Kwanini mwanamke avae nusu-uchi halafu aogope kukaa uchi?

Kwanini mwanamke avae nusu-uchi halafu aogope kukaa uchi?

Mtambuzi

Platinum Member
Joined
Oct 29, 2008
Posts
8,809
Reaction score
15,442
Don't+tell+me+how+to+dress+tell+them+not+to+rape.jpg


tcc.JPG


Nakumbuka mwaka 2004 huko nchini Afrika Kusini kulizuka mjadala mkali sana kuhusiana na nguo za nusu uchi, hasa kwa wasichana wa shule. Mjadala huo ambao ulihusisha maoni ya wananchi wakiwemo wale wanaohemkwa pindi waonapo tupu za wanawake, ulizuka baada ya walimu wakuu wa shule mbalimbali za huko kusema nguo fupi zinazovaliwa na baadhi ya wanafunzi wa kike hualika kubakwa.

Unajua ni kwa nini kauli hiyo ya waalimu wakuu wa sekondari nchini humo imezua mjadala? Ni kwa sababu Afrika Kusini inaongoza katika Afrika kwa kasi ya ubakwaji na hata mauaji ya wanawake kwa njia zenye kutia kinyaa.

Wakizungumza na gazeti la Saturday Star la nchi hiyo, waalimu hao, ambao kauli yao hiyo imevifanya vikundi vyenye kutetea haki za wanawake nchini humo kuja juu, walisema, wanaamini uvaaji nao unachangia katika kufanya wanawake wabakwe. Kauli kama hiyo, imekuwa ikipingwa sana na vikundi hivyo nchini humo.

Akizungumza kwa hasira Delphine Serumanga wa taasisi ya kupambana na ufujwaji wa wanawake Afrika Kusini, ya People Against Women Abuse (POWA), alisema, waalimu hao wasitake kuwafanya watu waamini kwamba, wanaume ni binadamu wanaoshindwa kuwa tofauti na mbuzi kwa kuendeshwa na mihemko tu ya miili yao. Amesema, kumbaka mwanamke hakuhusiani kabisa na uvaaji, bali ni zaidi ya hapo. ‘Hata wabakaji wa wanawake, ukiwauliza, watakwambia kwamba, wanabaka kama njia ya kutafuta au kuonesha nguvu, madaraka au uwezo dhidi ya mwanamke. Siyo suala la uvaaji .' Alisema Serumanga.

Lakini waalimu wengi wamesema kwamba, wanapopata kesi ya kubakwa msichana, mara nyingi kama siyo zote, msichana huyo ni lazima atakuwa ni mvaaji wa nguo za nusu-uchi. Wameongeza kusema kwamba, hawajawahi kupata kesi ambapo mbakwaji ni mvaaji wa nguo za heshima. Elizabeth Mnyuku, mkuu wa chuo cha Liberty Community katika mji wa Bramley, alisema, ‘sijawahi kukutana na kesi ya kubaka ambayo msichana alityebakwa ni mvaaji wa nguo za heshima, hapana.'

Aliendelea kusema, mwanafunzi akilalamika kwamba amebakwa au kafanyiwa jaribio la kubakwa, angalia tu namna alivyovaa. Siku zote utabaini kwamba, uvaaji wake ni wa kihasara. Anasema ni vigumu wakati mwingine hata kwa mwalimu wa kiume kufundisha kwa umakini anapokuwa mbele. Wanafunzi wa kike wenye viguo vifupi, huku wakiwa wamepanua mapaja, huwafanya waalimu hao kukosa amani kabisa.

Kuna wakati hata wanafunzi wenyewe wanakosa amani, ambapo inabidi wachukue mikoba ya madaftari na kufunika mapaja yao, wanapogundua kwamba, mwalimu anababaika baada ya kuona mapaja yao. Anasema, hali hiyo huwafanya wanafunzi hao kushindwa kuzingatia masomo kwa hofu ya kwamba watakaa uchi.

