Sipo hapa kuleta ligi. Mimi ni mkristo, kuwa mkristo haimaanishi hutakiwi kunifunza au kuuliza. Nauliza nijue ili kuamini zaidi badala ya kuamini juu juu tu.
Sihitaji kujua HOW(jinsi gani) hayo nayajua
Sihitaji kujua references (vyanzo), hivyo navijua. Labda viwe vyanzo vinavyoeleza sababu
Nahitaji kujua sababu, sababu ya Mungu kuhitaji sadaka kutoka kwa masikini. Si masikini hana uwezo anaunga-unga kujikimu? Kwa nini asipokee badala ya kutoa?
Umelijenga swali lako katika msingi potofu.
Ni wapi ambapo Mungu amesema anahitaji sadaka ya maskini au ya tajiri?
Hivi unajua sadaka inatolewa kwaajili ya nini?
Yafahamu yafuatayo, hutauliza swali kama hilo tena:
Katika agano la kale, kulikuwa na sadaka za aina nyingi. Ni Walawi pekee ndio waliokuwa wameruhusiwa kula sadaka. Walawi ambao ni descendants wa Lawi, mtoto wa Yakobo, wao ndio waliokuwa wakitoa makuhani. Sadaka haiendi kwa Mungu bali inabarikiwa na Mungu kwaajili ya matumizi ya watumishi wake, ambao hawafanyi kazi ya kujitafutia kipato, bali wameyatoa maisha yao kwaajili ya kumtumikia Mungu.
Hata katika agano jipya, sadaka ndiyo zilizokuwa zikitumika na mitume katika kazi zao za kueneza ujumbe wa Kristo. Kuna wakati, sadaka hizo hizo zilitumika kuwasaidia watu maskini na wale waliokuwa katika dhiki.
Kwa hiyo, swali lako umelitengeneza katika msingi usio sahihi.
Ufahamu tu kuwa kila muumini anastahili kutoa sadaka yake kwa kadiri alivyojaliwa, kwa kadiri ya wema wake, na kwa kadiri ya nia yake. Kiimani, kila sadaka unayoitoa inatakiwa kwenda sambamba na nia yako. Sadaka haitolewi kama mchango.
Sadaka ni kwaajili ya kuhani, mapadre/wachungaji.
Zaka ni kwaajili ya maendeleo ya Kanisa.