Kwanini mwalimu siku hizi haaminiki?

Kwanini mwalimu siku hizi haaminiki?

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
16,252
Reaction score
16,171
Maagizo ya sasa ni kwamba Kama kuna mzazi ambae anataka kujitolea kutoa mchango wa kuisaidia shule fulani kwenye jambo lolote mchango wake huo upelekwe moja kwa moja na upokelewe na Mkurugenzi. Mwalimu asipokee mchango wowote pale shuleni kwake. Mwaalimu haaminiki tena.

Kwanini mwalimu wa leo haaminiki? kumetokea nini kwa mwalimu mpaka mwl wa leo haaminiki kama zamani pamoja na kumkabidhi watoto wetu awafundishe taaluma na maadili?
 
mwalimu siku hizi ndiye shetwani mkuu!
Hiyo haizekani kuwa hivyo. Mzee Nyerere ni mwalimu, Mzee Mwinyi ni mwalimu, Rais Magufuli ni mwalimu, Mh. Majaliwa ni mwalimu,.... kwavyovyote vile mwl sio shetani, una kitu unakitafuta utakipata.

Tunachosema sisi ni kwanini mwalimu wa leo anafananishwa na mwizi asiyepaswa kushika hela ya mchango wowote? bila shaka kuna ushahidi kuwa hela zinazochangwa na kupokelewa na mwalimu hazifanyi kazi iliyokusudiwa. Kwa nini maadili ya mwalimu yameporomoka kwa kiasi hiki? Zamani mwalimu ndiye aliyekuwa anaaminiwa kwenye jamii kuliko mtu yeyote, leo vipi mwalimu jamii haimuamini tena.

Kwanini mwalimu wa leo anatoza wanafunzi na wazazi michango mingi?
a) ni mwizi anataka kuiba michango ya wazazi na kuitumia kinyume na madhumini ya michango?
b) anataka watoto wapate elimu bora?
c) Ana huruma zaidi kwa watoto kuliko serikali yenyewe?
d) Anaifichia aibu serikali?
e) Kipato kidogo anataka kujalizia kilichopungua?
 
Mwalimu hana thamani tena kwenye jamii hii ya Tanzania hii nikutokana na waheshimiwa kuonshesha dharau kwao. Walimu wanatumika kama nyenzo yakujipatia umarufu na baadhi ya viongozi hapa nchini. Serikali inawanyonya sana kwa kutumia mabavu lakini walimu wamekaa kimya, raia nao wanawaita mashetani. Daaa hii ni dharau iliyokithiri kwao. Mungu akusamehe wewe uliyowaita walimu shetani.
 
Mwalimu siku hizi anakula hadi vitoto vya darasa la kwanza. (Japo siyo wote, nisamehewe tu)


Pia, mwalimu anatumika kuibebe ccm kisha inamtelekeza. Hivyo, kote amekosa heshima na thamani.
 
4d761c67a7f243be571f6e1dc89790b4.jpg
 
Zamani ualimu ulikuwa ni wito siku hizi ni kama tu shughuli nyingine
 
Aisee naamini wewe hujasoma pia huna mtoto, huwezi mwita mwalimu shetani kama amekufundisha na leo unaingia jf, pia unamwachia watoto wako masaa 8
Sihivyo tu, kwa miaka mingi Mwalimu alitumika pia kwenye chaguzi zetu, kampeni na matukio mengine mengi yaliyohitaji watu wanaojua kusoma, kuaandika na kuhesabu kama kuandikisha idadi ya watu, sensa, kuandikisha wapiga kura. Haya ni yale matukio ambayo washiriki watalipwa kidogo.
Kutoaminika huku kwa sasa ni changamoto kwao
 
Hiyo haizekani kuwa hivyo. Mzee Nyerere ni mwalimu, Mzee Mwinyi ni mwalimu, Rais Magufuli ni mwalimu, Mh. Majaliwa ni mwalimu,.... kwavyovyote vile mwl sio shetani, una kitu unakitafuta utakipata.

Tunachosema sisi ni kwanini mwalimu wa leo anafananishwa na mwizi asiyepaswa kushika hela ya mchango wowote? bila shaka kuna ushahidi kuwa hela zinazochangwa na kupokelewa na mwalimu hazifanyi kazi iliyokusudiwa. Kwa nini maadili ya mwalimu yameporomoka kwa kiasi hiki? Zamani mwalimu ndiye aliyekuwa anaaminiwa kwenye jamii kuliko mtu yeyote, leo vipi mwalimu jamii haimuamini tena.

Kwanini mwalimu wa leo anatoza wanafunzi na wazazi michango mingi?
a) ni mwizi anataka kuiba michango ya wazazi na kuitumia kinyume na madhumini ya michango?
b) anataka watoto wapate elimu bora?
c) Ana huruma zaidi kwa watoto kuliko serikali yenyewe?
d) Anaifichia aibu serikali?
e) Kipato kidogo anataka kujalizia kilichopungua?
Tatizo ni moja tuu mkuu,

Siku moja funga chumba chako hafu weka funguo mfuko halafu usahau uone utakavohangaika.


