Kwanini nashabikia mapinduzi ya UKAWA

Kwanini nashabikia mapinduzi ya UKAWA

Davion Delmonte Jr.

JF-Expert Member
Joined
Oct 27, 2013
Posts
2,149
Reaction score
1,720
Mimi kura yangu ukawa. Hivi nyie mliopigwa upofu. Ni mwaka jana tu serikali ilichakachua katiba pamoja na kugharamia mabilioni yote hayo.

Kimsingi kabisa sio kwamba naipinga kwamba haijafanya chochote CCM.

Ila Kuna mambo ya hovyo na ya hasara yanafanyika kila mwaka kwenye taifa Hili sababu ya hawa watu kulewa madaraka.

Kama kweli tuna dhamira ya utanzania na kujali maslahi ya kizazi kijacho, ni bora watanzania tuungane tufanye sub dakika hii ya themanini CCM apumzike kidogo.

Ama hakika tusipoamua sasa na kupata watu wa kuotesha misingi imara juu ya maslahi yetu ya kitaifa kama utajiri wa asili tulionao.

Hakika huko tunapoenda faida zitazidi kuwa ndogo kuliko madhara.

Ukiangalia mambo yanayotokea duniani kwa sasa ni dhahir kama taifa halitajipanga kwa miaka kumi ijayo hakika wengi watasaga meno.

Tufanye maamuzi sahihi, miaka hamsini hawa watu wametutawala lakini cost zimekuwa kubwa kuliko benefits. Hivi vilio vya kila siku sio bahati mbaya uongozi wa taifa hili haukuwahi kuwa na manufaa yoyote kwa wananchi wa kawaida.

Hata nimefanya simple research ya uchumi wetu tangu enzi za mwalimu hakika hakuna kitu.

Kuna watu wamepigwa upofu lakini watambue pale madhara yanapotokea ni wote tunahathirika.

Hakika hii chance tukipoteza hawa hawa viongozi watu ipo watatuambia si ni wasengerema
 
Mimi kura yangu ukawa. Hivi nyie mliopigwa upofu. Ni mwaka jana tu serikali ilichakachua katiba pamoja na kugharamia mabilioni yote hayo.

Kimsingi kabisa sio kwamba naipinga kwamba haijafanya chochote CCM.

Ila Kuna mambo ya hovyo na ya hasara yanafanyika kila mwaka kwenye taifa Hili sababu ya hawa watu kulewa madaraka.

Kama kweli tuna dhamira ya utanzania na kujali maslahi ya kizazi kijacho, ni bora watanzania tuungane tufanye sub dakika hii ya themanini CCM apumzike kidogo.

Ama hakika tusipoamua sasa na kupata watu wa kuotesha misingi imara juu ya maslahi yetu ya kitaifa kama utajiri wa asili tulionao.

Hakika huko tunapoenda faida zitazidi kuwa ndogo kuliko madhara.

Ukiangalia mambo yanayotokea duniani kwa sasa ni dhahir kama taifa halitajipanga kwa miaka kumi ijayo hakika wengi watasaga meno.

Tufanye maamuzi sahihi, miaka hamsini hawa watu wametutawala lakini cost zimekuwa kubwa kuliko benefits. Hivi vilio vya kila siku sio bahati mbaya uongozi wa taifa hili haukuwahi kuwa na manufaa yoyote kwa wananchi wa kawaida.

Hata nimefanya simple research ya uchumi wetu tangu enzi za mwalimu hakika hakuna kitu.

Kuna watu wamepigwa upofu lakini watambue pale madhara yanapotokea ni wote tunahathirika.

Hakika hii chance tukipoteza hawa hawa viongozi watu ipo watatuambia si ni wasengerema

Sio kwamba hatutaki mabadiliko Tunayataka Sana lakini waliopo Nyuma ya Haya mabadiliko hawapo na nia thabiti Na Tanzania Yetu Wameanza kusema watavunja Muungano kabla hawajaingia madarakani mara watamuachia Babu seya .Sasa imani tutaweka kwa CCM hatuna njia Nyingine
 
Sio kwamba hatutaki mabadiliko Tunayataka Sana lakini waliopo Nyuma ya Haya mabadiliko hawapo na nia thabiti Na Tanzania Yetu Wameanza kusema watavunja Muungano kabla hawajaingia madarakani mara watamuachia Babu seya .Sasa imani tutaweka kwa CCM hatuna njia Nyingine

Sasa mkuu unajua Kuna vitu vingine havina msingi wowote Bali ni formalities tu. Huo muungano unaoulilia ki uhalisia umeshakufa na haupo.