Kumekuwa na swali la, ni kwa nini mwanamke avae nguo fupi, halafu aogope tena kukaa uchi. jibu lake limekuwa gumu sana. Siyo kwa Afrika Kusini pekee, hata hapa kwetu huwa tunawaona wanawake wengi , ambao wamevaa nguo fupi sana, lakini wamekuwa wakijitahidi sana kujiziba au kujifunika wasije wakakaa uchi, iwe wakati wa kupanda gari, kuruka mahali au pengine popote ambapo atahitajika kupanua miguu. Utakuta mwanamke kavaa kimini na kitopu, lakini kila saa utamkuta anajitahidi kukishusha hicho kimini na kitopu wakati akitembea barabarani. Je ulivalishwa? Au unaweza kukuta msichana kavaa skin jinzi na blouse au T-Shirt, lakini muda wote mkono uko nyuma akijitahidi kushikilia hiyo blouse au T-Shirt yake isipande na kuonesha kiuno chake. Sasa shida yote hiyo ni ya nini?

CC: Thanda and Thando

BCC: lara 1, gfsonwin, Lisa, charminglady, Nyamayao, marejesho, Preta, Kaunga, BADILI TABIA, King'asti, Paloma, MadameX, Zion Daughter, amu, Angel Msoffe, cacico, Mrembo by Nature, MwanajamiiOne, Madame B, Nivea
 
Last edited by a moderator:
yay 1st reply.
rape is NOT acceptable under ANY circumstances. nguo za wadada zinavutia lakini hazina uwezo wa ku-induce/justify rape. kama huwezi ku-handle then ma.l.a.y.a wamejaa kwa bei chee, watumie hao.
 
hahahaha kwa hiyo mzee unataka wajiachie uwe unatazama bila chenga au unataka wasivae viwanda vya malighafi hiyo vifungwe,mtu mwenye akili timamu huwezi kubaka kwa kisingizio cha mavazi,hizo ni tamaa zako na uzembe wa kushughulisha ubongo.
 
Wewe wasema.....
Ahh mimi nimeisha mbaka huyu aliye kalia kiti cheupe, hata kama sio specification yangu lakini naona kidogo mzuri kuliko hao ulio tuwekea kwenye picture:biggrin:
 
Haaa Haaa Mtambuzi hawa wanawake wanatabia hizi
::
Wanajilazimisha kuwa wengine ili wafanane na taswira za mvuto zilizo akilini mwao! Ukiwaambia walipo hawatakubali ili dhamira yao ya ku-possess all qualities at a go wasizipoteze.
::
Mwanamke mmoja Uingereza niliwahi kumuuliza swali kama hilo kupitia mitandao yetu hii twitter-jibu lake lilikuwa hivi "Men in London are so busy that they forget our existence,,so long as a man is caught by eyes,we automatically found ourselves in min skirts to gain their attention"
::
Nilichojifunza ni kuwa wako radhi wahangaike na kutooneka uchi ila nguo ndefu hadi kisiginoni ng'ooo! Watakupataje ikiwa mwanamke asiposumbuliwa barabarani au asipotazamwa tazamwa anafungua pochi,,anachukua kioo kujitathimini upya.
::
LET WOMEN BE WOMEN,,if we force to understand them we will be confused.
=
 
Last edited by a moderator:
babu zetu kabla waarabu na wazungu hawajatuletea dini pamoja na tamaduni zao walikuwa wanafunika hapo ikulu tuu kwingine kulikuwa wazi kabisa na walikuwa hawabakani.tusisingizie mavazi kwenye uovu acha dada zetu wapendeze.tusilete tamaduni za dini za kiislam na kikristo kuhusu uvaaji na kutaka kila mtu aamini unavyoamini wewe.chunguza kwa umakini kabila lako kabla ya kuja kwa waarabu na wazungu walikuwa wanavaaje.basi ukupata jibu ndio utamaduni wako na utamaduni wa makabila karibia yote ya kiafrika au kama wewe ni mvivu wa kuuliza asili yako angalia baadhi ya makabila wanaodumisha mila zao mpaka leo kama wamasai ,wabarabaig,makirikiri ,wazulu na wengineo wengi wanavaaje?hata wanyama wanatebea hawajavaa nguo lakini hawabakani wana kipindi chao maalumu.
 
