Kwanini mauaji yamezidi kuongezeka nchini?

Resilience

JF-Expert Member
Jan 4, 2023
888
4,136
Mauaji yamezidi kuongezeka nchini. Matukio ya vifo vya utata vinavyofanywa na wanajamii pamoja na dola vimekuwa vingi. Mapuuza yamezidi kuwa mengi na Mamlaka za uchunguzi zimezidi kutoa ufafanuzi wenye utata kwenye matukio yanayofanywa na dola au wananchi.

Hakuna waziri anayekemea hali hii. Hakuna kiongozi wa dini aliyesimama adharani akasema polisi mmekosea na kuomba au kushauri uchunguzi ufanyike. Hakuna mwanaharakati aliyejitokeza kuonyesha kukerwa na hali hiyo.

Kinachotokea sasa, bila taarifa kuandikwa kwenye mitandao hakuna hatua inayochukuliwa. Na zikiandikwa zisipopata comments nyingi serikali nayo inapuuza.

Nichukue mfano wa kesi ya mwanamke aliyechomwa visu ishirini na tano huko Moshi ambaye amezikwa leo. Jaribu kusikiliza waombolezaji wanavyolalamikia jeshi la polisi then soma taarifa ya msemaji wa jeshi husika. Kuna utata mkubwa na uzembe ila hakuna anayekubali huo uzembe.

Ukimya wa vyombo vya dola sambamba na mawaziri wenye dhamana hauna afya kwa nchi. Mimi siyo mtabiri ila naona wazi upo uwezekano mkubwa ukimya wa mwenye nchi ukaja na tumbua ya kisiasa kutuliza upepo. Tujirekebishe.

Kadri mapuuza yanavyozidi kuathiri jamii kubwa ndivyo chuki inavyoongezeka. Kesho hii inakwenda kuwa agenda kwenye mitaa kwamba serikali imewapuuza wananchi. Uthibitisho utakuwa haya haya tunayoyapuuza leo na chama kitaathirika na chuki hii.

Watu wenye dhamana chukueni hatua.....haipendezi kusikia watu wanatamka adharani kwamba hakuna serikali
 
Nichukue mfano wa kesi ya mwanamke aliyechomwa visu ishirini na tano huko Moshi ambaye amezikwa leo
Kuna mwanamke askari huko Arusha aliyekodi majambazi kumuua mumewe ili aendelee kusagana.

Mm nadhani tatizo kubwa ni hizi NDOA mnazolazimisha kuzifunga ktk zama hizi ambazo ni za "utandauchi". Kwann mnaingia kwenye ndao??

Kataa ndoa uepuke kifo
 
Takwimu sahihi zinatakiwa, inawezekana ni kuwa ndiyo trend ya ripoti za habari Tanzania kuhusu vifo vya kutokana na mauaji kutokana na ukatili wa kijinsia, ushirikina, tamaa ya urithi, tamaa ya mali ndiyo vinabebwa na vyombo vya media na kufuatiliwa sana.

Pia teknolojia ya habari na mawasiliano TEHAMA kupamba moto hivyo taarifa zaidi ambazo hazikuweza kuenea nchi nzima kwa kasi sasa ni rahisi habari hizo kufika maeneo ya mbali na kulipotokea tukio, tofauti labda zamani tukio likiishia habari zake maeneo ya jirani hivvyo kuokuwa habari ya kitaifa ikaishia kuwa habari za mtaa / kijiji ( local news).

