Kwanini Mkapa hakuzungumzia EPA hadharani

umbeya huo na fitina zenu sasa munataka kumsafisha mkatoliki wenu mkapa kuwa hahusiki na ufisadi!!!!! Wacheni unafiki na kutuletea habari zisizo na chanzo na zenye harufu ya uoga!!!

imekuaje mkapa azungumzie epa akiwa nje ya nchi! Mbona akiwa nyumbani hafungui domo lake na zaidi tunaambiwa tumwache mzee apumzike!!!

habari hiyo imekaa kiumbea umbea na hata alieileta anaonekana amekaa kiumbea umbea!!!!!

Ndugu yangu Zubeda usijadili mambo yenye maslahi kwa taifa kwa kuweka mbele udini! kama mkristu au muislamu kaibia nchi huyo hafai kutetewa iwe kwa dini yake,kabila lake au rangi yake! Fisadi ni fisadi tu awe mkatoliki au mlokole au muislamu au mnyakyusa au mkwere au mhindi au mzungu!

Ukiweka udini tu kwenye mambo ya msingi kama haya unaonyesha jinsi ulivyo na mtindio wa ubongo maana huwezi kufikiri kama binadamu mwenye akili timamu ila fikra zako zinaona dhambi akifanya mtu wa dini ambayo hauko wewe! huu ni ujinga sana najua hata utaenda kupiga kura kwa udini pia!

Unaonyesha huna uchungu wala uzalendo kwa taifa lako bali una uzalendo kwenye affiliation yako ya dini! nimechukizwa sana kuona Dada sijui Kaka Zubeda uko low namna hii!

Tutafika kweli tukiwa na akina Zubeda asilimia 80% katika nchi hii? si tutabaki hapa tulipo milele? Tafakari Zubeda na chukua hatua!
 
great thinker au great stinker?????

karne ya 21 unaongelea ukabila...hii ni unaccepatable stereotyping....

tujaribu kuwa objective kidogo na kuacha kujadili watu!!!!!!

Kha!! Ukabila mbona sijauona hapo!!
 
Akina Zubeda na wengine ndo haswa wadini... Mtu anatoa hoja badala ya kujibu hoja unakuja na sera mbof mbof za udini sijui ukabila.... I am just cant emagine:nono:!! You should change pepo!!!
 
Asubuhi ya jana kidogo nimtwange kofi mama yeyoo (yule muhibu wangu) kisa ka misplace card yangu ya kupigia kura na tukaitafuta kwa masaa zaidi ya mawili. Kwa nini nilitaka kumtwanga? niliona nataka kupoteza fursa muhimu kwangu kama mwajiri, Kumstaafisha kazi Rais aliyeko madarakani sasa hivi hapo tarehe 31.10.2010.
Mamlaka hayo ninayo na ni nadra sana kupata nafasi ya kuyatumia.
 
umbeya huo na fitina zenu sasa munataka kumsafisha mkatoliki wenu mkapa kuwa hahusiki na ufisadi!!!!! Wacheni unafiki na kutuletea habari zisizo na chanzo na zenye harufu ya uoga!!!

imekuaje mkapa azungumzie epa akiwa nje ya nchi! Mbona akiwa nyumbani hafungui domo lake na zaidi tunaambiwa tumwache mzee apumzike!!!

habari hiyo imekaa kiumbea umbea na hata alieileta anaonekana amekaa kiumbea umbea!!!!!

Elimika acha udini hautokusadia!
 
Sijui kwa nini mna fikra potofu namna hii!! Ndo nyie mnatuharibia upinzani nchini kwa ubinafsi wenu.. Sisi tunataka maendeleo ya nchi.. I mean rasilimali za nchi ziwafaidishe watanzania wote si wachache kama ilivyo sasa na itakavyoendelea kama hiki chama cha kifisadi kitaendelea kutawala nchi.

Miaka ya nyuma CUF kilikuwa chama fulan hiv chenye nguvu tukasema yees,, amepatikana wa kuichachafya ccm, watu na ubinafsi wao wakazusha chama cha kidini(uislam).