ila kiukweli huu uvaaji wa nusu uchi unachangia sana kubakwa hawa mabinti, maana mihemko ya mwanaume rijali inachochewa na kuona sehemu fulani fulani kwa mwili wa mwanamke, sasa hawa madada hizo sehemu zote za mihemko wanaziacha wazi wakati kuna midume mingine ya shoka yenye nguvu ya simba na isiyo ogopa risasi, ina ugwadu wa siku nyingi wa kufa mtu, kila ikitongoza inachomolewa na inakuta hawa mabinti wamejiweka kihasara hasara tena katika angle ambazo zimetulia kulazimisha ulaji wa tunda la mti wa katikati!! nani wa kulaumiwa!!??, ingawaje midume mingine inazidisha ugwadu au nadhani ni imani za kishirikina kubaka vikongwe wa miaka sabini na kuendelea. Ni hayo tu.
 
Nguo fupi ila huoni kitu aiseee hao wadada ni wataalamu kweli!

ehee! Bora umekuja Best lara 1,,hebu nisaidie,,huwa uko kundi hilo,,kama hauko je,ulipowauliza wanasemaje?
 
Last edited by a moderator:
Nguo fupi ila huoni kitu aiseee hao wadada ni wataalamu kweli!
ha ha!! ndio inavyotakiwa. it shud be short enough to be sexy but not enough to be trashy/horish. a simple check is to try bending over na kama bikini haitaonekana then its okay
 
Kukaa uchi si ndio kukuita.
Just wearings
 
yay 1st reply.
rape is NOT acceptable under ANY circumstances. nguo za wadada zinavutia lakini hazina uwezo wa ku-induce/justify rape. kama huwezi ku-handle then ma.l.a.y.a wamejaa kwa bei chee, watumie hao.

Kwa namna yoyote huwezi kuhalalisha ubakaji eti kwa vile msichana kavaa nguo fupi. Kambake mama yako kama nguo fupi ndio kisa! Adhabu yake iwe kunyongwa mpaka kufa! Kama huwezi kuhimili nguo fupi jiue uepukane na adha hiyo!
 
Kwa namna yoyote huwezi kuhalalisha ubakaji eti kwa vile msichana kavaa nguo fupi. Kambake mama yako kama nguo fupi ndio kisa! Adhabu yake iwe kunyongwa mpaka kufa! Kama huwezi kuhimili nguo fupi jiue uepukane na adha hiyo!
we binti mbona unaniwakia kama gesi ya mtwara?! i do NOT support rape, naona ume-quote the wrong person. elekeza hizo hasira kwenye posti 11
 
nusu uchi .ni matangazo Kuwait huduma inapatikana hapa ...
 
watu wanabaka bata na mbuzi sijui nao wamefunikwa nusu uchi....

Anyway siwezi kujibu sana hoja yako...
Mie naamini nguo huvaliwa kutokana na sehemu na sehemu kuna vazi la disco kuna cazi la cokteili kuna la dinner nk....

Pia naamini kuna age na age...kuna age ya kuvaa kata k kuna ya kuvaa vibana ------ na kuna ya kuvaa kawaida....kuna mavazi ya binti chini ya miaka 20...kuna ya 21-30 kuna ya 30's na kuendelea kinachotakiwa ni kujitambua na kujielewa...na mavazi yanaangalia umbo pia......

All in all kwangu mie nguo ikiwa juu ya goti its ok....but itakapofika nusu paja mmmmh inategemea na tukio though nikiwa kwangu ni mwendo wa vibukta.......

Najua sijajibu hoja yako......ntarudi ...lakini naamini nguo sio kigezo cha kubaka
 
Back
Top Bottom