Utashangaa kuwa ripoti sahihi za polisi takwimu za maeneo yanayoongoza kwa mauaji ni maeneo yasidhaniwa maana huko huonekana ni shamba na hakuna taarifa zake nyingi ktk media, blogs, vlogs, FB, X n.k :
1 Dec 2020 — Kitengo cha takwimu cha Jeshi la Polisi kinajukumu la kupokea taarifa na ripoti : mchanganuo wa makosa mbalimbali:
2.5.1 Mauaji na Sababu Zake
Makosa ya mauaji hutokana na sababu mbalimbali zikiwemo watu kujichukulia sheria mkononi na visasi. Idadi kubwa ya mauaji ilijitokeza kwenye matukio yaliyohusisha wizi wa kawaida, ujambazi, ugomvi majumbani, imani za kishirikina, wivu/ugoni, visasi na ugomvi vilabuni. Idadi ya matukio ya watu kuuawa ilijitokeza kwa wingi katika mikoa ya Kagera (163), Tabora (152), Dodoma (119), Kigoma (111) na Mwanza (103). (Jedwali Na. 2.13) .
2.2.1 Makosa Dhidi ya Binadamu
Kundi hili linahusisha makosa ya mauaji, kubaka, kulawiti, wizi wa watoto, kutupa watoto, kunajisi na
usafirishaji haramu wa binadamu. Katika kipindi cha Januari hadi Desemba, 2020 jumla ya makosa
11,001 yaliripotiwa ikilinganishwa na makosa 12,223 kwa mwaka 2019. Huu ni upungufu wa makosa
1,222 sawa na asilimia 10.0. Makosa yenye ongezeko kubwa la idadi ni Kunajisi (23), Kutupa watoto
(5) na Usafirishaji haramu binadamu (1). Aidha, makosa yaliyopungua sana kiidadi ni Kubaka (574),
Mauaji (394) na Kulawiti (278) (Jedwali Na. 2.4).......
Source www.nbs.go.tz/ kitengo cha takwimu jeshi la Polisi

MAKALA MAALUM:

Ezekiel Kamwaga
Mchambuzi
23 Februari 2021

Kwa mujibu wa takwimu rasmi za Idara ya Taifa ya Takwimu (NBS), zilizotokana na Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012, zinaonyesha kwamba kwa wastani, Watanzania tisa kati ya kila 1000 hufariki dunia kila mwaka hapa nchini.

Kama tutachukulia kwamba Tanzania ina watu milioni 60 sasa, maana yake mwaka huu ilikadiriwa watu 540,000 watapoteza maisha kwa sababu mbalimbali. Hizi ni takwimu rasmi za serikali.

Lakini, shirika la ujasusi la Marekani, linaeleza kwamba kiwango hicho cha vifo (crude death rate) kinafikia watu saba kwa kila watu 1,000. Kwa sababu hiyo, Tanzania wanakufa watu wachache kwa mwaka kulinganisha na marekani kwa sababu kwa wao, kiwango ni wastani wa watu nane kwa kila wananchi 1000.

Kuna uwiano usio sawa baina ya mkoa na mkoa au mijini na vijijini. Mkoa wa Njombe, kwa mfano, kiwango ni watu 13.5 kwa kila watu 1000. Kwa maana hiyo, kama Njombe ingekuwa ni nchi yenye idadi sawa na ya Tanzania, watu 810,000 wangekuwa wanakufa kila mwaka katika taifa hilo.

Walatini wana msemo maarufu; Mors certa, incerta vita. Kwa tafsiri ya Kiswahili maneno hayo yana maana " kifo ni lazima, kuishi ni bahati". Msemo huu mara nyingi humaanisha kwamba katika maisha ya binadamu, jambo la uhakika zaidi kuliko yote mengine ni kwamba kuna siku mwanadamu ataondoka duniani.

Hata hivyo, wakati vifo vinapotokea kwa watu wengi - maarufu na wasio maarufu na tena katika kipindi kifupi na kwa mfululizo, hilo haliwezi kuwa jambo la kawaida. Na wakati vifo hivyo vinapotokea katika wakati dunia inakumbana na tatizo lililotangazwa na shirika la afya duniani (WHO kuwa ni janga; maswali yanakuwa mengi zaidi.
Ndiyo hali inayoikumba nchi ya Tanzania kwa sasa.

Katika kipindi cha takribani mwaka mmoja kuanzia Machi mwaka jana hadi Februari mwaka huu, kumekuwa na taarifa nyingi za vifo vya watu mashuhuri na wasio mashuhuri. Hata hivyo, vifo vya watu mashuhuri vimetikisa zaidi kwa sababu wengi wao maisha yao yanawagusa watu wengi. Wengine, maisha yao yanagusa nchi kabisa.

Hili ndilo jambo lililosababisha baadhi ya magazeti yanayochapwa kwa lugha ya Kiswahili nchini Tanzania kuandika taarifa zinazoeleza mshtuko uliopo baada ya vifo hivyo. Ni mshtuko kwa sababu kinachotokea sasa hakijawahi kuonekana katika historia ya nchi tangu ipate uhuru wake zaidi ya miaka 60 iliyopita.
Source : BBC Swahili
 
Mwanadam kavurugwa tu

Dunia uwanja wa fujo

Watu hawawezi kutulia

Ova
 
Mauaji yamezidi kuongezeka nchini. Matukio ya vifo vya utata vinavyofanywa na wanajamii pamoja na dola vimekuwa vingi. Mapuuza yamezidi kuwa mengi na Mamlaka za uchunguzi zimezidi kutoa ufafanuzi wenye utata kwenye matukio yanayofanywa na dola au wananchi.