Sasa hivi CHADEMA wazushi mara ohh udini, mara ukabila... Mhchuuuuy!! I hate this:A S angry:
 
umbeya huo na fitina zenu sasa munataka kumsafisha mkatoliki wenu mkapa kuwa hahusiki na ufisadi!!!!! Wacheni unafiki na kutuletea habari zisizo na chanzo na zenye harufu ya uoga!!!

imekuaje mkapa azungumzie epa akiwa nje ya nchi! Mbona akiwa nyumbani hafungui domo lake na zaidi tunaambiwa tumwache mzee apumzike!!!

habari hiyo imekaa kiumbea umbea na hata alieileta anaonekana amekaa kiumbea umbea!!!!!
Ustaadha, punguza munkari na uchangie ya maana. Article haijazungumzia dini ya mtu kabisa...au unawachukia wakatoliki, watanzania wenzako?
 
Kuna taarifa zinasema kuwa; Mkapa baada ya kusakamwa sana na UFISADI, siku moja akiwa nje ya nchi, alikutana na Mwandishi mmoja ambaye alikwenda huko kwa ajili ya kupokea Tuzo, baada ya kusalimiana walialikana katika Mgahawa na kunywa Chai ambapo Mazungumzo yao baada ya kujuliana hali yalikuwa hivi;

Mkapa: Vipi Siasa za kwetu, hali ikoje.
Mwandishi: Zipo zinaendelea tu.
Mkapa: Hongera kwa kuchukua tuzo, kwani huu ndiyo uandishi niliokuwa nikiusema wakati wa utawala wangu ila hamkunielewa tu.
Mwandishi: Asante. mbona umekuwa kimya sana.
Mkapa: Ahaa! Nimeamua, tena wewe si mwandishi bwana sasa leo nakupa mtihani. naomba Muulizeni Kikwete anaifahamu vipi EPA?
Mwandishi: Kwani ilikuwaje mkuu?
Mkapa: Unajua mie nikiwa Madarakani, Kikwete alikuwa akitambulika ndani ya UWT kwa Codename ya 'Malaika'. Siku Moja kabla ya kuingia katika Uteuzi wa wagombea wa Chama, nilifuatwa na watu wa Usalama na kuambiwa kuwa Malaika atashinda. Sikuwa namtaka awe kiongozi kwa vile nilimfahamu, lakini watu wa Usalama wakaniambia, Mzee hamna namna kwani ameshakamata mfumo wote wa chama na baadhi ya UWT, Jeshi na sekta muhimu, hivyo wakanitaadharisha kwamba iwapo nitamzuia nchi itayumba. Nilishangaa lakini sikuwa na namna zaidi ya kuinusuru nchi, niliwasiliana na wazee katika chama na kuamua kukubaliana nao kuiepusha nchi katika matatizo.
Lakini siki chache baada ya Dodoma kumpitisha Malaika, nilifuatwa na maofisa wake na kuelezwa kuwa Malaika alikuwa akitaka fedha kwa ajili ya kampeni, Ukweli nilimaka, na kuhoji nitazipata wapi. Wakanieleza amesema zipo BoT. Niliamua kumuuliza gavana (Balali) kwa simu, kuwa Chama kilikuwa kikitaka fedha kwa ajili ya Uchaguzi, Balali akajibu hakukuwa na fedha.
Kutokana na majibu hayo Malaika akamfuata Mkapa na kumueleza anajua kila kitu na kwamba kulikuwa na Fedha za malipo ya nje alikuwa akiomba hizo kwa ajili ya kampeni za chama. Nikamueleza Balali ambaye alisema fedha hizo haziwezi kutolewa mpaka kuwepo na doccument, baada ya majibu hayo kufikishiwa Malaika na watu wake walifika na kuwasilisha doccument kwa Balali na kuzitoa fedha hizo.
Mwandishi: Duh...inamaana EPA alicheza Malaika?
Mkapa: Ndiyo maana nakutaka ukipata nafasi muulizeni Kikwete anaijua vipi EPA?
Rais wetu Mkapa najua ulifanya kazi kubwa na kuinua nchi kutoka chini mpaka mahali ambapo si pabaya, na pia nakubaliana na haya maelezo kuwa Malaika amehusika na nilisikia ulishawahi kusema kuwa hutakubali kikwete akuridhi baada yako ukasema over my dead body hivyo ni kweli
 
Kama kweli Mkapa alijua hizo habari akiwa bado Raisi,Kwanini hakukataa kwani kwake uraisi hauna ubia. Pili ikiwa gavana Balali alimtolea nje Kikwete,kwanini Raisi Mkapa akumuunga mkono Gavana Balali na kukataa ufisadi? Hizi habari ni utata mtupu.
 
Utu ni taasisi pana! Taasisi ambayo ndio uti wa mgongo wa maendeleo ya mtu na jamii yake.