Kama unataka kubaki na CCM unatakiwa utoe hoja zenye mashiko na ujaribu kufikiria kama Kuna kitu kimefanyika na ukanufaika nacho kwa miaka 50 uliyokuwa na CCM.

Jaribu kufikiria na mambo yanayotokea sahiv all kinds of ufisadi na uangalie prospect ya mjukuu wako miaka 50 ijayo. Kama hali ya maisha ya sasa imekuridhisha chaguo lako ni sahihi.

La hujaridhika fikiri mara mbili juu ya kubadilika
 
Hilo ni swahiliw naomba nieleweshwe 1.Muungano una kushidwa nini? 2.mfungwa mmoja na siyo ghaidi alitokea wewe ki uchumi unapata hasara gani? Tuasidie kwa kutupa sababu za msingi ili na sisi tuipigie CCM kwa sababu hakuna mtu yuko perfect 100%
 
Sorry mu unga no una kushidwa nini?mfungwa mmoja akitolewa unapata hasara au faida gani?
 
Sasa mkuu unajua Kuna vitu vingine havina msingi wowote Bali ni formalities tu. Huo muungano unaoulilia ki uhalisia umeshakufa na haupo.

Kama unataka kubaki na CCM unatakiwa utoe hoja zenye mashiko na ujaribu kufikiria kama Kuna kitu kimefanyika na ukanufaika nacho kwa miaka 50 uliyokuwa na CCM.

Jaribu kufikiria na mambo yanayotokea sahiv all kinds of ufisadi na uangalie prospect ya mjukuu wako miaka 50 ijayo. Kama hali ya maisha ya sasa imekuridhisha chaguo lako ni sahihi.

La hujaridhika fikiri mara mbili juu ya kubadilika

Mkuu inaniwia vigumu sana ninapo ona Viongozi wanataka Mabadiliko ili kulipa visasi Sijui kama utakubaliana na Mimi Kwamba pamoja na sababu hizo hapo juu najua Visasi ndio vinataka kuleta mabadiliko hapana hilo Mimi binafsi pamoja na wana ukoo wetu tumelikataa Nadhani kunavijana wapo kwaajili ya mabadiliko bila visasi.Mungu I baridi Tanzania
 
Mkuu inaniwia vigumu sana ninapo ona Viongozi wanataka Mabadiliko ili kulipa visasi Sijui kama utakubaliana na Mimi Kwamba pamoja na sababu hizo hapo juu najua Visasi ndio vinataka kuleta mabadiliko hapana hilo Mimi binafsi pamoja na wana ukoo wetu tumelikataa Nadhani kunavijana wapo kwaajili ya mabadiliko bila visasi.Mungu I baridi Tanzania
sijakuelewa kuhusu visasi. Mi sikuwahi mshabiki wa lowasa wala siasa. Ila ambacho nakiona kina thamani kwa sasa ni sisi nchi kama nchi na sisi raia ambao ni wengi kutathmini haswa tunataka nchi ya namna gani miaka kumi ijayo.
 
sijakuelewa kuhusu visasi. Mi sikuwahi mshabiki wa lowasa wala siasa. Ila ambacho nakiona kina thamani kwa sasa ni sisi nchi kama nchi na sisi raia ambao ni wengi kutathmini haswa tunataka nchi ya namna gani miaka kumi ijayo.

Mambo mengine ya visasi hizo ni hoja mufilisi za hawa viongozi wetu kutafuta huruma ya wananchi akati Kuna mambo ya hovyo hovyo wamefanya.
 