Hakuna waziri anayekemea hali hii. Hakuna kiongozi wa dini aliyesimama adharani akasema polisi mmekosea na kuomba au kushauri uchunguzi ufanyike. Hakuna mwanaharakati aliyejitokeza kuonyesha kukerwa na hali hiyo.

Kinachotokea sasa, bila taarifa kuandikwa kwenye mitandao hakuna hatua inayochukuliwa. Na zikiandikwa zisipopata comments nyingi serikali nayo inapuuza.

Nichukue mfano wa kesi ya mwanamke aliyechomwa visu ishirini na tano huko Moshi ambaye amezikwa leo. Jaribu kusikiliza waombolezaji wanavyolalamikia jeshi la polisi then soma taarifa ya msemaji wa jeshi husika. Kuna utata mkubwa na uzembe ila hakuna anayekubali huo uzembe.

Ukimya wa vyombo vya dola sambamba na mawaziri wenye dhamana hauna afya kwa nchi. Mimi siyo mtabiri ila naona wazi upo uwezekano mkubwa ukimya wa mwenye nchi ukaja na tumbua ya kisiasa kutuliza upepo. Tujirekebishe.

Kadri mapuuza yanavyozidi kuathiri jamii kubwa ndivyo chuki inavyoongezeka. Kesho hii inakwenda kuwa agenda kwenye mitaa kwamba serikali imewapuuza wananchi. Uthibitisho utakuwa haya haya tunayoyapuuza leo na chama kitaathirika na chuki hii.

Watu wenye dhamana chukueni hatua.....haipendezi kusikia watu wanatamka adharani kwamba hakuna serikali
Ajali za barabarani zinazotokana na uzembe zinagharimu maisha kwa mamia, lakini cha kushangaza adhabu ya makosa hayo ni ndogo kuliko adhabu ya mwizi wa kuku!
 
Watu kutekana ni kuona watakosa haki
Mtu unamdai,amekudhulumu unaona ukimpeleka kwenye vyombo vya sheria atakushinda,sasa wewe unaamua kuchukua sheria zako
Mwenyewe

Ukija kwenye domestic violence misukosuko ya kwenye ndoa na mahusiano,huko inaonesha hakuna mapenzi/upendo wa kweli watu wako huko kutumiana tu
Watu wanajali pesa na Mali sana tu

Ova
 
Hayo ni matokeo ya ile sheria iliyopitishwa kuhusu TISS kwamba wakiwa kwenye majukumu yao ikatokea wameua hawatoshtakiwa. Haihitaji mtu aende Shule kujua ni nani ayefanya haya mauaji ya kiholela namna hii. Taifa letu limefika sehemu mbaya sana, kila mtetea haki au anayeonekana ni kikwazo kwa watawala anapotezwa. Jana tu (Peter Madeleka) amelalamika kwamba kuna kikundi cha watu wachache kinataka kumpoteza kwa kile alichosema nikutokana na harakati zake za kutetea haki dhidi ya mfumo.
 
Mauaji yamezidi kuongezeka nchini. Matukio ya vifo vya utata vinavyofanywa na wanajamii pamoja na dola vimekuwa vingi. Mapuuza yamezidi kuwa mengi na Mamlaka za uchunguzi zimezidi kutoa ufafanuzi wenye utata kwenye matukio yanayofanywa na dola au wananchi.

Hakuna waziri anayekemea hali hii. Hakuna kiongozi wa dini aliyesimama adharani akasema polisi mmekosea na kuomba au kushauri uchunguzi ufanyike. Hakuna mwanaharakati aliyejitokeza kuonyesha kukerwa na hali hiyo.

Kinachotokea sasa, bila taarifa kuandikwa kwenye mitandao hakuna hatua inayochukuliwa. Na zikiandikwa zisipopata comments nyingi serikali nayo inapuuza.

Nichukue mfano wa kesi ya mwanamke aliyechomwa visu ishirini na tano huko Moshi ambaye amezikwa leo. Jaribu kusikiliza waombolezaji wanavyolalamikia jeshi la polisi then soma taarifa ya msemaji wa jeshi husika. Kuna utata mkubwa na uzembe ila hakuna anayekubali huo uzembe.

