiri unavyoongezeka ndivyo pia aina ya kafara hubadilika yaani kuku, mbuzi, ng'ombe na hatimaye binadamu.
Makafara yanatesa makafara ni mabaya ndio maana ni kawaida kuwaona baadhi ya watu kila wiki au kila mwaka kutoa makafara ya kuchinja wanyama ili kuuhami utajiri wao.
Kafara ni maagano ya kuzimu kama unafikiri kuzimu kunashiba damu umeula wa chuya...kama hujawahi kufanya tafadhali usifanye...kama mambo yanaenda Kombo usiogope wala kukata tamaa siku hazigandi na Mungu yupo utasimama tena.
Usiingie kwenye vifungo na mateso ya milele yenye laana ya damu uliyomwaga iso hatia