Mpaka sasa sijaona kwanini niipigie kura ukawa??
Ukawa sera yenu ni nini?? Utaambiwa mabaya ya CCM tuuu!!!
Nataka kusikia ukawa mtafanya nini??
 
Mpaka sasa sijaona kwanini niipigie kura ukawa??
Ukawa sera yenu ni nini?? Utaambiwa mabaya ya CCM tuuu!!!
Nataka kusikia ukawa mtafanya nini??

yaani kwa matatizo yaliyopo tanzania bado unaitaji kushwawishiwa? basi subiri ujengewe flyover!
 
Mpaka sasa sijaona kwanini niipigie kura ukawa??
Ukawa sera yenu ni nini?? Utaambiwa mabaya ya CCM tuuu!!!
Nataka kusikia ukawa mtafanya nini??

Inaonesha hauko tayar kusikia na kuelewa ukawa watafanya nini. Ila mambo ukawa waliyoahidi ni mambo ambayo hata wewe unayafahamu.

Usifikiri eti Kuna ahadi zitatoka mbinguni ambazo hazifahamiki. Shida za watanzania zinajulikana hata na mtoto wa darasa la kwanza.

Sasa unaposema ukawa hawana ahadi utakuwa wewe ni kichaa.

Kwani nikuulize tu hizo ahadi walizotoa CCM ni mara ya ngapi kuzitoa? Naona hakuna jipya kama miaka 10 iliyopita kulikua na ahadi ya uhakika wa umeme na mpaka leo Kuna mgao. We unadhani Kuna dhamiri ya kweli ya ccm kutekeleza ahadi?

Suala la wewe kutoona maana ya kuchagua ukawa mimi sinashida nalo. Ila pia inakatisha tamaa sana kwamba miaka kumi iliyopita uliahidiwa maji, elimu, ajira.... Halafu tena mwaka huu unasikia ahadi hizo hizo na wewe unaona ni sawa kabisa
 
Jamani kweli tunahitaji mabadiliko, mimi ni mwalimu niliajiriwa tangu mwezi wa tano na serikali mpaka leo sijapata mshahara wala pesa ya kujikimu. Kituo cha kazi ni mbali na nyumbani nauli ni sh. 45000/= ilibidi likizo ya mwezi wa sita nibaki shuleni maana sikuwa na nauli ya kurudi nyumbani. Nimebaki kuwa omba omba ili niweze kuishi. NI SHIDAAAAA!
 
Mimi kura yangu ukawa. Hivi nyie mliopigwa upofu. Ni mwaka jana tu serikali ilichakachua katiba pamoja na kugharamia mabilioni yote hayo.

Kimsingi kabisa sio kwamba naipinga kwamba haijafanya chochote CCM.

Ila Kuna mambo ya hovyo na ya hasara yanafanyika kila mwaka kwenye taifa Hili sababu ya hawa watu kulewa madaraka.

Kama kweli tuna dhamira ya utanzania na kujali maslahi ya kizazi kijacho, ni bora watanzania tuungane tufanye sub dakika hii ya themanini CCM apumzike kidogo.

Ama hakika tusipoamua sasa na kupata watu wa kuotesha misingi imara juu ya maslahi yetu ya kitaifa kama utajiri wa asili tulionao.

Hakika huko tunapoenda faida zitazidi kuwa ndogo kuliko madhara.

Ukiangalia mambo yanayotokea duniani kwa sasa ni dhahir kama taifa halitajipanga kwa miaka kumi ijayo hakika wengi watasaga meno.

Tufanye maamuzi sahihi, miaka hamsini hawa watu wametutawala lakini cost zimekuwa kubwa kuliko benefits. Hivi vilio vya kila siku sio bahati mbaya uongozi wa taifa hili haukuwahi kuwa na manufaa yoyote kwa wananchi wa kawaida.

Hata nimefanya simple research ya uchumi wetu tangu enzi za mwalimu hakika hakuna kitu.

Kuna watu wamepigwa upofu lakini watambue pale madhara yanapotokea ni wote tunahathirika.