Alikuwa JK Nyerere peke yake na sasa, Dr W Slaa ... aliyekuwa anadhubutu Kuusemea Utu na kuuweka kama kigezo cha ustawi wa Taifa!

Bila Utu, ambao ndiyo asili ya Mtu, maendeleo yote hayana maana yoyote! Yanakuwa ni maendeleo ya vitu! Ni utu kwanza...uwe chimbuko la demokrasia na maendeleo ya Taifa.

Utu ni Uungu ndani mtu, hatuwezi kuusaliti tukabaki salama kama watu... lazima utu kutangulia kila nyanja ya jamii bila hivyo hicho kinachoitwa ustawi, maendeleo na demokrasia vinakuwa havina maana.

Maendeleo ya Utu ndio yatawale maendeleo na ustawi wa jamii na taifa, na si maendeleo ya vitu bila kuujali, kuujenga na kuuendeleza utu.

Kitaalam: Utu unanyaushwa, kuharibiwa na kuangamizwa na UFISADI.

Kiua Utu ni Ufisadi. Kauli mbiu ni Utu Kwanza na Si ufisadi Kwanza.

Utu unarutubishwa na haki, upendo, maadili ya uongozi bora, kuheshimiana, haki na usawa wa pato la taifa, matumaini, ukweli, ujasiri na si ukatili, uimara wa kusimamia na kutetea sauti ya umma, utambuzi wa dhana nzima ya utu na kuwaongoza watu kuelekea kilele cha utu wao kama ukombozi wa mwandamu.

Ni Kweli na hakika: CCM na Kikwete wameutupilia mabali Utu ulioasili ya Mtu na kukumbatia kwa kiwango cha kutisha cha Ufisadi. Nani mwenye utu kamili anabishia hili?

Baada ya CCM na Kikwete kusaliti asili ya mtu, kinachofuatia nchini ni Mgawanyiko na Matabaka kwa Taifa. Mgawanyiko na mtabaka hayo vinazaa Udini, ukabila, kuimarisha, ujinga, dhuluma, maradhi nk. Kisa? Utu umewekwa kando, tumeutwika Ufisadi na sasa tumeisaliti asili yetu kama binaadamu. Na kama utu haupo ...ina maana tunatawaliwa na kinyume cha utu...ambacho ni unyama ndani ya Mtu, yaani ufisadi... Na usiombe kuishi ndani ya jamii au Taifa kama hilo! Nani haoni kiama kinachoweza kufuatia hapo?

CCM na Kikwete wana Utu na misingi yake ya kujibu hoja hii? Labda kwanza wawafilisi Mafisadi Papa Kumi (Kumi na Moja) waliowekwa hadharani tayari… Vinginevyo wakati wa kuichai nchi ni sasa!

Kwa kuwa CCM badala ya kupunguza maadui wa ustawi wa maendeleo ya jamii ya watanzania kutoka kuwa wa nne, sasa wanawajenga na kufikia sita. Yaani Ujinga, Maradhi, Umasikini, Ufisadi(Dhuluma), Ukabila na Udini.


Tunahoji: CCM na Kikwete wanacha kujitetea kwenye hili? Mna Utu na Ubinaadamu wa kuhitaji kuliongoza kwa hekima, utulivu na amani Taifa hili kwa kipindi kingine cha miaka mitano? ....Tuwasikie
 
umbeya huo na fitina zenu sasa munataka kumsafisha mkatoliki wenu mkapa kuwa hahusiki na ufisadi!!!!! Wacheni unafiki na kutuletea habari zisizo na chanzo na zenye harufu ya uoga!!!

imekuaje mkapa azungumzie epa akiwa nje ya nchi! Mbona akiwa nyumbani hafungui domo lake na zaidi tunaambiwa tumwache mzee apumzike!!!

habari hiyo imekaa kiumbea umbea na hata alieileta anaonekana amekaa kiumbea umbea!!!!!

Hivi kwa nini mnapenda kukimbilia udini? Mtu yoyote anayekimbilia udini AMEFILISIKA kimawazo
 
Wapo malaika wa aina mbili...wa Nuru na.....

Ni kweli kwa wanaoamini Masuala haya, wapo Malaika wema na wabaya.

