Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 18,269
- 33,872
Naitafuta mantiki ya majaji wanaojiuzulu kabla ya wakati wao wa kustaafu kufika kupeleka barua zao za kusudio la kujiuzulu kwa Rais. Ni kwa nini majaji hao wasipeleke barua hizo kwa Jaji Mkuu ambaye ndiye Mkuu wa Mhimili wao badala yake wanapeleka kwa rais?
Mbona yule Mbunge aliyeteuliwa na Rais (Abdalah Possi) alipotaka kujiuzulu kusudio lake hakulipeleka kwa Rais badala yake alilipeleka bungeni? Ni kwa nini basi na hawa majaji wasipeleke kusudio lao kwa Jaji Mkuu na kuridhiwa naye kujiuzulu kisha mamlaka ya uteuzi (Rais) ikajulishwa kwamba kuna Jaji kajiuzulu? Hivi hii si mihimili miwili tofauti inayojitegemea?
Petro E. Mselewa
Mbona yule Mbunge aliyeteuliwa na Rais (Abdalah Possi) alipotaka kujiuzulu kusudio lake hakulipeleka kwa Rais badala yake alilipeleka bungeni? Ni kwa nini basi na hawa majaji wasipeleke kusudio lao kwa Jaji Mkuu na kuridhiwa naye kujiuzulu kisha mamlaka ya uteuzi (Rais) ikajulishwa kwamba kuna Jaji kajiuzulu? Hivi hii si mihimili miwili tofauti inayojitegemea?
Petro E. Mselewa