Hakika hii chance tukipoteza hawa hawa viongozi watu ipo watatuambia si ni wasengerema

Kweli nimekusoma na nimeamini wewe ni mshabiki.
Umeandika kishabiki.
Hebu rudia hilo andiko lako uone kama linaweza kumshawishi mwana ccm ahame kambi na kupigia unaposhabikia.
Uchaguzi wa mwaka huu ni wa muhimu na kampeni zake si lelemama au za ushabiki.
Kura zisipotosha usimlaumu mtu.
 
tatizo hapo si UKAWA bali mtu waliomuweka kupeperusha bendera ya ukawa. ccm A kwa ccm B bora ya ccm A.
 
# UKAWA na chadema mmekosa demokrasia ya kweli ndani ya chama, kama mlishindwa kuteua mgombea uraisi kwa kufuata misingi ya kidemokrasia ndani ya UKAWA, mnathubutu vipi kuja kwangu kuniomba kura? Kwa sababu hii siwezi kuwapa kura yangu. Kama alliance imekosa demokrasia, sidhani kuwa mnaweza kuongoza nchi kidemokrasia.
# Kile mlichokuwa mnaimba kila siku majukwaani, mkiongozwa na Dr. Slaa, Lissu, Mnyika na wengine kuhusu ufisadi ambao limekuwa kero kwa wananchi walio wengi, huku mkiaminisha umma kuwa baadhi ya viongozi ndani ya CCM ni mafisafi papaa, leo hamuwezi tena kuwasema, bali mmeungana nao. Hilo ni dhahiri kuwa mpo kimaslahi na sio kulipigania taifa. Ndio wale wale tu hakuna tofauti. Sioni sababu ya kuwapa kura yangu.
# UKAWA haina sera, zaidi ya kuongea kuitoa CCM madarakani, sioni sera wala mkijinadi kwa sera. We need to know what you'll do to the people of this nation, tuna kero nyingi...hatutaki hadidhi za kuuchukia umasikini huku hamna strategies za kuuondoa umasikini.
# Nina wasiwasi na afya ya mgombea wa UKAWA, Mimi sio Mungu lakini ni dhahiri kuwa kiafya Lowassa hayuko sawa, haruwezi kuweka mtu ambaye afya yake ni tatizo, nchi inagitani kiongozi mwenye afya imara ili atumie nguvu, busara, uwezo na ajili zake zote kutuongoza. Kwa sababu hiyo pia, siwezi kumpa kura yangu.
 
Hao ukawa ndo hamna kitu kabisa. Hamna watakacho kifanya zaid ya kuanza kukwapua na kulipa visasi ambavyo havitakuwa na tija yoyote kwa nchi kama nchi.
 
Kweli nimekusoma na nimeamini wewe ni mshabiki.
Umeandika kishabiki.
Hebu rudia hilo andiko lako uone kama linaweza kumshawishi mwana ccm ahame kambi na kupigia unaposhabikia.
Uchaguzi wa mwaka huu ni wa muhimu na kampeni zake si lelemama au za ushabiki.
Kura zisipotosha usimlaumu mtu.
Mimi sio mshawishi mkuu kama wewe upo CCM ni sawa we baki huko.

Ila nachojaribu kusema ni kwamba kwa hali ya hii nchi tangu tupate uhuru mpaka leo narudia tena hasara ni nyingi kuliko faida.

Sikatai kwamba CCM wamefanya mazuri Ila waliyofanya ni kidogo kuliko tuliyoyastahili kulingana na potentiality ya nchi yetu.

Hivo kwa mwenye akili ya kawaida tu. Tunahitaji kubadilika kwanza ili tuone hawa hawa wengine wanaweza kulifanyia nini taifa.

Uzalendo haupimwi kwa mtu kuwa CCM pekee. Hii nchi ni yetu sote hata sisi tunahaki ya kuona Inaenda kwenye misingi iliyonyooka.

Siko kwenye ligi ya kushawishi watu Ila najaribu kusema ni kwanini mimi ntawapa nafasi ukawa
 
Ukawa kipindi cha kina Dr Slaa na professor Lipumba ilikuwa inajulikana inaenda wapi na angalau itafanya nini. Sio hii ukawa ya mtoswa ccm
 
Back
Top Bottom