Matatizo mengi mno sasa hivi yanageuzwa changamoto hapo ndipo shinda inpoanzia.
Na utatuzi wa changamoto hizo unahitaji mikakati ya kitaalamu unafanywa na wanasiasa hapo ndipo tatizo linapoanzia.

Mfano: watoto wanamwomba mwalimu wawe wanakula shule mida ile ya kutawanyika kwani wengine wakifika nyumbani hawawezi kusoma tena hasa vidato vy mituhani
Mwalimu kwa busara yake anaitisha kikao cha wazazi kuyasikia maoni ya watoto wao, kweli kikao kinaendeshwa na kukubalina kwamba kila mmoja atachangia kwa ajiri ya mwanae
Kimbembe kinakuja pale mmoj au wengine wanapopata changamoto ya kuikosa michango
Hapo hukimbia kwa diwani ili wote wakose badala ya kukubaliana n wazazi wenzake

Kiukweli sasa hivi wazazi ndio wanaotamani kuwaona walimu wakifukuzwa na pengine kufungwa.

Hiki ni kizazi cha tukose wote,
Mwanangu akikosa mchango wa makubaliano wote wakose badal ya kutumia busara.

Embu fuatilieni michango wanayolalamikia utakuta ni ile waliyokubaliana kuchangia na wakti mwingine anaechangisha hata sio mwalimu ni mtoto mwenyewe.


Hay nimeyaona kwenye shule ambayo mimi ni nimo kwenye kamati ya bodi ya shule hiyo
 
mwalimu siku hizi ndiye shetwani mkuu!
Acha kukurupuka zwazwa mkubwa wewe, jinsi walim wanavyo fight kuhangaika na mitoto ya watu wewe unawaita shetani!!
Utakua hujitambui na huna mtoto unaesomesha.. na kama una somesha yawezekana hujui hata darasa alilopo sasa.
Serikali yako na sera ya elimu bure ndio iliyo sababisha hayo, kuhusu mambo yote ya michango hisiwepo shuleni. Ukizingatia michango mingine ni kwa faida ya wanafunzi.
 
Tatizo ni moja tuu mkuu,

Siku moja funga chumba chako hafu weka funguo mfuko halafu usahau uone utakavohangaika.


Matatizo mengi mno sasa hivi yanageuzwa changamoto hapo ndipo shinda inpoanzia.
Na utatuzi wa changamoto hizo unahitaji mikakati ya kitaalamu unafanywa na wanasiasa hapo ndipo tatizo linapoanzia.

Mfano: watoto wanamwomba mwalimu wawe wanakula shule mida ile ya kutawanyika kwani wengine wakifika nyumbani hawawezi kusoma tena hasa vidato vy mituhani
Mwalimu kwa busara yake anaitisha kikao cha wazazi kuyasikia maoni ya watoto wao, kweli kikao kinaendeshwa na kukubalina kwamba kila mmoja atachangia kwa ajiri ya mwanae
Kimbembe kinakuja pale mmoj au wengine wanapopata changamoto ya kuikosa michango
Hapo hukimbia kwa diwani ili wote wakose badala ya kukubaliana n wazazi wenzake

Kiukweli sasa hivi wazazi ndio wanaotamani kuwaona walimu wakifukuzwa na pengine kufungwa.

Hiki ni kizazi cha tukose wote,
Mwanangu akikosa mchango wa makubaliano wote wakose badal ya kutumia busara.

Embu fuatilieni michango wanayolalamikia utakuta ni ile waliyokubaliana kuchangia na wakti mwingine anaechangisha hata sio mwalimu ni mtoto mwenyewe.


Hay nimeyaona kwenye shule ambayo mimi ni nimo kwenye kamati ya bodi ya shule hiyo
Iko sahihi kabisa!
Yaaani kunawaliowatukana walimu baada ya tamko hili!

Ila wako wanaolilia waendelee kama walivyokubaliana
Kwa upande mwingine, walimu wamefurahi kupaunguziwa masaa ya kukaa shuleni na watoto,
Kuja shule jumamosi, kusahihisha Mitihani mingi,
Kusimamia foleni za chakula!

Yaani ule ushindani wa masomo ulionza kujengeka Unaenda kudorora hadi huruma!
 
Iko sahihi kabisa!
Yaaani kunawaliowatukana walimu baada ya tamko hili!

Ila wako wanaolilia waendelee kama walivyokubaliana
Kwa upande mwingine, walimu wamefurahi kupaunguziwa masaa ya kukaa shuleni na watoto,
Kuja shule jumamosi, kusahihisha Mitihani mingi,
Kusimamia foleni za chakula!

Yaani ule ushindani wa masomo ulionza kujengeka Unaenda kudorora hadi huruma!
Yani sasa hivi mwalimu anafurahi huwezi amini

Kuna mkuu mmoja kaninunulia ka kinywaji kwa furahi. Yani ikifika saa nane anawakumbusha walimu tu ni marufuku kujadili vitu baada ya saa nane na ukirudi kitakachokifuata hatohusika.

Yani watoto wamekosa pa kuanzia, wazazi kila siku wanazunguka.

Jibu moja tu pelekeni kwa mkurugenzi
 
Back
Top Bottom