Lakini cha muhimu hapa ni kuwa katika mfumo wa kiusalama wanaweza kukuzungumza wewe ukiwa hapo kama hujui alama ama majina wanayotumia usitambue nini kinaendelea. Vivyovivyo hata na polisi, ukisikiliza radio Call zao utasikia EG: wito huu 'Sato Furu' akimaanisha mwito wa kijeshi 'Anga na mbili' mbili inaweza kuwa ni namba ya afisa wa cheo fulani. Kumbe hata wakati Mwinyi ni Rais wake Mkapa alikuwa na Codename yake vivyo hivyo Kikwete ambayo ni Malaika. Jina hili halikuwa likimaanisha uzuri ama ubaya, lilitolewa tu kama alama ya utambuzi.
 
Ustaadha, punguza munkari na uchangie ya maana. Article haijazungumzia dini ya mtu kabisa...au unawachukia wakatoliki, watanzania wenzako?

Mungu akijali ukweli utabaki adharani. Yeshua; mwache Zubeda, Msamehe bure, nadhani ni mfuasi wa Malaika, ila ipo siku na wala haipo mbali Ukweli wa mambo utajulikana kama ni udini ama wizi

Kama kweli Mkapa alijua hizo habari akiwa bado Raisi,Kwanini hakukataa kwani kwake uraisi hauna ubia. Pili ikiwa gavana Balali alimtolea nje Kikwete,kwanini Raisi Mkapa akumuunga mkono Gavana Balali na kukataa ufisadi? Hizi habari ni utata mtupu.

Nadhani kama Mkapa anayauliza haya, anatafuta njia, kwani alikiwa Kiongozi, na alifuatwa, jambo hili ndilo ambalo atapaswa kusimama KIZIMBANI kujibu. pengine alifanya kwa woga wa kuhanggaishwa wakati wa kupumzika. Hapa tunawahitaji wachunguzi makini kutubainishia hili, mbona MEREMETA leo tunaijua wazi.

Kwa vile Mwandishi huyo yupo, na ni mwanachama JF basi natumaini atakuwa Mzalendo kwanza kufafanua na pili kubainisha kama ni ukweli ama laa! Juu ya kile nilichosema.
 
umbeya huo na fitina zenu sasa munataka kumsafisha mkatoliki wenu mkapa kuwa hahusiki na ufisadi!!!!! Wacheni unafiki na kutuletea habari zisizo na chanzo na zenye harufu ya uoga!!!

imekuaje mkapa azungumzie epa akiwa nje ya nchi! Mbona akiwa nyumbani hafungui domo lake na zaidi tunaambiwa tumwache mzee apumzike!!!

habari hiyo imekaa kiumbea umbea na hata alieileta anaonekana amekaa kiumbea umbea!!!!!

I'm glad that you now know who's responsible for all these allegations. No indian was mentioned here. As I've been over and over saying, indians have nothing to do with corruption in this country. We mind our own business and work hard
 
Great thinker au great stinker?????

Karne ya 21 unaongelea ukabila...hii ni unaccepatable stereotyping....

Tujaribu kuwa objective kidogo na kuacha kujadili watu!!!!!!


Rejea maandiko mekundu hapo juu:

Tutambue kuwa kustawisha jamii na kufikia kilele cha juu kabisa cha maendeleo si swala la ushabiki wa hisia na fikra!

Ni uwezo wa Kiufahamu na Kiutu unao tuwezesha kutizama na kuona kinachotakiwa kuonekana na kukifanyia kazi kwa faida ya jamii yote.

Watanzania inabidi tuone chanzo na msingi wa mgawanyiko wetu na kutambua ni nani sasa hivi tayari anafaidi mgawanyiko huo na kwa nini angependa uendelee hata kwa gharama yeyote.

Tuone ni nani anataabika kwa unyonge na kuvuna maumivu ya kutosha kutokana na mgawanyiko huo.

Hivi ni huyo mkristu na muislam aliye fukara, mgonjwa na maskini asiyejua mlo wa siku moja ataupata wapi? Au ni huyo Fisadi aliye kiuka misingi ya uongozi bora na kuruhusu uwekezaji mbovu wa mali ya asili ya Taifa na kuifaidi yeye, familia na marafiki zake?

Hivi wanao faidi mali ya asili ya taifa kifisadi, wametengana kulingana na makabila yao? umewasikia wakigombana kwa udini wao? Umesikia wapi Fisadi wa Kikristu akipipambana na Fisadi wa kiislam, umeona wapi Fisadi waliobobea wakitofautiana katika biashara haramu kwa sababu eti sio wa Kabila moja? au kwa kuwa rangi za ngozi hazilandani? Wameshikana kwa nguvu zote ili hatua za kisheria zisichukuliwe dhidi yao.