Ukimya wa vyombo vya dola sambamba na mawaziri wenye dhamana hauna afya kwa nchi. Mimi siyo mtabiri ila naona wazi upo uwezekano mkubwa ukimya wa mwenye nchi ukaja na tumbua ya kisiasa kutuliza upepo. Tujirekebishe.

Kadri mapuuza yanavyozidi kuathiri jamii kubwa ndivyo chuki inavyoongezeka. Kesho hii inakwenda kuwa agenda kwenye mitaa kwamba serikali imewapuuza wananchi. Uthibitisho utakuwa haya haya tunayoyapuuza leo na chama kitaathirika na chuki hii.

Watu wenye dhamana chukueni hatua.....haipendezi kusikia watu wanatamka adharani kwamba hakuna serikali
Profiling kwenye jeshi letu la Polisi iko Chini, ma psycho wanapaswa kuwascanned from childhood ' umewahi kujiuliza vipi kama silaha za moto zingekuwa available kama huko SA na USA ingelikuwaje
 
Mauaji yamezidi kuongezeka nchini. Matukio ya vifo vya utata vinavyofanywa na wanajamii pamoja na dola vimekuwa vingi. Mapuuza yamezidi kuwa mengi na Mamlaka za uchunguzi zimezidi kutoa ufafanuzi wenye utata kwenye matukio yanayofanywa na dola au wananchi.

Hakuna waziri anayekemea hali hii. Hakuna kiongozi wa dini aliyesimama adharani akasema polisi mmekosea na kuomba au kushauri uchunguzi ufanyike. Hakuna mwanaharakati aliyejitokeza kuonyesha kukerwa na hali hiyo.

Kinachotokea sasa, bila taarifa kuandikwa kwenye mitandao hakuna hatua inayochukuliwa. Na zikiandikwa zisipopata comments nyingi serikali nayo inapuuza.

Nichukue mfano wa kesi ya mwanamke aliyechomwa visu ishirini na tano huko Moshi ambaye amezikwa leo. Jaribu kusikiliza waombolezaji wanavyolalamikia jeshi la polisi then soma taarifa ya msemaji wa jeshi husika. Kuna utata mkubwa na uzembe ila hakuna anayekubali huo uzembe.

Ukimya wa vyombo vya dola sambamba na mawaziri wenye dhamana hauna afya kwa nchi. Mimi siyo mtabiri ila naona wazi upo uwezekano mkubwa ukimya wa mwenye nchi ukaja na tumbua ya kisiasa kutuliza upepo. Tujirekebishe.

Kadri mapuuza yanavyozidi kuathiri jamii kubwa ndivyo chuki inavyoongezeka. Kesho hii inakwenda kuwa agenda kwenye mitaa kwamba serikali imewapuuza wananchi. Uthibitisho utakuwa haya haya tunayoyapuuza leo na chama kitaathirika na chuki hii.

Watu wenye dhamana chukueni hatua.....haipendezi kusikia watu wanatamka adharani kwamba hakuna serikali
Nakubaliana na wewe mkuu, kunafukuto lingine liko huko mkoa wa Simiyu, polisi wameua kijana mmoja lakini viongozi wanatumia nguvu kubwa kufunika mwanaharamu apite, ni wiki sasa ndugu nao hawataki kuzika mwili wa mpendwa wao.
 
Sio mauwaji yameongezeka sema vyombo vya habari vinavyoripoti matukio vimeongezeka. Matukio hayo huwa yanatokea na polisi huwa wanafika maeneo ya tukio but huwa hawapeleki hizi taarifa kwenye vyombo vya habari mara kwa mara sababu mojawapo ya kazi ya polisi ni kulinda raia sio tu mali zao na raia wenyewe ila pia ni kulinda fikra zao juu ya usalama wao katika jamii wakati wao askari wakifanya kazi bila kuzua taharuki kama hii unayoipata baada ya kusikia matukio machache yamefululiza.

Ukitaka kujua balaa kaa na askari ambaye anadeal na kitengo cha homicide halafu akuonyeshe matukio ya site zao za kazi unaweza hisi ni maigizo. Wanakutana na visa vya ajabu sana kuliko hata hivi mnavyoona kwenye vyombo vya habari.

Haya matukio ya watu kufanyiana ukatili yapo common sana na askari wanajitahidi sana kupambana nayo trust me kwenye jamii watu waovu wapo wengi sana.
 
Back
Top Bottom