Mwacheni amalizie muda wake maana zimebaki siku chache ili bunge livunjwe. Sio mbunge peke yake ambae alishatangaza kuondoka CHADEMA.
Yeye aliondoka sababu kuna ukiritimba na matumizi mabaya ya pesa za chama. Makatibu wa wilaya hawalipwi, wabunge wanalazimishwa kuchangia chama kama vile wanalipia pango la nyumba.
Kuna wabunge zaidi ya wanne wameshatangaza wamehama CHADEMA na watagombea kupitia Nccr Mageuzi mbona hamjataka Spika awatimue bungeni?
Cecil Mwambe alisema amehama CHADEMA na atagombea kupitia CCM kwenda Bungeni kumalizia hizi siku kumi na nane ili avute mpunga wake mnaleta wivu. Mbona nyie watu mna sumu mbaya sana.
Wabunge wenu wameonyesha picha mbaya sana. Wametoroka bungeni baada ya kuweka kibindoni perdiem.
Hivyo mwacheni Mwambe akalie vile viti ambavyo nyie mlivikimbia mkisema vina Corona. Maana alivyoondoka Mwambe ni sawa na Komu na Selasini walivyoondoka.
N.b naweka randama ili wale bichwa maji wa chama flani wapate jibu sahihi.