Itambulike na kueleweka fika ; Kwa nini iwe sasa baada ya miaka karibu 50 ya Uhuru wa taifa hili swala la ukabila, udini, ukanada nk vinaanza kuonekana kuwa na sauti?

Jibu ni kuwa Taifa la Tanzania halijawahi kufikia katika uongozi wa kifisadi na usio na maadili kama leo. Tanzania haijawahi kuubusu na kuupakata ufisadi kama leo! Uovu wa kuikubali na kuihalalisha rushwa na kuulinda ufisadi uko kileleni.

Chimbuko la nyaraka za Kiislam na Kikristu ni kukomaa kwa ufisadi ulioyumbisha UONGOZI WA TAIFA. Nyaraka na viongozi wa dini zote walifanya hivyo baada ya kuona kuwa Taifa limekuwa ya Tima. Ombwe la uongozi ni kubwa na Jamii ya Watanzania imesahaulika. Ni hakika na ni kweli kuwa kama Hatua madhubuti za kisheria zingechukuliwa dhidi ya mafisadi wakuu wa Taifa hili NYARAKA ZA KIDINI zisingekuwa na nafasi na aibu ya misigano ya kidini na kikabila isingekuwako. Dini zingebaki kuwa dini na siasa zingebaki kuwa siasa kama ambavyo ni jadi ya Watanzania. Lakini hadi leo KAGODA na wenzake wanaburudika na hawana haraka ya kuwaunganisha watanzania kwani mifarakano ya kitaifa inapotokea kwao inakuwa ni CHAKA LA KIJIFICHA NA KUFICHIA MAOVU YAO!!

Kwa sisi tunao dhulumiwa; Si upuuzi tu, bali ni ujinga na uzuzu kuchukulia jibu rahisi la tatizo hili ni Kunyoosheana vidole vya udini na ukabila kwani Fisadi asiye na chembe ya aibu na hekima yoyote hicho ndicho anachotaka Ili kujidumisha katika kuwatumia na kuwatawala wakristu na waislam waliolala na kutawaliwa ufukara, umasikini, usugu wa magonjwa na dhuluma zote na kutokuwa na sauti yeyote juu ya mali na utajiri wa Taifa lao; Nini kitatokea kama dini zote zingeungana na kutaka hatua za kishera dhidi ya EPA, KAGODA nk zichukuliwe. Ni Kiogozi yeyote wa kifisadi atazima jaribio hilo hata kama nchi ikiingia kwnye machafuko ya kidini na kikabila.

TUAMKE;

1. Viongozi wa Kidini waungane na kuwajulisha waumini wao ukweli wa tatizo la kijamii na kuwa jibu si uadui wa kidini wala kikabila ila ni kupwaya kwa uongozi wa juu wa Taifa baada ya udhaifu na uzembe uliopelekea uogozi huo kumezwa na ufisadi. Sasa mafisadi wanaligawa taifa ili wadumu na kushamiri.

2. Tutambue kuwa ufisadi ni uovu na wanao utumia na kuwekeza kwenye ufisadi huo hawatenganishwi na udini, ukabila, ukanda, rangi zao, lugha zao nk. Na itambulike kuwa Fisadi wa kikristu hana uchungu na mkristu wala muislam na fisadi wa kiislm hana huruma kwa muislam wala mkristu. Ufisadi ni Udhalimu uliokidhiri na hauna dini wala kabila katika kufikia malengo yake.

Swali kwanini sisi tunodhulumiwa tunatengwa na kuburuzwa na tunakubaliana kuvunja UMOJA NA MSHIKAMANO WETU?
 
Ngoja Dr. Slaa atinge Ikulu halafu mengineyo yatajitokeza vizuri..wasiwasi wangu Jk ataikimbia nchi...............
 
Ngoja Dr. Slaa atinge Ikulu halafu mengineyo yatajitokeza vizuri..wasiwasi wangu Jk ataikimbia nchi...............

Nasikia na hiyo Hoteli ya Malaika Mwanza ambayo inayodaiwa kumilikiwa na Mhindi mmoja anayeitwa Manoji ni yake kwa Ukumbusho wa Codename yake ya Ikulu ya Malaika.
 
Japo source is occult ukiangalia timing ya EPA, mtiririko wa matukio na uchaguzi wa 2005 waweza tumia bongo kuunganisha lines na kupata mwanga. Nadhani ndo maana JK anapata kigugumizi kuongelea EPA au ufisadi kwa ujumla kwani anajua kuna nini nyuma ya pazia.
Taarifa zaidi zinahitajika.
 
Back
Top Bottom