Tunaopenda mabadiliko tuendelee kupiga kelele mpaka masikio ya baadhi ya watu yafunguke. Hoja za kutoipa CCM kura ziko wazi kabisa. Lakini inasikitisha kuna watu humu hata ungekesha unajenga hoja hawatakuelewa. Ni kama walevi waliopindukia. Wao ni ushabiki tu. Tukiondoka hapa jamii forum wote tunalala gizani, tunakunywa maji ya visima, tunapeleka wagonjwa kwa waganga wa kienyeji badala ya hopspitali, nk. Lakini tunapoongelea mabadiliko, utawasikia baadhi yetu hasa hawa "Mashabiki" wanaanza kupiga ramli kuhusu UKAWA, eti hawana hakika na sera zao, au viongozi wao, nk. Nchi hii itaendelea kuogelea katika lindi la umasikini kwa muda mrefu sana kama tutaendelea kuwa na kundi kubwa la watu wenye fikra hizi. Ni lazima tufike mahali kama sera za serikali tuliyoipa kura hazifanyi kazi kuondoa matatizo yetu, tuikatae serikali hiyo kwa nguvu ya kura zetu. Hiyo ndiyo njia pekee ya kuhakikisha wale tunaowapa mamlaka kupitia kura zetu wanakuwa na nidhamu na kutekeleza kwa vitendo yale wanayoahidi. La sivyo tutaendelea kuishi kwa matumaini mpaka lini?